Ni sera ya Tanzania Kuvutia uwekeazji wa ndani na wa nje, Tanzania imejaliwa rasilimali nyingi za asili ikiwemo Madini. Kwa bahati mbaya Watanzania wengi tunafahamu madini ya vito kuliko ya viwanda. Mradi huu ni wa maana kwani utaongeza pato la taifa, utaoongeza ajira, na utahamasisha maendeleo kwani Eneo la mradi na maeneo jirani yote yatanufaika.
Watanzania tuache woga, Nchi yetu inaongozwa kwa sheria kanuni na taratibu kwa kila jambo. Si kila uchimbaji wa madini ni mbaya , au ni ufisadi au ni hatari ndo maana tuna mamlaka zilizowekwa kisheria kufanya kazi ya kupembua madahara na faida za kitu chochote katika jamii yetu kabla ya kuanza.
Mradi huu unamilikiwa na watanzania, wachimbaji wadogwadogo ambao wamepewa leseni kwa mujibu wa sheria, na wametafuta wabia watakaofanya nao mradi huu, sawasawa na sera ya serikali ya kuhamasisha ubia kibiashara kati ya serikari na watu/taasisi binafsi.
Kesho ni siku ya mkutano tujitokeze kwa wingi kuunga mkono mradi ili tuanze kunufaika na uuzaji wa madini haya nje ya nchi. Tuwapinge wote wanaoleta siasa kwenye mambo yanayohusu maisha yetu. Magamba oyeeee.