nahisi wazazi wako wanasumbuliwa na ukabila zaidi, hayo mambo siku hizi yamepitwa na wakati, unabidi uwe na msimamo sana katika maamuzi yako. najuwa unawaheshimu sana wazazi wako, na ni haki yao kuheshimiwa, naomba ukae na wazazi wako ongea nao kwa upole na kuwaeleza maamuzi yako, ikishindikana washirikishe ndugu zako wa karibu, nayo ikishindikana wahusishe viongozi wa dini, sikushauri kabisa kuoa mtu usiye mjua wala kumpenda lazima itakuwa ndoa ya machungu, siku nzote upendo huziba mapungufu mengi kwenye ndoa, sasa hiyo ndoa ambayo haina upendo unadhani itahimili misukosuko ya ndoa, au ndio kuachana baada ya muda. sikushauri kabisa huo ujinga wa kuchaguliwa, umeshapitwa na wakati ndugu.