#COVID19 Waziri Gwajima aagiza Askofu Gwajima kukamatwa ili athibitishe kauli anazozitoa dhidi ya Serikali na viongozi kuhusu chanjo ya UVIKO-19

Baada ya askofu Gwajima kukamatwa na Takukuru ni vema akahojiwa na jopo la wanasayansi ili baada ya hapo mjadala ufungwe rasmi tuendelee na majukumu mengine

Mungu ni mwema wakati wote!
Hahitaji hata jopo

vijana wawili watatu tu wa Muhas wanatosha

Tatizo Yule shabiki mandazi wa uongo
 
Misimamo inaweza kukuweka sehemu pabaya.
Misimamo ya Daniel ilimfanya atupwe ndani ya shimo la Simba wenye njaa kali lakini kwa uwezo usiofikirika kwa akili za kibinadamu alitoka salama.
 
Tuanze hapa

Ukipata chanjo unaweza kuugua/kuambukizwa uviko au huwezi?

Kama UNAWEZA kwanini unachanja; Kama HUWEZI naomba twende swali la pili
Unaweza kupata na chanjo sio kigezo cha kutopata isipokuwa madhara yake hata ukipata si makubwa kama ukiwa huna chanjo!
 
Hata Mbowe anaungwa mkono na wananchi wengi lakini amekamatwa!

Acha wakamatwe kamatwe hovyo ili mwisho wananchi wakikosa wa kuwasemea mambo yao watasema wenyewe kwa vitendo...

Tuendelee kula mtori nyama tutazikuta chini
Narudia, WAKAMATWE WOTE
 
nahisi hawajakuelewa..🙂
 
Chanjo zilizoletwa awamu ya kwanza ni 1m ambazo bado hazijaisha. Idadi ya madaktari na watumishi wa idara ya afya ni zaidi ya 1m nchini. Kwa kuwa hawa ndio wanapaswa kutoa chanjo na wamesita wenyewe kuchanjwa, iweje Dr Gwajima amkomalie Askofu Gwajima?

Dr Gwajima anajivuruga mwenyewe. Anapaswa kuhakikisha kwanza watu wa Wizara yake wanapata chanjo kama wanaamini ni bora na salama
 
Jimbo liwe wazi asap
Tumsamehe Halima
Tumrudishe kundini kwani hakuna binadamu aliyekamilika.
Mwenyezimungu Mkubwa tuendelee kuamini kwamba DHULMA HAIDUMU NA ENDAPO ITADUMU BASI ITA ANGAMIZA
 
Wao ndiyo wathibitishe na watoe scientific proof ya kuwa chanjo ni salama, inazuia ugonjwa na ina life span ipi.
ACHA KUJIDHALILISHA. CHANJO IMETENGENEZWA KUFUATA MTIRIRIKO WOTE WA KISAYANSI NA IMETHIBITIKA HAINA MADHARA NDIO MAANA IKARUHUSIWA NA TAASISI HUSIKA KAMA WHO. DAI NA SCIENTIFIC PROOF YA CHANJO NYINGINE ZOTE BASI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…