Waziri Aweso ajitosa sakata wanawake Kijiji cha Oltepes kutumia mkojo wa ngombe kujisafisha wakiwa hedhini kutokana na ukosefu wa maji

Waziri Aweso ajitosa sakata wanawake Kijiji cha Oltepes kutumia mkojo wa ngombe kujisafisha wakiwa hedhini kutokana na ukosefu wa maji

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Zikiwa zimepita saa chache tangu Mwananchi iripoti wanawake katika Kijiji cha Oltepes kilichopo Kata ya Orbomba, wilayani Longido kutumia mkojo wa ng’ombe kujisafisha wakiwa hedhini kutokana na ukosefu wa maji, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema analifanyia kazi.

Akijibu changamoto hiyo katika ukurasa wa Instagram wa Mwananchi (@mwananchi_official) leo Jumanne Novemba 12, 2024, Aweso ameandika: “Nakiri kulipokea jambo hili na niahidi baada ya kulifuatilia kwa undani wake Wizara ya Maji utalitolea ufafanuzi yakinifu.”

Soma Pia: Ukosefu wa maji: Watumia mkojo wa ng'ombe kujisafisha wakiwa hedhini

Eneo hilo lenye wakazi wapatao 4,000, hutembea umbali wa kilomita tano kutafuta maji, lakini nyakati za kiangazi wanapolazimika kutumia mkojo wa ng’ombe, hutembea mpaka kilomita 10 kutafuta maji ya kunywa na kupikia kwenye mabwawa.
 
Zikiwa zimepita saa chache tangu Mwananchi iripoti wanawake katika Kijiji cha Oltepes kilichopo Kata ya Orbomba, wilayani Longido kutumia mkojo wa ng’ombe kujisafisha wakiwa hedhini kutokana na ukosefu wa maji, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema analifanyia kazi.

Akijibu changamoto hiyo katika ukurasa wa Instagram wa Mwananchi (@mwananchi_official) leo Jumanne Novemba 12, 2024, Aweso ameandika: “Nakiri kulipokea jambo hili na niahidi baada ya kulifuatilia kwa undani wake Wizara ya Maji utalitolea ufafanuzi yakinifu.”

Soma Pia: Ukosefu wa maji: Watumia mkojo wa ng'ombe kujisafisha wakiwa hedhini

Eneo hilo lenye wakazi wapatao 4,000, hutembea umbali wa kilomita tano kutafuta maji, lakini nyakati za kiangazi wanapolazimika kutumia mkojo wa ng’ombe, hutembea mpaka kilomita 10 kutafuta maji ya kunywa na kupikia kwenye mabwawa.
Ndio inavyotakiwa,hizi sio zama za watu kutaabika hivyo wakati Serikali Ina pesa
 
Utashangaa hao wamasai wana mbunge bungeni, wana mkuu wa wilaya, wana mkurugenzi, wana diwani, wana mwenyekiti wa mtaa, wana uongozi wa CCM, na viongozi wote hao wanaimba Mama Samia anaupiga mwingi.

Hii nchi imelaaniwa kabisa.
 
Back
Top Bottom