Nyie Wazenji,
Kwanza nakushaurini muwe mnakunywa BIA kama anavyosema Kibunango. Totoz zenu zinapata sana wine ndiyo maana Wabara huwa tunakuja huko kula maisha weekend na nyie mnabaki tu kuumia roho kuwa Wabara wanakuja kwetu kutalii na sisi hizo mbuga za wanyama hatujawahi kufika. Fanyeni kazi, njooni Arusha, Moshi, Serengeti nk mje muone goodtime ilivyo na si kukaa miaka nenda na joto la Zenji huku vikwapa vikitoa maji kama mvua za vuli. Mungu bariki harufu ya karafuu inawasaidia kutosikia harufu.
Juu ya kakisiwa kenu ka Zanzibar, nawakumbusha ule wimbo wa Khadija Kopa wa 'Mwanamke mambo' ambao anaimba "...nishamsomba, nishamsomba, nishamchukua...". Hamna cha kufanya zaidi ya kuwaambia Bwageni-Moyo. Hihiiii, nilikuwa sijui kuwa kumbe Tanganyika tuna kakoloni. This is real very sweet and Mswano kwa sana sana tu.
Mafuta mtaachiwa mchimbe ila kuuza nje ni sisi tutasimamia. Heri msipige sana kelele maana tukishaanza kuzifisadi hela za mafuta tukiongozwa na brother Edo wa Monduli, tutaanza kuimba "walibanaaaaaa...... wameachia."
We love you very much watani wetu wa milele na milele, bila yetu hamuwezi kuishi. Kuna swali? hakuna swali...... utani unaendelea...