Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Mnakumbuka ile story ya wale vijana watano waliotekwa Desemba 2021 kule Kariakoo.
Hivi karibuni wazazi wa vijana hao wamejitokeza tena kuomba msaada kwani mpaka sasa hakuna kitu kimefanyika ili kujua vijana hao walipo.
================================================
Miaka mitatu ikiwa imepita hadi sasa tangu vijana watano wapotee katika mazingira tata Kariakoo jijini Dar es Salaam, wazazi na ndugu wa vijana hao wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan aingilie kati suala hilo.
Hii ni makala fupi iliyoandaliwa na Global Online TV wakiwahoji wazazi wa vijana hao.
"Mmoja ya wazazi wa vijana hao amesema kuwa kuna kipindi walipata taarifa kutoka kwenye kituo kimoja cha haki za binadamu Tanzania kuwa ripoti nzima ya kutoka kwa vijana hao imekamilika na Jeshi La Polisi wanayo"
Walipojaribu kufuatilia kwa IGP Camillus Wambura kuhusu ripoti na majibu ya wapi walipo vijana hao, waliambiwa waende Central Police, walipoenda waliambiwa mpelelezi wa kesi hiyo ameamishwa na wakapewa mpelelzi mpya ambaye alifungua upya jalada la uchunguzi
Mnakumbuka ile story ya wale vijana watano waliotekwa Desemba 2021 kule Kariakoo.
Hivi karibuni wazazi wa vijana hao wamejitokeza tena kuomba msaada kwani mpaka sasa hakuna kitu kimefanyika ili kujua vijana hao walipo.
================================================
Miaka mitatu ikiwa imepita hadi sasa tangu vijana watano wapotee katika mazingira tata Kariakoo jijini Dar es Salaam, wazazi na ndugu wa vijana hao wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan aingilie kati suala hilo.
Hii ni makala fupi iliyoandaliwa na Global Online TV wakiwahoji wazazi wa vijana hao.
"Mmoja ya wazazi wa vijana hao amesema kuwa kuna kipindi walipata taarifa kutoka kwenye kituo kimoja cha haki za binadamu Tanzania kuwa ripoti nzima ya kutoka kwa vijana hao imekamilika na Jeshi La Polisi wanayo"
Walipojaribu kufuatilia kwa IGP Camillus Wambura kuhusu ripoti na majibu ya wapi walipo vijana hao, waliambiwa waende Central Police, walipoenda waliambiwa mpelelezi wa kesi hiyo ameamishwa na wakapewa mpelelzi mpya ambaye alifungua upya jalada la uchunguzi