Wavulana wapeta matokeo kidato cha Sita, 2014

Wavulana wapeta matokeo kidato cha Sita, 2014

FikraPevu

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2010
Posts
304
Reaction score
236

NECTA.jpg

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha Sita yaliyofanyika Mei, 2014 mwaka huu, ambapo limesema ufaulu umeongezeka kwa jumla ya watahiniwa 30,225 sawa na asilimia 85.73 ambao wamefaulu katika madaraja ya I- III.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumatano Julai 16, 2014 jijini Dar es salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dakta Charles Msonde, amesema kiwango cha ufaulu kwa mwaka huu kimeongezeka kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na kipindi cha miaka iliyopita.

Amesema Wavulana wameendelea kuongoza katika ufaulu wa jumla katika mtihani wa kidato Sita nchini, na kuwa kati ya watahiniwa waliofanya mtihani huo Wasichana waliofaulu ni 12,080 na wavulana waliofaulu ni 26,825.

Amesema jumla ya watahiniwa 41,968 walioandikishwa kufanya mtihani huo wakiwemo wasichana 12,674 (30.20%) na wavulana 29,294 (69.80%), watahiniwa wa shule walikuwa 35,650 ikilinganishwa na watahiniwa 43,231 walioandikishwa kufanya mtihani huo mwaka 2013.

Jedwali lifuatalo linaonesha ufaulu kwa kila daraja kwa watahiniwa wa shule

Soma Pia Matokeo mengine kuanzia 2009
Daraja la UfauluWavulanaWasichanaJumla
IdadiAsilimiaIdadiAsilimiaIdadi Asilimia
I2,2329.201,54114.023,77310.70
II6,17925.463,45231.429,63127.32
III11,86048.874,96145.1516,82147.71
IV3,47414.319468.614,42012.54
05242.16880.806121.74



''Kati ya watahiniwa 41,968 waliosajiliwa kufanya mtihani wa Kidato cha Sita Mei 2014, watahiniwa 40,695 sawa na asilimia 96.97 walifanya mtihani na watahiniwa 1,273 sawa na asilimia 3.03 hawakufanya mtihani na watahiniwa 35,650 waliosajiliwa, watahiniwa 35,418 sawa na asilimia 99.35 walifanya mtihani na kuwa wasichana walikuwa ni 11,022 (99.63%) na wavulana ni 24,396 (99.22%), watahiniwa 232 (0.65%) hawakufanya mtihani'' alikaririwa na FikraPevu.

Hata hivyo, amesema kwa upande wa watahiniwa wa kujitegemea 6,318 waliosajiliwa, watahiniwa 5,277 sawa na asilimia 83.52 walifanya mtihani na watahiniwa 1,041 sawa na asilimia 16.48 hawakufanya mtihani huo kwasababu mbalimbali.

Amebainisha kuwa ufaulu wa watahiniwa katika masomo yote (14) ya msingi umepanda ikilinganishwa na mwaka 2013 na kuwa ufaulu wa juu kabisa ni ule wa somo la Kiswahili ambapo asilimia 99.88 ya watahiniwa waliofanya somo hilo wamefaulu.

Aidha, amesema ufaulu katika masomo ya Sayansi (Fizikia, Kemia, Baiolojia na Hisabati) umeendelea kuimarika kwa kulinganisha na ufaulu wa masomo hayo mwaka 2013.

Shule bora 10
Ametaja shule 10 zilizoongoza kitaifa kuwa ni Igowole ya Iringa, Feza Boys ya Dar es Salaam, Kisimiri ya mkoani Arusha, Iwawa ya Njombe, Kibaha ya mkoani na Marian Girls zote za mkoani Pwani, Nangwa ya mkoani Manyara, Uwata ya Mbeya, Kibondo ya mkoani kigoma na Kawawa iliyupo mkoani Iringa.

Shule 10 zilizofanya vibaya
Aidha, Msonde, ametaja shule ambazo zimefanya vibaya na kushika nafasi ya mwisho kuwa ni pamoja na...

Habari zaidi, soma=>Wavulana wapeta matokeo kidato cha Sita, 2014
 
Safi sana mtoa thread unaweka na picha juu ndio story inanogaaaa
 
tunakoelekea kwenda chuo kikuu itakuwa ni sawa na kutoka darasa la saba kwenda kidato cha kwanza ilivyo sasa.
 
tunakoelekea kwenda chuo kikuu itakuwa ni sawa na kutoka darasa la saba kwenda kidato cha kwanza ilivyo sasa.

Tatizo nn acha vijana wapige shule huoni ss ndo tuna wasomi kiduchu EA na population yetu ni kubwa zaidi yao?
 

NECTA.jpg

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha Sita yaliyofanyika Mei, 2014 mwaka huu, ambapo limesema ufaulu umeongezeka kwa jumla ya watahiniwa 30,225 sawa na asilimia 85.73 ambao wamefaulu katika madaraja ya I- III.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumatano Julai 16, 2014 jijini Dar es salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dakta Charles Msonde, amesema kiwango cha ufaulu kwa mwaka huu kimeongezeka kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na kipindi cha miaka iliyopita.

Amesema Wavulana wameendelea kuongoza katika ufaulu wa jumla katika mtihani wa kidato Sita nchini, na kuwa kati ya watahiniwa waliofanya mtihani huo Wasichana waliofaulu ni 12,080 na wavulana waliofaulu ni 26,825.

Amesema jumla ya watahiniwa 41,968 walioandikishwa kufanya mtihani huo wakiwemo wasichana 12,674 (30.20%) na wavulana 29,294 (69.80%), watahiniwa wa shule walikuwa 35,650 ikilinganishwa na watahiniwa 43,231 walioandikishwa kufanya mtihani huo mwaka 2013.

Jedwali lifuatalo linaonesha ufaulu kwa kila daraja kwa watahiniwa wa shule


[TABLE="width: 570"]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]Daraja la Ufaulu[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, colspan: 2, align: center"]Wavulana[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, colspan: 2, align: center"]Wasichana[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, colspan: 2, align: center"]Jumla
[/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]Idadi[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]Asilimia[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]Idadi[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]Asilimia[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]Idadi[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"] Asilimia
[/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]I[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]2,232[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]9.20[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]1,541[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]14.02[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]3,773[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]10.70[/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]II[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]6,179[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]25.46[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]3,452[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]31.42[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]9,631[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]27.32[/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]III[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]11,860[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]48.87[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]4,961[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]45.15[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]16,821[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]47.71[/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]IV[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]3,474[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]14.31[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]946[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]8.61[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]4,420[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]12.54[/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]0[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]524[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]2.16[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]88[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]0.80[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]612[/TD]
[TD="bgcolor: transparent, align: center"]1.74[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



‘’Kati ya watahiniwa 41,968 waliosajiliwa kufanya mtihani wa Kidato cha Sita Mei 2014, watahiniwa 40,695 sawa na asilimia 96.97 walifanya mtihani na watahiniwa 1,273 sawa na asilimia 3.03 hawakufanya mtihani na watahiniwa 35,650 waliosajiliwa, watahiniwa 35,418 sawa na asilimia 99.35 walifanya mtihani na kuwa wasichana walikuwa ni 11,022 (99.63%) na wavulana ni 24,396 (99.22%), watahiniwa 232 (0.65%) hawakufanya mtihani’’ alikaririwa na FikraPevu.

Hata hivyo, amesema kwa upande wa watahiniwa wa kujitegemea 6,318 waliosajiliwa, watahiniwa 5,277 sawa na asilimia 83.52 walifanya mtihani na watahiniwa 1,041 sawa na asilimia 16.48 hawakufanya mtihani huo kwasababu mbalimbali.

Amebainisha kuwa ufaulu wa watahiniwa katika masomo yote (14) ya msingi umepanda ikilinganishwa na mwaka 2013 na kuwa ufaulu wa juu kabisa ni ule wa somo la Kiswahili ambapo asilimia 99.88 ya watahiniwa waliofanya somo hilo wamefaulu.

Aidha, amesema ufaulu katika masomo ya Sayansi (Fizikia, Kemia, Baiolojia na Hisabati) umeendelea kuimarika kwa kulinganisha na ufaulu wa masomo hayo mwaka 2013.

Shule bora 10
Ametaja shule 10 zilizoongoza kitaifa kuwa ni Igowole ya Iringa, Feza Boys ya Dar es Salaam, Kisimiri ya mkoani Arusha, Iwawa ya Njombe, Kibaha ya mkoani na Marian Girls zote za mkoani Pwani, Nangwa ya mkoani Manyara, Uwata ya Mbeya, Kibondo ya mkoani kigoma na Kawawa iliyupo mkoani Iringa.

Shule 10 zilizofanya vibaya
Aidha, Msonde, ametaja shule ambazo zimefanya vibaya na kushika nafasi ya mwisho kuwa ni pamoja na...

Habari zaidi, soma=>Wavulana wapeta matokeo kidato cha Sita, 2014



kawawa shule yangu nimesoma hapo
 
sina hamu na BRN, matokeo yamechezeshwa kwa SCINCES,, TAMBAZA , IYUNGA. UNBELIEVABLE.,,,hawa vijana wanalazimishwa kwenda kuw walimu kwa mbinde!!
 
Sawa mmefaulu, miaka minne ijayo kazi kupata watapata wachache sana kati yenu
 
wamefaulisha ma arts ambayo ni valueless ktk market,,
thinking criticaly'. Ni siasa tu naiona hapa..
 
Hivi basis ya kuainisha wavulana wameshinda wangapi na wasichana wameshinda wangapi separetely inasaidia nini? Ili wasichana wajione wanyonge wakishindwa na wavulana au wavulana wajione wanyonge wakishindwa na wasichana?? if yes, kwa hiyo tunashindanisha genders?? Ili iweje??
 
Tatizo nn acha vijana wapige shule huoni ss ndo tuna wasomi kiduchu EA na population yetu ni kubwa zaidi yao?
Tatizo huko chuo watadisco tu,labda huko vyuo vya private,yaani elimu inashuka,Mtu anamaliza la saba hajui kusoma eti anafaulu kwenda shule za kata,tunakwenda wapi jamani?
 
Hivi basis ya kuainisha wavulana wameshinda wangapi na wasichana wameshinda wangapi separetely inasaidia nini? Ili wasichana wajione wanyonge wakishindwa na wavulana au wavulana wajione wanyonge wakishindwa na wasichana?? if yes, kwa hiyo tunashindanisha genders?? Ili iweje??

em fikiria kwanza wewe mwenyewe, ukikosa jibu uje tena.
 
Back
Top Bottom