Wawekezaji Mtaani kwetu

NATA

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2007
Posts
4,492
Reaction score
1,313
Uswahili ni kwetu kuna wawekezaji kutoka china.
Jamaa ni balaa wanaharibu miundo mbinu ya kimasikini tuliyo nayo ile mbaya kwani wanapitisha yale maroli yanayobeba macointainer bila huruma na kusababisha barabara kudidimia na kuwa kisiwa kila baada ya nvua kunyesha.

Wanamtaa wote hatuoni faida ya hawa wawekezaji kabisa zaidi wanaleta machungu kwa sisi tunaotumia barabara hiyo.

Serikali inapaswa kuangalia haya mamabo ya wawekezaji kujiamulia mambo mengine yanayo kera raia na kuharibu miundo mbinu yetu
 

Ni malori mangapi kwa wastani yanayoendeshwa na wachina, na mangapi yanayoendeshwa na wasio wachina (ambao pengine nao si watanzania, ila ni weusi)?

Isije ikawa kama magazeti ya shigongo ambaye akiona machinga wa kichina watano, anasema wachina wamejaa. Lakini kukiwa na wasomali au wakenya 20, hamna kinachosemwa!
 
hivi hawa jamaa ni wawezekaji kweli au ujanjaujanja.....
 
hakuna serikali ya mtaa hapo kwenu?? hakuna wajumbe wa shina?? wanafanya kazi gani??? anzia huko
 
hakuna serikali ya mtaa hapo kwenu?? hakuna wajumbe wa shina?? wanafanya kazi gani??? anzia huko

Hivi kama serikali kuu imelala usingizi fofofo inaota ndoto mchana kweupe unategemea serikali ya mtaa-kata-wilaya-mkoa zifanye kazi? Hili ni gumu sana na haliwezi kutokea kwani culture ya utendaji kazi ni kama zilivyo culture zingine huwa zinajengwa top-down na si down-top. So ni maumivu tu mwanzo mwisho.
 

Yote ya hapa mtaani kwetu ni wachina tu hakuna wawekezaji wengine wa kigeni wanaoishi uswahilini kwetu ni hawa ndugu zetu wakwa MAO
 
hakuna serikali ya mtaa hapo kwenu?? hakuna wajumbe wa shina?? wanafanya kazi gani??? anzia huko

Wanagopa hata kuwasogelea, wanawaheshimu au wanawaogopa sijajua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…