Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 590
- 1,648
Taarifa ya wizara hiyo iliyotolewa na Waziri Dk Dorothy Gwajima, imeleza kuwa baada ya kesi hiyo kufika mahakamani, Wizara ilifuatilia na kugundua kesi hiyo iliondolewa baada ya walalamikaji na watuhumiwa kutoitikia wito wa mahakama.
Alisema video fupi inayosambazwa ikionesha malalamiko ya wazee hao kuchapwa viboko kwa tuhuma za uchawi, liliripotiwa Juni, 2022 na lilifikishwa mahakamani, lakini liliondolewa baada ya mahakama kutopewa ushirikiano na walalamikaji.
Kutokana na hali hiyo, Waziri Gwajima ameeleza kulaani vitendo vya watu kuchukua sheria mkononi kwa kuhukumu wananchi kwa vipigo na kwamba atalifuatilia ili sharia ichukue nafasi kwa yeyote aliyehusika na jambo hilo.
Habari Leo