Wazee wa kiswahili

bichwa72

Member
Joined
May 28, 2012
Posts
11
Reaction score
0
Kuna ubaya gani wa lugha yetu tuliozaliwa nayo isiwe ya kutungiwa mitihani ya Taifa?
 
Kuna ubaya gani wa lugha yetu tuliozaliwa nayo isiwe ya kutungiwa mitihani ya Taifa?

Hakuna ubaya lakini kwanza mitaala na mafunzo lazima yafanyike katika Kiswahili. Hili ni jukumu kubwa sana. Tuanze nalo.

However, english must be taught aggressively in schools because currently it is the international language of business until Mandarin takes over.
 
Naomba mnijulishe neno ukiritimba ni kiswahili sahihi na kama ni kiswahili sahihi kwa lugha ya kigeni ya kiengereza linatamkwaje?
 
Naomba nifahamishwe kiswahili safi kabisa katika bara la Afrika kinazungumzwa nchi gani?
 
Naomba mnijulishe neno ukiritimba ni kiswahili sahihi na kama ni kiswahili sahihi kwa lugha ya kigeni ya kiengereza linatamkwaje?

Ukiritimba ni neno sahihi la kiswahili na neno jingine mbadala wake ni "Uhodhi"
Kwa lugha ya Umombo huijulikana kama "Monopoly"
 
Unguja mjini

(......katika nchi ya Zanzibar?)

:dizzy:
 
Sina hakika "usafi" wa lugha ni kitu gani. Nilipata kusoma makala moja juu ya Kiingereza cha Marekani. Mtafiti alikuwa na ramani ya Marekani, akazunguka Marekani nzima kuuliza: Kiingereza kibaya kinasemwa wapi na Kiingereza kizuri kinasemwa wapi Marekani. Wa New York na mashariki walisema watu wa kusini wa Kiingereza kibaya. Watu wa kusini walisema watu wa pwani ya mashariki na magharibi wana Kiingereza kibaya. Watu wa sehemu za nyanda za kati walisema watu wa kusini wanasema Kiingereza kibaya. Kila mmoja alikuwa na MAONI tofauti juu ya ubora wa lugha au lahaja mbalimbali.
Kwa hivyo basi, usafi wa lugha au ubora wa lahaji si sifa ya lugha yenyewe, bali ni maoni ya watu. Maoni hutofautiana kulingana na vigezo. Yumkini mtaalamu isimu atakwepa kutoa sifa ya "usafi" wa lugha kwa sababu kila lahaja inafuata kanuni fulani. Lahaja kama Kisanifu ni lahaja zilizoteuliwa tu, na jambo hili lisidhaniwe kuwa ni ubora wa lahaja.
 
hakuna lugha iliyo safi wala bora, lugha bora au ubora wa lugha hupimwa kulingana na mahitaji y awatumiaji wake.
 
Naomba nifahamishwe kiswahili safi kabisa katika bara la Afrika kinazungumzwa nchi gani?

Maeneo mengi ya Pwani ya Africa Mashariki wanangea Kiswahili fasaha. Mfano ni Unguja, Kilwa, Mombasa, Malidi, Makunduchi nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…