Wawekezaji katika Sekta ya Utalii wakaribishwa kuwekeza katika hifadhi ya mazingira asili Kalambo

Wawekezaji katika Sekta ya Utalii wakaribishwa kuwekeza katika hifadhi ya mazingira asili Kalambo

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dunstan Kitandula ametoa rai kwa Uongozi wa Mkoa wa Rukwa kuendelea kushirikiana na Wizara katika kuhamasisha wadau na wawekezaji waliopo katika Mkoa wa Rukwa na nje ya Mkoa huo kuwekeza huduma mbalimbali za kijamii katika Maporomoko ya Kalambo yaliyopo katika mkoa wa Rukwa.

Mhe. Kitandula ameyabainisha hayo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe Josephat Sinkamba Kandege (Mb) aliyetaka kujua Serikali ina mpango gani mahsusi wa kuhakikisha Maporomoko ya Kalambo yanatangazwa kitalii.

Aidha, Mhe. Kitandula aliongeza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuendeleza na kuyatangaza maporomoko ya Kalambo ikiwemo kuboresha miundombinu mbalimbali kwenye hifadhi ya mazingira asilia ya Kalambo na kufanya kampeni za kuyatangaza maporomoko hayo.

Soma Pia: Bodi ya utalii tanzania kuendelea kuutangaza mlima meru


Aidha Mhe. Kitandula alitanabaisha kuwa katika uboreshaji wa miundombinu, Serikali imeboresha barabara; njia za waenda kwa miguu; ngazi za kushuka kwenye maporomoko na kupandisha; miundombinu ya vyoo; mabanda ya kupumzika wageni na eneo la maegesho.

Vilevile serikali imefanya matangazo kwa kutoa makala maalum na kurushwa kwenye televishen lakini pia kumekuwa na uandaaji wa matukio na vifurushi vya misimu maalum ikiwemo kuandaa mabango na vipeperushi na kutumia njia za kidijitali katika kutangaza maporomoko hayo.

Maporomoko ya Maji Kalambo, ni kivutio muhimu cha utalii nchini na barani Afrika kwa ujumla. Maporomoko haya yana urefu wa mita 235 ambao unayafanya kuwa ya kwanza kwa urefu nchini Tanzania na ya pili Barani Afrika baada ya Maporomoko ya Maji ya Victoria
 
Back
Top Bottom