Mbu
Once again, karibu kwenye jukwaa na aksante kwa topic nzuri (na picha).
Kama nimekuelewa vizuri ni kuwa unaulizia hoe do we guide our baby gals kwenye maisha yao yote ya mahusiano. Kama ni hivyo then kumbuka kuwa kwa tamaduni zetu, maisha yetu na maadili yetu watanzania tulio wengi tuna tendency ya kuassume kuwa mabinti zetu ni "watoto" mpaka siku watakapotuletea mimba, magonjwa au taarifa za uchumba ......ile ya .........Mom/Dad ...there is something I want to talk to you, ...kuna wageni wanataka kuja kujitambulisha........ ndo tunashtuka ilhali ukweli ni kuwa wenetu wanakuwa mapema kuliko tunavyofikiria na ni muhimu kuwaweka karibu kama marafiki na si kama watoto.
Ila kabla sijawezajibu hoja yako, ninaomba unisaidie maswali yangu haya ili nijione kama nimeielewa vizuri mada;
1. Kuwazuia/ kuwachunga wasiingie deeply kwenye mahusiano kabla ya 21 (kama tunaweza) au
2. Unazungumzia kuwavusha kwa maana ya kuwamonitor na number, aina na design ya boyfriends anaotoka now ?(assuming anakueleza kila kitu)? au kivipi?
juzi nimetoka ku visit kids skul, nilivyomuona binti yangu(wa mr) ckuamni kama ndio huyo juzi alitoka likizo, next week anakuja likizo nina mpango wa kumweka chini na kuongea nae vizuri mambo ya ujana haswaaa, ile hofu ya kusema tutakuwa tunawakuza watoto kwa kuwaambia mambo ya kikubwa kabla ya umri tunatakiwa tuiondoe sasa na kuwa karibu nao kama marafiki, awe free kwangu niwe free kwake, MJ1 nilishtuka katoto kalivyokuwa karembo!
Mhhh ni mtihani mwingine sana maishani maana hawa watoto wa Dot.Com ni balaa
nafikiri kukaa na binti mhusika na kumwelewesha madhara ya kila hatua ya maisha yake na sio ile biashara ya kuambiwa wanaume ni wabaya
Hii misemo ya wanaume ni wabaya imepitwa na wakati
Mpe elimu hasa ya maisha ambayo itasaidia kumpa uelewa wa kila hatua aanayopitia na sio kuacha mpaka mambo yanakuwa too late ndo unakuja kushtuka na hii ianzie mapema kabisa (sijui nimeelewa )
Umeona eeh nyamayao?! na hivi watoto wetu siku hizi si kama sie ambao muda mwingi tulikuwa na wazazi wetu, wao muda mrefu wanakuwa na marafiki yaani ni mitihani haswa.........lakini kama unaweza kushare na sie nyamayao (pengine itasaidia pia kujibu swali la Mbu) umepanga kuongea naye mambo gani??
Mimi nilishawahikulkaa na binti wa Mr wangu (japo ilikuwa kwa siku mbili tu) kalikuwa katoto ka miaka saba and I was shocked aliponiambia .........Mamiii nikifika eleven nitahakikisha ninae Boyfriend mzuri kama Alehandro (wa kwelye tamthilia) nilijikuta najiuliza maswali ya nianzie wapi ku'zungumza' na huyu bunti but ah.......MUNGU hakupenda nipate jukumu hilo!
MJ1, huyu boyfriend unayemzungumzia ni kijana atakayekuwa anammega matesha wangu, au boyfriend kwa maana ya urafiki wa kawaida?.....Nachelea nisije kuua mtoto wa mtu!Having my daughter nadhani ni vema kwanza kuwa unaelewa na kufahamu kama mzazi
1. Number of marafiki alionao (wa kiume) na aina ya urafiki alionao
2. kama ni boyfriend nafikiri ni vema ukamfahamu (na sometimes ukawa unazungumza naye kwa simu japo salamu - hapa tena ni mtihani wa aina yake maana kama ndo binti anaye jibaba aliye sawa na Babake afu yeye anamwita Boyfriend lol)
3. Kuwa makini pale anapopata matatizo na current boyfriend wake, kuwa karibu na kumconsole kama imefikia break up lakini pia kumwongoza kwenye jinsi ya kuhandle emotional hurt na pia kumguide kuwa asiwe na uharaka wa kutafuta replacement.
Kuna pia namna ya kumguide juu ya madhara ya kuwa na boyfriends wengi kwa umri wake au kubadili boyfriends mara kwa mara kwani kama Mbu ulivyoiweka inachangia kuharibu CV ya mtoto wa kike.
Mie nimeyaorodhesha tu but namna ya kuyatekeleza ni mtihani kwa kweli! inahitaji ukaribu wa hali ya juu kati ya binti na mzazi!
MWJ1 ....SWADAKTAA!
majibu ya maswali yako ndio haswa lengo nia na madhumuni ya mdahalo huu.
Magazeti ya shigongo hayamung'unyi maneno na picha kuonyesha kizazi kinachoteketea, nasi wazazi na wasomaji tupo mstari wa mbele kuwanyooshea vidole mabinti wa wenzetu kukosa adabu, nidhamu na kujiheshimu, ilhali wengine imefikia hatua ya kuwalaumu wazazi wa hao wanaopamba sura za magazeti hayo.
je, sisi kama wazazi....tunakosea wapi? tumeshindwa kukabiliana na kasi ya utandawazi? au ndio tunajivua lawama na kuwatupia kina facebook, sms chats, whatsapp chats nk?
Tunaweza ku control vipi aina ya marafiki wa kike au wa kiume, na temptations nyingine za maisha ya kisasa, ikiwamo outings, sugar daddies, fashions etc...etc...?
MWJ1 ....SWADAKTAA!
majibu ya maswali yako ndio haswa lengo nia na madhumuni ya mdahalo huu.
Magazeti ya shigongo hayamung'unyi maneno na picha kuonyesha kizazi kinachoteketea, nasi wazazi na wasomaji tupo mstari wa mbele kuwanyooshea vidole mabinti wa wenzetu kukosa adabu, nidhamu na kujiheshimu, ilhali wengine imefikia hatua ya kuwalaumu wazazi wa hao wanaopamba sura za magazeti hayo.
je, sisi kama wazazi....tunakosea wapi? tumeshindwa kukabiliana na kasi ya utandawazi? au ndio tunajivua lawama na kuwatupia kina facebook, sms chats, whatsapp chats nk?
Tunaweza ku control vipi aina ya marafiki wa kike au wa kiume, na temptations nyingine za maisha ya kisasa, ikiwamo outings, sugar daddies, fashions etc...etc...?
MJ1, huyu boyfriend unayemzungumzia ni kijana atakayekuwa anammega matesha wangu, au boyfriend kwa maana ya urafiki wa kawaida?.....Nachelea nisije kuua mtoto wa mtu!
GOD FORBID!Hah ODM bwana .......hapana nakushauri ufumbe macho tu na kuashumu kuwa ni boyfriend ambaye ana feelings naye (hawafanyi lol) kwa sababu ukianza kufikiria hayo kweli hutopata ukweli wa Matesha na Mashanga Babu. Assume hajawahi hata kufunua goti. Ingawa ukweli ni kuwa siku hizi Binti wa miaka 18- 20 uwezekano wa yeye kujaribu japo mara moja ni mkubwa kuliko tunavyowafikiria, ingawa wapo ambao bado ni strong kutokana na malezi.
Having my daughter nadhani ni vema kwanza kuwa unaelewa na kufahamu kama mzazi
1. Number of marafiki alionao (wa kiume) na aina ya urafiki alionao
2. kama ni boyfriend nafikiri ni vema ukamfahamu (na sometimes ukawa unazungumza naye kwa simu japo salamu - hapa tena ni mtihani wa aina yake maana kama ndo binti anaye jibaba aliye sawa na Babake afu yeye anamwita Boyfriend lol)
3. Kuwa makini pale anapopata matatizo na current boyfriend wake, kuwa karibu na kumconsole kama imefikia break up lakini pia kumwongoza kwenye jinsi ya kuhandle emotional hurt na pia kumguide kuwa asiwe na uharaka wa kutafuta replacement.
Kuna pia namna ya kumguide juu ya madhara ya kuwa na boyfriends wengi kwa umri wake au kubadili boyfriends mara kwa mara kwani kama Mbu ulivyoiweka inachangia kuharibu CV ya mtoto wa kike.
Mie nimeyaorodhesha tu but namna ya kuyatekeleza ni mtihani kwa kweli! inahitaji ukaribu wa hali ya juu kati ya binti na mzazi!
Mie ninachoona hapa wazazi tunapaswa kuwa na muda zaidi na watoto wetu ,tujenge mazingira ya kuwa rafiki na binti zetu ili hata pale mtoto anapokuwa na jambo linamtatiza anakuwa free kuja kuongea na wewe kama mzazi bila woga ,
Pia nadhani pale tunapoona mtoto anakuwa inabidi tuanze kumpa mafunzo madogo madogo yanayohusiana na ukuaji ,Mazingira yanayotukabili,Hili janga la ukimwi ,kwa ujumla anatakiwa kusikia kutoka kwa mzazi,mafunzo yanayoendana na umri alionao kwa wakati huo na kila anavyoendelea kukua bado anahitaji ukaribu na ushauri wa wazazi.
Kuna jambo liliwahi kunitokea nikiwa na 14-16 years sikuweza kuongea na mama ama mtu awaye yote kwani niliogopa na siku zote sikuwa nimejengewa mazingira ya kufanya hivo..nilikuwa namuogopa mama yangu na hivi alikuwa ticha kwa kipindi hicho...yaani ndo nilikuwa nachanganyikiwa kabisa
Hivo sitaki mtoto wangu apate wakati mgumu kuelezea hisia zake kwangu..napenda awe free kabisa
nilivyomuona nilihic tayari kameshavunja ungo may b matron kasahau kunical kuniambia coz nilishamuomba ikitokea hivyo anical mapema iwezekanavyo, ikawa bado, ndio pakuanzia hapo....hiyo week mitoko mie na yeye itakuwa mfululizo, hapo nitaanzia mbali kidogo (story za skul) mpaka nitaingia kwenye ishu ya kukua, awali nilimwambia matron anijulishe, sasa nikishaongea nae mwenyewe itakuwa jukumu lake kunijulisha itakapotokea, nitamweleza kila step anayotakiwa aichukue kwenye hiyo c2ation kama itamkutia skul( i wish imkutie home)....2kivuka hiyo step ndio ntakuja kumwelezea hayo mengine ya kujitambua yeye kama binti na c mtoto tena na kuingia kwenye ishu za mahusiano sasa!
Hapa mimi baba wa mabinti wawili wazuri sana, acha nikae kimya nipate darasa.
Ahsate moskwito kwa hii yuziful sredi. Ntaiprinti nimpelekee mama matesha naye apate maujuzi.
Niko nawasomeni jamani, msichakachue.
Suala la malezi ni jambo gumu sana hasa watoto wanapokua na kubalehe nadhani presha zinazidi kipindi hiki.
Kama mzazi inabidi u-play your part, ongea na muelimishe mwanao pia muda mwingine uwe na misimamo kwenye maamuzi yako..Kuwasiliana na mtoto isiwe mpaka siku amekosea au laa, bali iwe muda wote ili mradi uhakikishe kila ushauri ulionao umemshirikisha mwanao.
Mwisho wa siku, tuwaombee watoto wetu nao wawe na upeo wa kuchambua mambo na kuacha kufuata mikumbo au kutaka kujaribu kila kitu kisa fashion n.k.
Hali ya maisha na mabidiliko kiujumla kama teknolojia inachangia sana kuharibu watoto kwa upande mwingine!!