Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 1,278
- 797
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amekabidhi Bendera ya Taifa kwa Timu ya Fountain Gate inayokwenda nchini Afrika Kusini kwenye Mashindano ya Soka la Wanawake Afrika kwa Shule za Sekondari yanayotarajiwa kufanyika Mwezi Aprili, 2023.
Tukio hilo limefanyika leo Machi 31, 2023 jijini Dar es Salaam, ambapo amewasihi wachezaji hao watambue ukubwa wa mashindano hayo kwa kuwa hawaiwakilishi Tanzania pekee bali Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
"Mtakapokuwa nchini Afrika Kusini, hakikisheni mnapeperusha vyema Bendera yetu, mkafanye vizuri lakini pia mzingatie maadili, Mila na Desturi za Nchi yetu pamoja na kutangaza lugha ya Kiswahili.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fountain Gate Bw. Japhet Makau amesema Shule hiyo imeendelea kufanya vizuri katika michezo ambapo Ina wachezaji katika Timu ya Taifa ya Wanawake, pamoja na Timu inayoshiriki na kufanya vizuri katika Ligi kuu ya Wanawake nchini.
Timu hiyo ya Fountain Gate ndiyo wawakilishi wa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati CECAFA huku ukanda mwingine ni UNAF ambao ni Afrika Kaskazini, WAFU wa Afrika Magharibi na UNIFFAC wa Afrika ya Kati.View attachment 2572318View attachment 2572319 View attachment 2572320
Tukio hilo limefanyika leo Machi 31, 2023 jijini Dar es Salaam, ambapo amewasihi wachezaji hao watambue ukubwa wa mashindano hayo kwa kuwa hawaiwakilishi Tanzania pekee bali Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
"Mtakapokuwa nchini Afrika Kusini, hakikisheni mnapeperusha vyema Bendera yetu, mkafanye vizuri lakini pia mzingatie maadili, Mila na Desturi za Nchi yetu pamoja na kutangaza lugha ya Kiswahili.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fountain Gate Bw. Japhet Makau amesema Shule hiyo imeendelea kufanya vizuri katika michezo ambapo Ina wachezaji katika Timu ya Taifa ya Wanawake, pamoja na Timu inayoshiriki na kufanya vizuri katika Ligi kuu ya Wanawake nchini.
Timu hiyo ya Fountain Gate ndiyo wawakilishi wa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati CECAFA huku ukanda mwingine ni UNAF ambao ni Afrika Kaskazini, WAFU wa Afrika Magharibi na UNIFFAC wa Afrika ya Kati.View attachment 2572318View attachment 2572319