Wazee wa Yanga wagomea mchezo wa July 3, wasema walishacheza Mei 8

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Wazee wa Yanga Sc wamesema hawautambui mchezo wao na Simba Sc ulipangwa kufanyika Julai 3

Wamesema mchezo wao ulishachezwa Mei 8, kama TFF wanafuata kanuni Simba Sc waporwe alama ili wapewe

Wameyasema hayo leo walipokuwa na mkutano na waandishi wa habari
 
Mzee wa yanga tunayemtambua ni mzee MPILI hao hapo ni viongozi wa dini
 

Hahaaa,wameshanusa Wekundu wa Msimbazi wanachukua ubingwa kabla ya kufika hata hiyo tarehe! Ila huku kwetu tunatia aibu sana! Ulishaona huko Ulaya na kwingineko kuna wazee wanapeleka au kuzuia timu isiende uwanjani!
 
Hawa Yanga wenzangu wanaanza kunishangaza.
Ati Simba wapokwe pointi 3. Kwani Simba walipews lini hizo pointi 3!?

Mchezo kupangiwa tarehe nyingine maana yake ni kuwa hakuna aliyepewa pointi.

Serikali iliweka maslahi ya waliolipa kiingilio ili wapate haki ya kuangalia mchezo walioulipia.

Waache mashabiki tupate burudani. Binafsi sina wasiwasi Simba tunawapiga mapema tu
 
Yanga waoga sana, huo mchezo ulichezwa wapi hao wazee watuambie tujue, na wasipoleta timu uwanjani TFF wasipowashusha Yanga daraja sitawaelewa.
 
Watakuwa wametumwa na wagombea wa TFF wenye mlengo wa utopolo.
 
Kiukweli namshukuru mungu hakunifanya niwe shabiki wa yanga ,yaan hili timu lina watu majuha sana ,hiyo tar8 mechi ilichezwa wapi ,serikali ndio ilisogeza muda mbele kwa sabab zake inazozijua Sasa kwa lugha nyepesi yanga wanatunishiana msuli na serikali ?

Serikali ifanye jambo moja tu nao wakatae uwanja wao wa mkapa na uhuru kutumiwa na yanga ,yanga watafute uwanja wao ,.

Wasipewe ulinzi wowote ule kwenye mechi zao .

Ifike wakat yanga wasijione wapo juu ya serikali ,maana serikali ikiamua kuwakazia wao ndio wataumia ,haiwezekan jambo lilipita lakin wao wamekomalia tu ,tukisema mnaogopa kuingiza timu uwanjan kwa kuhofia kipigo kikubwa tutakuwa tunakosea?

Yanga mnajifanya wajeuri Sasa kwa hili swala nataka nione ujeuri wenu utaishia wap ,hiyo tar3 msilete timu uwanjan ,na hiki ndio kipimo cha tff kutoa maamuz magumu ambayo hayajawah kutokea .tunawasubil hiyo siku msilete timu uwanjan
 
Eti Simba waporwe points 3 wapewe Yanga! Kwani kuna points alizopewa Simba? Yaani Mizee iliyopitwa na Wakati inajitutumua yaonekane nayo yako Active wakati hayana lolote zaidi ya kuamini Uchawi.
 
Hivi kuna aliyewahi kusikia " wazee wa Liverpool,wazee wa Barcelona,wazee wa Real Madrid,wazee wa Jeventus au wazee wa PSG ?! "

Kuna mambo yanapaswa kuachwa kwani yamepitwa na wakati.Hao wazee hawajawahi kuwa msaada kwa club zaidi ya kuleta migogoro.
 
Mimi nilihitimisha hii timu haina watu wenye akili, siku walipogomea logo ya mdhamini.

Asante Mungu kunifanya nisiwe yanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…