Yoyo Zhou
Senior Member
- Jun 16, 2020
- 126
- 215
Kampuni kadhaa za Rwanda, zilishiriki kwenye maonyesho ya saba ya kimataifa ya uagizaji wa bidhaa za China (CIIE) yaliyofanyika mjini Shanghai.
Maonyesho hayo ambayo yameandaliwa na Wizara ya Biashara ya China kwa kushirikiana na Shirika la Biashara Duniani (WTO), ni maonesho makubwa zaidi ya kuagiza bidhaa kutoka nje na yamekuwa ni jukwaa kubwa la ununuzi wa kimataifa na kuhimiza uwekezaji.
Rwanda imekuwa ikishiriki kwenye maonyesho hayo tangu yalipozinduliwa mwaka 2018, na kuhimiza watumiaji wa China kuzifahamu bidhaa za Rwanda, pamoja na kutafuta fursa za uwekezaji.
Kwa mujibu wa ubalozi wa Rwanda nchini China, kampuni za Rwanda zilizoshiriki katika CIIE ya mwaka huu ni pamoja na zile zinazotangaza kahawa, pilipili, asali na sanaa za mikono.
Maonyesho hayo ambayo yameandaliwa na Wizara ya Biashara ya China kwa kushirikiana na Shirika la Biashara Duniani (WTO), ni maonesho makubwa zaidi ya kuagiza bidhaa kutoka nje na yamekuwa ni jukwaa kubwa la ununuzi wa kimataifa na kuhimiza uwekezaji.
Rwanda imekuwa ikishiriki kwenye maonyesho hayo tangu yalipozinduliwa mwaka 2018, na kuhimiza watumiaji wa China kuzifahamu bidhaa za Rwanda, pamoja na kutafuta fursa za uwekezaji.
Kwa mujibu wa ubalozi wa Rwanda nchini China, kampuni za Rwanda zilizoshiriki katika CIIE ya mwaka huu ni pamoja na zile zinazotangaza kahawa, pilipili, asali na sanaa za mikono.