Waziri Gwajima ajitosa suala la DC kumpiga binti kibao

Waziri Gwajima ajitosa suala la DC kumpiga binti kibao

FbUser

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2014
Posts
439
Reaction score
644
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt . Dorothy Gwajima ameeleza kusikitishwa na tukio linalodaiwa kufanywa na mkuu wa wilaya ya Songwe, Simon Simalenga la kumpiga na kumjeruhi binti mwenye umri wa miaka 20 Florenencia Mjenda, mkazi wa kata ya Mbangalo wilayani humo.

Dkt. Gwajima amesema tukio hilo ni la kweli kama lilivyoripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na tayari binti huyo amefungua kesi polisi ya shambulio la aibu katika kituo cha Mkwajuni.

Waziri Gwajima amesema ametuma kikosi cha maafisa ustawi wa jamii kwenda nyumbani kwa binti huyo, ili wampe ushauri nasihi wakati shauri hilo likiendelea na amewataka wasaidizi wa kisheria wafuatilie kwa karibu hatua zote.

Ametoa wito kwa viongozi kuacha kwenda nje ya taratibu na kuanza ugomvi binafsi na wananchi ambapo wanawake, wasichana na watoto wanakuwa waathirika.
 
Vema kama Kuna docket police, hope's hata hizi NGOs zetu zitamsaidia huyu binti kupata haki yake mahakamani, na ninategemea police wamechukua statement iliyoambatanishwa na evidence kama Doctor reports, mtaalamu kutoka ustawi wa jamii, crime scene na ofcoures key eye witness, maana hii inasaidia kutengeneza water tight case dhidi ya suspect.
 
Nimemsikiliza huyo binti anayesemekana kapigwa na amesema ana umri wa miaka 16 na wewe unasema ana miaka 20. Nani mkweli?

Kwa maoni yangu, naona kama binti kapangwa fulani.
 
Nimemsikiliza huyo binti anayesemekana kapigwa na amesema ana umri wa miaka 16 na wewe unasema ana miaka 20. Nani mkweli?

Kwa maoni yangu, naona kama binti kapangwa fulani.

Huyo mbali ya kutimuliwa kazi anatakiwa kuswekwa ndani haraka sana! DC uchwara huyo, arudi huku Njombe kulima viazi mvua zimeshaanza kunyesha!
 
Hyo DC ukimuangaliaga ni km Mtu wa hasira hasira au mbabe fulani hv....by the way kipindi cha mwendazake kuna waziri aliunda kamat kuchunguza tukio la mteule wa rais baada ya majibu kutoka ikawa historia kwa wazir ... ss sijui Mama Gwajima ana kumbukumbu na hilo....maana sidhan km aliyemteua hana information zaid au ndio tunasafishana ....ngoja tuendelee kunywa mtori
 
Back
Top Bottom