Pre GE2025 Waziri Gwajima: Jamii iwape wanawake nafasi na sauti katika uongozi

Pre GE2025 Waziri Gwajima: Jamii iwape wanawake nafasi na sauti katika uongozi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, ametoa wito kwa jamii kuwapa wanawake nafasi na sauti katika uongozi, akisema kuwa bila juhudi za makusudi za kuwaunga mkono, usawa wa kijinsia hautafikiwa.

Waziri Gwajima ameyasema hayo mkoani Dar es Salaam, Februari 11, 2025 alipohutubia kama mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa Programu ya Uongozi wa Wanawake Vijana (Young Women Leadership Program - WYLP) inayoratibiwa na Care International Tanzania kwa kushirikiana na Mwanamke Initiatives Foundation.

Soma Pia: Kipindi hiki cha Uchaguzi wanawake wanapata nafasi ya kutosha kushiriki kwenye masuala ya uchaguzi?

Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Mwanamke Initiatives Foundation, Wanu Hafidh, ameeleza kuwa yeye mwenyewe ni mnufaika wa programu za uongozi na anafahamu umuhimu wake kwa wanawake vijana, hivyo anaamini kuwa programu hiyo itatoa mafunzo ya uongozi, ushawishi na utetezi wa haki za wanawake, hivyo kuwawezesha wanawake vijana kushika nafasi mbalimbali za maamuzi.

Naye Mkufunzi wa programu hiyo Imani Kajula amesema kuwa ana imani wanawake hao watajifunza masuala mengi yanayohusu uongozi na kuongeza idadi kubwa ya viongozi wanawake katika jamii lengo likiwa ni kupunguza pengo lililopo kati ya wanaume na wanawake katika uongozi.

"Baada ya kuhitimu mafunzo kama haya, hatua inayofuata ni utekelezaji wa yale tuliyojifunza ili kuleta mabadiliko. Uzinduzi wa WYLP ni sehemu ya kuandaa viongozi wa baadaye ambao watakuwa na mchango mkubwa katika jamii na taifa kwa ujumla," amesema.
 
Wanawake wanajitahidi kuelimishana kila iitwapo leo,Sasa njoo upande wa pili,pangu pakavu tia mchuzi.
Mwalimu wa mwanaume ni maisha

Wanaume ni kupeana michongo na sio kufundishana sababu wote tunajua tayari
 
Wanawake wanajitahidi kuelimishana kila iitwapo leo,Sasa njoo upande wa pili,pangu pakavu tia mchuzi.
Upo sahihi kabisa.
Lakini hii ya kupewa uongozi kisa tu ni mwanamke binafsi napinga kwa nguvu zote. Mwanamke apewe uongozi pale ambapo anastahili na anazo sifa za kuwa kiongozi na si abebwe na jinsia yake.
 
Meritocracy must be observed..
We should not select leader just because he is a man or she is a woman
 
Kwa kumzingatia tu boss wake anayemlipa mshahara hii jinsia kama kuongoza inafaa iwaongoze watoto zao majumbani wanaume wakiwa kwenye majukumu mengine ya msingi.

Vyeo visigawiwe kwa jinsia ndiyo maana tunayumba vibaya.
 
Ninyi ndio chanzo hamko kama mama zetu waliotulea sisi,

Mmebadirika sanaaaa
Lini nyie mlifanana na baba zetu? Dunia inabadilika na nyie mnabadilika lakini nyie mnataka sisi tuwe na mentality ya mwaka 47 inawezekana vipi?
Kubadilika kwa mwanamke kuna sababu, unyanyasaji, kudidimizwa na ukatili alioupata.
Pambanieni vijana wenu wa kiume mkisubiri wanawake wafanye hivyo mtasubiri sana. Kijana wa kiume anahitaji father figure, mafunzo yatoke kwa mwanaume na si kwa mwanamke. Mwanamke atabaki kuwa mlezi tu.
 
Ili wapate nafasi wanalalwa kwanza hawana ubunifu wowote hao

Bila kutoa mwili hawajiamini kama wanaweza

Watumishi walio wengi katika serikali na taasisi binafsi ni malaya, walianza kuuza miili yao ili wapate kazi na kupandishwa vyeo
Umeshawanunua wangapi hadi sasa ili uwape nafasi?
 
Back
Top Bottom