Wazazi wangu wanataka kuachana, nifanyeje?

Pole sana.
Hayo ya wazazi yasiku-affect kabisa. walipoanza mapenzi yao we hukuwepo na sasa wakiamua kuachana waache wajiamulie wenyewe. Kuna mambo mengi yanaendelea kati yao we huwezi yaelewa.
Naona kuachana kwa wazazi wako kumekufanya u-panick na uone kama mapenzi ni kitu so complicated, hadi unajiuliza kama wewe utakuja olewa. usifananishe mfano wa mama yako na wa kwako. Kama Mungu alikuandikia utaolewa tu.
 

Naomba utusaidie kutueleza nini tatizo la ugomvi wao sometimes inaweza ikawa best solution ni Kutengana kutokana na aina ya tatizo.POLE SANA YATAPITA NDUGU YANGU.
 
Achana nao,hao ni wazazi wako,watarekebisha wenyewe.
 


mwambie ukweli bana,mianaume ndivyo tulivyo,wao watuvumiliage tu.
 
Mpe pole mhusika ila mwambie asijifungamanishe na upande wowote either baba au mama awe tu katikati kwani kiukweli hajui nani mkosaji na kwa kiasi gani. kama wao wazazi wanafikiri kuachana ndio kutawapa nafuu sawa, kwasababu wanachoangalia kwa sasa ni furaha zao personaly na sio watoto.

Ni kweli kwamba watoto hata kama ni wakubwa wataathirika kwa namna fulani sababau lets say kuna familu gathering ambazo zinawaleta pamoja alafu kila mtu anakuweo kwenye tukio kivyakevyake say misiba, harusi etc. ni ngumu sana. Sitaki hata kujiweka kwenye hiyo nafasi kwasababu sijui ningekuwa mimi ningefanyaje, but anyways it will come to pass na maisha yataendelea wao sio wa kwanza. Maombi na sala ndio vinahitajika zaidi.
 
Ni ngumu kuwashauri kuachana au kuendelea kuwa pamoja kwa sababu haujui reason inayopelekea mambo hayo, ukiijua utafanya uamuzi sahihi!
Pole sana we jipange na maisha yako yawe na furaha na amani..
 
We embu acha ugomvi wa wazazi waumalize wenyewe,kama hao ni wanandoa basi malalamiko yapelekwe kwa mshenga,matron au patron watotoa suluhu.Hivi unadhani wazazi wako wakitoa malalamiko yanayohusu undani wao utaweza jibia?

Kuhusu wewe,hakikisha unamshirikisha Mungu kwani mume na mke nzuri ni uweza wa Mungu pekee.
 

hapo mbili usifanye hvyo,zidi kuwasihi au waache ila endelea kuwaombea na jf members 2ko nyuma yako,btw waweza kunipm tukaongea
 
natafuta mke coz Ester sidhani kama ntampata tena nimeshatoa history yake hapo naomba nijue vitu vifuatavyo
Dini yako,kabila siaangalii coz tabia ya mtu siyo tabia ya kabila,
Elimu yako
Kimo chako sipendi kabsa wanawake wafupi(samahanini wahusika)
kama uko interesting na mm ntakupa namba yangu bt naogopa kuitoa hapa
sasa hivi sipo TZ npo masomon nje ya Africa,na nataka kuoa nyumbani(mtz) sitaki mzungu
 
nilipopitia hii story yako imenisikitisha pia imenikumbusha jambo flani. hata mimi mwaka huu wazazi wangu nusura waachane jambo ambalo lilinipa wakati mgumu sana si mimi peke yangu ila familia yote kwa ujumla kwani wazazi wangu wameishi pamoja kwa muda mrefu sana zaidi ya miaka 40 maana mimi baba yangu ana umri wa miaka 66 na mama 63 sasa lilikuwa ni jambo la ajabu na tena la aibu eti watengane uzeeni. nilitamani sana washauri lakini nilijua wasingeweza kunisikiliza na mbaya zaidi baba alitaka tuchague kati yake au mama. yani ukichagua upande wa mama baba usimjue na ukichagua upande wa baba mama usimjue jambo ambalo lilikuwa gumu sana. ilibidi sisi watoto kama familia tukae na kuamua kwakuwa sisi ni watu wazima maana wa mwisho kuzaliwa ana umri wa miaka 18 ndiye yuko form six sasa. tulifanya kikao sisi kama watoto na uamuzi wetu ukawa kwamba hatuto chagua baina ya baba au mama. kama ni ugomvi unawahusu wao wenyewe sisi wote wawili ni wazazi wetu na haiwezekani tuchague baina yao. basi tulimkalisha chini baba na mama na kumueleza uamuzi wetu japo baba alijifanya kutoelewa laknini baadaye alielewa na namshukuru Mungu walimaliza tofauti zao na sasa mambo yako shwari.
ndugu yangu wewe usikate tamaa uzidi kumwomba Mungu kwani yeye ndiye mweza wa yote.
 
pole sana ila wacha kabsa kuwaingilia kwa ushauri cha kufanya waombee kwa Mungu kwa mujibu wa imani yako ikiwezekana funga kabsa kwa sala na maombi
npe mawasiliano yako hata mm natafuta mchumba mwema coz mm mwenyewe najiamini ni mwema
ww ni dini gani?kabila ,elimu yako,kabila sichagui coz kila mtu na tabia yake,samahani kama ni mfupi coz naona huwa ni wabishi sna bila sababu za msingi,sitani kabsa kwa hili,
 

Nakutabiria utaoa mke mfupi na utampenda hakuna mfano.
 
Jitahidi uwe kiungo kipatanishi kati ya baba na mama. Piga magoti ukasali, ikiwezeka ufunge kwa ajili ya hilo.

Waweza kuwashirikisha wazee wenye busara kukusaidia pia,lakini lazima wawe ni wale ambao wanaheshimiwa na kukubaliwa na wazazi wote wawili,zaidi usiache kumuomba mola wako sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…