Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo (Mb) amesema kuwa wananchi 595 waliofanyiwa uhakiki wa mali katika eneo la mradi wa Engaruka (Monduli) wanalipwa jumla ya shilingi bilioni 6.26
Amebainisha hayo Januari 09, 2025 jijini Arusha akihojiwa asubuhi na Azam Tv na kusema kuwa "Agosti 24, 2024 alifika katika eneo la Engaruka na kukutana na wananchi kwa niaba ya Serikali na kuahidi kuwa Serikali ni sikivu na itawalipa fidia hivi karibuni".
Aidha, Dkt. Jafo amesema mradi wa Engaruka utakuwa na faida kubwa kwa wananchi kwa kufungua fursa mbalimbali ikiwa ni pamoja na ajira na kukuza uchumi wa mtu mmojammoja na Serikali kwa ujumla.
Amebainisha hayo Januari 09, 2025 jijini Arusha akihojiwa asubuhi na Azam Tv na kusema kuwa "Agosti 24, 2024 alifika katika eneo la Engaruka na kukutana na wananchi kwa niaba ya Serikali na kuahidi kuwa Serikali ni sikivu na itawalipa fidia hivi karibuni".
Aidha, Dkt. Jafo amesema mradi wa Engaruka utakuwa na faida kubwa kwa wananchi kwa kufungua fursa mbalimbali ikiwa ni pamoja na ajira na kukuza uchumi wa mtu mmojammoja na Serikali kwa ujumla.