KERO Waziri Aweso unasema DAWASA kuna hujuma? Njoo Morogoro, huduma ya Maji ni kero kubwa

KERO Waziri Aweso unasema DAWASA kuna hujuma? Njoo Morogoro, huduma ya Maji ni kero kubwa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Naomba Serikali kupitia Waziri wa Maji, Juma Aweso afuatilia chanzo cha Wakazi wengi wa Mkoani Morogoro kukosa huduma ya maji.

Hii hali inatutesa sisi wakazi wa Morogoro kwa muda mrefu sasa, tumekuwa tukipiga kelele kwa mamlaka lakini ni kama hatusikilizwi.

Baadhi ya Watendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA) hawatimizi majukumu yao na hawatoi taarifa stahiki, kwa ufupi ni kuwa kuna mgao wa maji ambao ni mkali na hatuambiwi nini kilichotokea au kinachoendelea kutokea.

Taarifa zilizopo mitaani ambazo sio rasmi japo unaweza kuzifikiria kwa jicho la tatu kuwa zina ukweli ni kuwa inadaiwa Waziri Aweso ana ukaribu na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji ya Moro kiasi kwamba anakuwa mzito pia katika kumuwajibisha au pengine Aweso hapewi taarifa sahihi.

Namuomba Aweso hicho anachokifanya kuzunguka kwenye mamlaka mbalimbali wa DAWASA ambapo amenukuliwa akisema kuwa kuna hujuma na uzembe kwenye uwajibikaji, basi aje huku Morogoro ndio atajua hajui.

Baadhi ya maeneo ambayo huduma ya maji ni kero ni; Kata za Kihonda, Kichangani, Tungi, Mkundi, Mindu na Kilakala.

Pia soma ~ Waziri Aweso ateua Mkurugenzi Mpya wa Maji Morogoro, aelekeza iundwe timu maalum ya Wataalam

===============================​

TBC1 nao wameripoti juu ya changamoto ya maji iliyopo Morogoro


Ufafanuzi wa MORUWASA ~

MORUWASA: Tuna upungufu wa uzalishaji maji kwa 49% ndio maana Morogoro kuna mgao

MREJESHO:

Waziri Aweso: Bwawa la Mindu ni roho ya Wananchi wa Morogoro. Watu kukosa maji wiki 3 Morogoro ni uzembe. MORUWASA Msikae Ofisini
NA
- Meneja wa usambazaji maji MORUWASA asimamishwa kazi
 
Nimeishi Morogoro miaka ya 2011 hadi 2013 nikiwa na soma chuo, nlikaa mitaa ya kigurunyembe baadae kuhamia maeneo ya Makapchini, nane nane na Kihonda nilipomaliza chuo nilikaa maeneo ya Mwembesongo kumbe matatizo ya Morogoro kuhusiana na maji bado niyale yale na yako vilevile tena palepale zaidi ya miaka 10 nimetoka mji huo.

Natumaini ni wakati wa Serikali kuchukua hatua stahiki tena kutafuta Ufumbuzi wa kudumu kwa mahitaji ya maji kwa wakazi wa Morogoro wanapata changamoto sana.

Morogoro ni mji mzuri kuishi ikichangiwa na gharama nafuu za maisha, njia zilizofunguka kufika maeneo ya nchi yetu, uwekezaji katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo na mifugo, biashara, Utalii, Elimu nk
 
Huduma ya maji Morogoro ni ya hovyo kuliko mkoa wowote ule.

Walikuwa na mradi wa bwawa la mindu litanuliwe, mpaka sasa hakuna kilichofanyika.

Pia maji yao hayawi treated kwa kuwekewa dawa. Ndio maana mkoa huo unaongoza kwa magonjwa ya matumbo, hasa typhoid. Nadhani Waziri aanze kuwa anatembea na kifaa cha kupimia maji kama yako treated. Asiishie kukagua tu mashine na mitambo.

Ewura pia wawe na utaratibu wa kutoa taarifa kwa umma lini wanafanya ukaguzi wa treatment ya maji, na matokeo yalikuwa nini, ili mteja apate value for money.

Mamlaka ya Maji Morogoro ni ya hovyo kabisa na inastahili kuvunjwa
 
Hili tatizo limevuka mpaka sasa ni udhalilishaji. Yaan mvua ikikata wiki 2 tu basi maji yanakatwa milele.
Ni mwendo wa kununia maji kwa bowser.
Lini wananchi wa Morogoro tutajivunia uhuru wa nchi yetu. CCM mmepoteza kura nyingi sana.
 
Usihangaike na Waziri. Waziri msanii na watendaji wake wote wasanii! Tangu lini Wizara inayohitaji mwansayansi anaweka mtu wa historia? Hapo wamewekwa ili kupiga pesa za miradi, basi!

Sasa hivi MORIWASA wako tayari kusukuma maji kwenda viwanja vya maonesho nane-nane- ili kulima mahindi, bila kujali wananchi wanakunywa nini! RUBBISH!
 
Njoo malamba pia maji ni shida wakati 2015-2021 maji yalikuwa yanatoka lakin Saiz mnaweza kuachwa hata wiki moja ya pili ndio yatoke kama hawawezi kazi toa wote weka wanaoweza kazi wanatutesa wananchi,Mbona watu wapo wengi tu Tanzania mnawabembeleza nini hata mvua zikinyesha bado tu maji hayatoki kama vile hayo maji wanayazalisha wenyewe wakati ni ya Mungu sio yao
 
Hili tatizo limevuka mpaka sasa ni udhalilishaji. Yaan mvua ikikata wiki 2 tu basi maji yanakatwa milele.
Ni mwendo wa kununia maji kwa bowser.
Lini wananchi wa Morogoro tutajivunia uhuru wa nchi yetu. CCM mmepoteza kura nyingi sana.
Kwa mafuriko yaliyotokea Morogoro ni aibu kukosa maji
 
Usihangaike na Waziri. Waziri msanii na watendaji wake wote wasanii! Tangu lini Wizara inayohitaji mwansayansi anaweka mtu wa historia? Hapo wamewekwa ili kupiga pesa za miradi, basi!

Sasa hivi MORIWASA wako tayari kusukuma maji kwenda viwanja vya maonesho nane-nane- ili kulima mahindi, bila kujali wananchi wanakunywa nini! RUBBISH!
 
Back
Top Bottom