Waziri Dkt. Gwajima aagiza kesi ya Diwani aliyewachapa viboko wazee ifufuliwe

Waziri Dkt. Gwajima aagiza kesi ya Diwani aliyewachapa viboko wazee ifufuliwe

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648

22f8d97d-b5ef-4aaf-9bf2-68027f5520ae-780x470.jpg

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, imeielekeza ofisi ya Ustawi wa Jamii Mkoa wa Tabora kwa niaba ya Kamishna wa Ustawii wa Jamii, kushirikiana na vyombo vya haki mkoani humo kuhakikisha wanafufua shauri la wazee waliochapwa viboko kwa tuhuma za kishirikina, ili mashahidi watoe ushahidi wao kuhusu kesi hiyo..

Taarifa ya wizara hiyo iliyotolewa na Waziri Dk Dorothy Gwajima, imeleza kuwa baada ya kesi hiyo kufika mahakamani, Wizara ilifuatilia na kugundua kesi hiyo iliondolewa baada ya walalamikaji na watuhumiwa kutoitikia wito wa mahakama.

Alisema video fupi inayosambazwa ikionesha malalamiko ya wazee hao kuchapwa viboko kwa tuhuma za uchawi, liliripotiwa Juni, 2022 na lilifikishwa mahakamani, lakini liliondolewa baada ya mahakama kutopewa ushirikiano na walalamikaji.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Gwajima ameeleza kulaani vitendo vya watu kuchukua sheria mkononi kwa kuhukumu wananchi kwa vipigo na kwamba atalifuatilia ili sharia ichukue nafasi kwa yeyote aliyehusika na jambo hilo.

Habari Leo

 
Serikali haiutambui uchawi, hao waliohusika kuchapa bakora lazma wapumulie mashine.
 
Taarifa ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imesema ilifuatilia na kubaini kesi hiyo iliondolewa baada ya kilichodaiwa Walalamikaji na Watuhumiwa hawakutoa ushirikiano kwa Mahakama.

Tukio la kesi hiyo liliibua mjadala baada ya kusambazwa video ikionesha malalamiko ya Wazee waliochapwa viboko kwa tuhuma za Uchawi ambapo Juni 2022 liliripotiwa na kufikishwa Mahakamani.

Waziri Gwajima amekemea utaratibu wa kuchukua Sheria mkononi na kuhukumu wananchi kwa vipigo na kuahidi kuwa atalifuatilia suala hilo hadi wahusika wawajibishwe.

Tazama Video hapa chini kuhusu mkasa huu

 
Dr. hapa niko na wewe, baraka za mweyezi mungu zitakuwa nawe daime haki ikitendeka. huyu diwani bado yuko mtaani kwa kuvunja sheria wazi wazi na ukatili wa kijinsia!
 
Dr. hapa niko na wewe, baraka za mweyezi mungu zitakuwa nawe daime haki ikitendeka. huyu diwani bado yuko mtaani kwa kuvunja sheria wazi wazi na ukatili wa kijinsia!
Vp huyu Diwani ni kweli alikamatwa!? Je na wazee walipata haki zao!? Muendelezo pls!!
 
Kesi iliishia wapi hii
Muheshimiwa Gwajima yumo humu, naamini akipata wasaa mzuri atatupa mrejesho wa maagizo yake kwa vyombo vyetu vya kisheria kwenye swala hili!!
 

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, imeielekeza ofisi ya Ustawi wa Jamii Mkoa wa Tabora kwa niaba ya Kamishna wa Ustawii wa Jamii, kushirikiana na vyombo vya haki mkoani humo kuhakikisha wanafufua shauri la wazee waliochapwa viboko kwa tuhuma za kishirikina, ili mashahidi watoe ushahidi wao kuhusu kesi hiyo..

Taarifa ya wizara hiyo iliyotolewa na Waziri Dk Dorothy Gwajima, imeleza kuwa baada ya kesi hiyo kufika mahakamani, Wizara ilifuatilia na kugundua kesi hiyo iliondolewa baada ya walalamikaji na watuhumiwa kutoitikia wito wa mahakama.

Alisema video fupi inayosambazwa ikionesha malalamiko ya wazee hao kuchapwa viboko kwa tuhuma za uchawi, liliripotiwa Juni, 2022 na lilifikishwa mahakamani, lakini liliondolewa baada ya mahakama kutopewa ushirikiano na walalamikaji.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Gwajima ameeleza kulaani vitendo vya watu kuchukua sheria mkononi kwa kuhukumu wananchi kwa vipigo na kwamba atalifuatilia ili sharia ichukue nafasi kwa yeyote aliyehusika na jambo hilo.

Habari Leo

View attachment 2447734
Dah! Kwa kweli hii kesi inafaa ianze upya ili huyo diwani na hao sungusungu 1) wathibitishe huo uchawi na 2) waonyeshe walifanya hivyo kwa mamlaka ya sheria gani.
 
Back
Top Bottom