PAMOJA na Tanzania kupanua wigo wa ukuaji wa uchumi, imebainika kwamba asilimia 90 ya ukuaji huo umeshikiliwa na wawekezaji kutoka nje ya nchi.
Hayo yalibainishwa juzi jijini Dar es Salaam na Mhadhiri Msaidizi wa Chuo cha Diplomasia, Abdallah Majura, alipozungumza na Tanzania Daima wakati wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Taasisi ya Uchumi na Jamii (ESRF).
Alisema wawekezaji hao wameshikilia sekta muhimu kama sekta ya madini, ujenzi, ardhi, mabenki pamoja na mawasiliano na kusema kuwa ili uchumi ukue kuna haja ya wazawa kushikilia au kusimamia sekta muhimu nchini. Alisema kutokana na wawekezaji kushikilia sekta hizo kwa kigezo cha kuwekeza, wamesababisha uchumi kuendelea kuporomoka huku maisha ya wananchi nayo yakizidi kudidimia.
"Uchumi wa Tanzania unamilikiwa na wageni kutoka nje ya nchi hasa kwa kuzishika sekta muhimu ambazo zingetumiwa vizuri na wazawa kwa kutumia wataalamu wa ndani zingeweza kuongeza pato la taifa," alifafanua Majura.
Source: Tanzania Daima 27 May 2012
My take: CCM kupitia tamko lake na NEC siku chache zilizopita walisema kuwa serikali iendelee kumiliki njia kuu za uchumi! Sasa kama 90% ya ukuwaji wa sekta muhimu kama madini, matumizi ya ardhi, mabenki na mawasiliono yamo mikononi mwa wageni serikali inamiliki nini?
Hii ni hatari kwa uhai wa taifa na ningeshauri kwenye bunge linalokuja wabunge wazalendo wanaoona hili balaa wapige kelele. Hapa uhuru wa Tanzania hakuna.
Hayo yalibainishwa juzi jijini Dar es Salaam na Mhadhiri Msaidizi wa Chuo cha Diplomasia, Abdallah Majura, alipozungumza na Tanzania Daima wakati wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Taasisi ya Uchumi na Jamii (ESRF).
Alisema wawekezaji hao wameshikilia sekta muhimu kama sekta ya madini, ujenzi, ardhi, mabenki pamoja na mawasiliano na kusema kuwa ili uchumi ukue kuna haja ya wazawa kushikilia au kusimamia sekta muhimu nchini. Alisema kutokana na wawekezaji kushikilia sekta hizo kwa kigezo cha kuwekeza, wamesababisha uchumi kuendelea kuporomoka huku maisha ya wananchi nayo yakizidi kudidimia.
"Uchumi wa Tanzania unamilikiwa na wageni kutoka nje ya nchi hasa kwa kuzishika sekta muhimu ambazo zingetumiwa vizuri na wazawa kwa kutumia wataalamu wa ndani zingeweza kuongeza pato la taifa," alifafanua Majura.
Source: Tanzania Daima 27 May 2012
My take: CCM kupitia tamko lake na NEC siku chache zilizopita walisema kuwa serikali iendelee kumiliki njia kuu za uchumi! Sasa kama 90% ya ukuwaji wa sekta muhimu kama madini, matumizi ya ardhi, mabenki na mawasiliono yamo mikononi mwa wageni serikali inamiliki nini?
Hii ni hatari kwa uhai wa taifa na ningeshauri kwenye bunge linalokuja wabunge wazalendo wanaoona hili balaa wapige kelele. Hapa uhuru wa Tanzania hakuna.