Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Bashungwa ameeleza hayo Wilayani Muleba Mkoani Kagera katika Ibada ya Shukrani ya Miaka 12 ya Uchungaji wa Askofu Grayson Mutegeki Katunzi pamoja na Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Anglikana Mt. Yohana Kimbugu, iliyoambatana na Ibada maalum ya kuwaombea Viongozi wa Kitaifa na Serikali.
“Katika utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuwezesha fedha tunaendelea na ujenzi wa njia nne kuanzia Rwamishenye Round about kupitia Kwenye daraja la Kanoni hadi Stendi ya Bukoba Mjini na wakati tunakamilisha, tumepanga kujenga njia nne kuanzia Rwamishenye hadi stendi mpya ya Kyakailabwa” amesema Bashungwa.
Bashungwa amesema Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara ya Karagwe – Benako kwa kiwango cha lami, sehemu ya Bugene-Burigi Chato (km 60), Mkandarasi anaendelea na kazi ambayo imefikia asilimia 41 ya utekelezaji.
Aidha, Waziri Bashungwa amesema Makandarasi wanaendelea na ukarabati wa barabara ya Lusahunga- Rusumo (km 92) kwa kiwango cha lami kwa gharama ya Shilingi Bilioni 153.6.
Vile vile, Amesema Serikali inakamilisha taratibu za kuanza ujenzi wa madaraja matano ya Kemishango, Kanoni, Kalebe, Kyanyabasa na Kyetema katika Mkoa wa Kagera.