Wazazi wako walikuonyesha mapenzi kihisia au walitimiza majukumu yao ya kimsingi kama chakula, mavazi, na makazi basi?

Wazazi wako walikuonyesha mapenzi kihisia au walitimiza majukumu yao ya kimsingi kama chakula, mavazi, na makazi basi?

Mshangazi dot com

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
1,345
Reaction score
3,503
Je, wazazi wako walikua na ukaribu na wewe, walikutia moyo, waliongea na wewe pale ulipohitaji, walitenga muda kwa ajili ya kufanya vitu pamoja na wewe au upendo wao ulionyeshwa kwa kutimiza majukumu yao ya kimsingi na kutilia mkazo nidhamu zaidi (baba au mama akifika nyumbani kila mtu anatetemeka).

Umejifunza nini kutokana na wazazi wako walivyokulea na unapanga kuwalea vipi watoto wako?

Familia 1.jpg
 
Unakuwaje na mapenzi ya kihisia kwa mwanao?! Uhuni wa namna gani huu?! Wewe mshangazi vipiii? Wazazi wanakuwaga na upendo kwa watoto wao siyo mapenzi ya kihisia😡😡😡😡
 
Wote walikua wananipenda sana na mimi nikawa nawapenda ila nilipofika miaka 14 mzazi mmoja akamfanyia kosa mzazi wangu mwingine kosa la dhahiri lililonifanya nimchukie sana huyo mzazi wangu aliefanya kosa hilo maana Impact yake ilikua mbaya sana hadi kwangu.

kwenye moyo wangu akawa adui nisietaka hata kumuona, ila nilipofika miaka 18 yule mzazi naempenda ambae ndie aliekosewa aligundua sitaki kuskia stori ya mzazi wangu mwingibe kwahiyo akanishauri sana kwa zaidi ya mwaka mzima kuwa nimpende sana huyo mzazi wangu mwingine na nisamehe kwa sasa nipo nao sawa wote.

Nimejifunza kuwa uadui haurithishwi
 
Unakuwaje na mapenzi ya kihisia kwa mwanao?! Uhuni wa namna gani huu?! Wewe mshangazi vipiii? Wazazi wanakuwaga na upendo kwa watoto wao siyo mapenzi ya kihisia😡😡😡😡
Soma na nyuzi basi siyo kichwa cha habari tu. Mapenzi na watoto
 
Ningependa kusikia kutoka kwenu Nomadix , makutupora , Anastasia21 , realMamy , Demi , Intelligent businessman min -me , mshamba_hachekwi


Pendaelli , siwezi kukuangusha kwenye daily maswali 😂
Wazazi wangu walionyesha upendo na pia kutimiza majukumu, sikuwahi kuhisi kupungukiwa chochote kile katika maisha yangu yote hadi namaliza chuo kikuu.

Baba yangu alikuwa mtu wa upendo mno mwenye hofu ya mungu, alisisitiza nidhamu lakini si kwa ubabe na hatukuwa tunamuogopa bali tunamuheshimu.

Mama yangu bana na yeye ni mtu mzuri tu ila ameninyoosha sana kwa fimbo na kwa kufanya kazi, ni yule mama ambaye ilikuwa ukikaa nae hata dakika mbili lazima akupe kazi ya kufanya so tulikuwa tunakimbia kukaa nae karibu maana ataibuia kazi usiyoitarajia.
Tukisikia anasafiri tunaruka kwa furaha lakini baada ya siku mbili tu tunamkumbuka tunatamani arudi.
Sasa hivi nimekuwa mkubwa namshukuru sana mama yangu kwa kuwa vile alivyokuwa maana hakuna kazi inayonishinda, naishi mazingira yoyote..ya raha na ya shida pia ninao huo uvumilivu.

Sasa hivi mama ni mshkaji sana tunapiga mastori, nikienda home sifanyi kazi labda niamue mwenyewe😅.

Sikuwahi kukosa upendo, sikuwahi kukosa chakula, nguo, wala mahitaji ya shule.
Kiufupi mimi.mwenzenu nilikuwa mtoto wa kishua..ila kwenye upande wa kufanya kazi nimefanya kama watoto wa kijijini.
 
Wote walikua wananipenda sana na mimi nikawa nawapenda ila nilipofika miaka 14 mzazi mmoja akamfanyia kosa mzazi wangu mwingine kosa la dhahiri lililonifanya nimchukie sana huyo mzazi wangu aliefanya kosa hilo maana Impact yake ilikua mbaya sana hadi kwangu.

kwenye moyo wangu akawa adui nisietaka hata kumuona, ila nilipofika miaka 18 yule mzazi naempenda ambae ndie aliekosewa aligundua sitaki kuskia stori ya mzazi wangu mwingibe kwahiyo akanishauri sana kwa zaidi ya mwaka mzima kuwa nimpende sana huyo mzazi wangu mwingine na nisamehe kwa sasa nipo nao sawa wote.

Nimejifunza kuwa uadui haurithishwi
Somo zuri sana "Uadui haurithishwi" hasa kwa wazazi na watoto.
 
Unakuwaje na mapenzi ya kihisia kwa mwanao?! Uhuni wa namna gani huu?! Wewe mshangazi vipiii? Wazazi wanakuwaga na upendo kwa watoto wao siyo mapenzi ya kihisia😡😡😡😡
Tatizo unawaza kukojoa tu,unajua hisia wewe,yaan mapenzi Yale indeep...
Ndivyo tunavyowapenda wanetu...
Yaan zile hisia za ndani kabisa...aisee,sikia tu..watoto 😘😘😘
 
Wazazi wangu walionyesha upendo na pia kutimiza majukumu, sikuwahi kuhisi kupungukiwa chochote kile katika maisha yangu yote hadi namaliza chuo kikuu.

Baba yangu alikuwa mtu wa upendo mno mwenye hofu ya mungu, alisisitiza nidhamu lakini si kwa ubabe na hatukuwa tunamuogopa bali tunamuheshimu.

Mama yangu bana na yeye ni mtu mzuri tu ila ameninyoosha sana kwa fimbo na kwa kufanya kazi, ni yule mama ambaye ilikuwa ukikaa nae hata dakika mbili lazima akupe kazi ya kufanya so tulikuwa tunakimbia kukaa nae karibu maana ataibuia kazi usiyoitarajia.
Tukisikia anasafiri tunaruka kwa furaha lakini baada ya siku mbili tu tunamkumbuka tunatamani arudi.
Sasa hivi nimekuwa mkubwa namshukuru sana mama yangu kwa kuwa vile alivyokuwa maana hakuna kazi inayonishinda, naishi mazingira yoyote..ya raha na ya shida pia ninao huo uvumilivu.

Sasa hivi mama ni mshkaji sana tunapiga mastori, nikienda home sifanyi kazi labda niamue mwenyewe😅.

Sikuwahi kukosa upendo, sikuwahi kukosa chakula, nguo, wala mahitaji ya shule.
Kiufupi mimi.mwenzenu nilikuwa mtoto wa kishua..ila kwenye upande wa kufanya kazi nimefanya kama watoto wa kijijini.
Inawezekana you are my lost baby sister, my childhood was identical 😂 😂 😂
 
Binafsi wazazi wangu walikua wakali ila Babà alizidi. Akirudi hujalala saa 3 usiku ni kesi ya jinai. Mchana akirudi kazini saa 9 hujalala ni kosa kubwa sana kwake,kuamka saa 11 jioni

Niwashukuru sana kwa mahitaji ya shule na kila kitu tulipata ila muda wa kukaa na sisi ilikua nadra sanaa.
Badae mama alibadilika akawa anazungumza na mimi kwa baadhi ya mambo.
Nakumbuka nikiwa form six alikua ananipigia simu sana kila weekend.

Kuna siku nilipomaliza form six mama aligundua Nina mahusiano na bint flan hivi mtaani,alinikalisha usiku saa 7 na kuzungumza kuhusu tabia za yule binti ambazo sio nzuri akaniomba niachane nae.

Hii ilinijenga sana,mzee nae akakazia nilichoambiwa na Mama aliponitoa kwenda matembezini na yeye.

Matokeo yalitoka nilifaulu vizuri sana(Hili namshukuru sana Mungu)
nimeona niliseme hili sababu kuna kitu cha kujifunza hapa, nilijifunza wazazi wanalipwa na furaha sana mtoto wao akifaulu,wanasikia faraja kutembea sababu yako.Kuna namna thamani yangu ilipanda mtaani,tulikua kota za kampuni flan hivi morogogo,walimu walionifundisha shule ya msingi waliniomba niwafundishe jioni, wengi walikua wanatafuta credit na kujiendeleza kielimu.Ilinifanya Niongeze viwango vya nidhamu yangu mtaani

Wajomba zangu jitahidini msituamgushe tumiwalipia Ada.

Watoto wangu nazungumza nao sana kwa ukaribu nijue walau changamoto zao za kila siku nikipata nafasi.
Napenda kujua ndoto za wanangu na vipaji vyao nizifanyie kazi mapema ilizimee na kuzaa matunda mazuri kwa Neeema na Baraka za Mungu.
 
Binafsi wazazi wangu walikua wakali ila Babà alizidi. Akirudi hujalala saa 3 usiku ni kesi ya jinai. Mchana akirudi kazini saa 9 hujalala ni kosa kubwa sana kwake,kuamka saa 11 jioni

Niwashukuru sana kwa mahitaji ya shule na kila kitu tulipata ila muda wa kukaa na sisi ilikua nadra sanaa.
Badae mama alibadilika akawa anazungumza na mimi kwa baadhi ya mambo.
Nakumbuka nikiwa form six alikua ananipigia simu sana kila weekend.

Kuna siku nilipomaliza form six mama aligundua Nina mahusiano na bint flan hivi mtaani,alinikalisha usiku saa 7 na kuzungumza kuhusu tabia za yule binti ambazo sio nzuri akaniomba niachane nae.

Hii ilinijenga sana,mzee nae akakazia nilichoambiwa na Mama aliponitoa kwenda matembezini na yeye.

Matokeo yalitoka nilifaulu vizuri sana(Hili namshukuru sana Mungu)
nimeona niliseme hili sababu kuna kitu cha kujifunza hapa, nilijifunza wazazi wanalipwa na furaha sana mtoto wao akifaulu,wanasikia faraja kutembea sababu yako.Kuna namna thamani yangu ilipanda mtaani,tulikua kota za kampuni flan hivi morogogo,walimu walionifundisha shule ya msingi waliniomba niwafundishe jioni, wengi walikua wanatafuta credit na kujiendeleza kielimu.Ilinifanya Niongeze viwango vya nidhamu yangu mtaani

Wajomba zangu jitahidini msituamgushe tumiwalipia Ada.

Watoto wangu nazungumza nao sana kwa ukaribu nijue walau changamoto zao za kila siku nikipata nafasi.
Napenda kujua ndoto za wanangu na vipaji vyao nizifanyie kazi mapema ilizimee na kuzaa matunda mazuri kwa Neeema na Baraka za Mungu.
Asante sana kwa kushare, tumepata jambo la kujifunza.
 
Back
Top Bottom