Waziri Jenista Mhagama akabidhi vifaa kuimarisha kitengo cha mawasiliano na elimu ya afya kwa Umma

Waziri Jenista Mhagama akabidhi vifaa kuimarisha kitengo cha mawasiliano na elimu ya afya kwa Umma

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

Jenista Mhagama akabidhi vifaa kuimarisha kitengo cha mawasiliano na elimu ya afya kwa umma
GWom5Y8XEAAH3lx.jpg
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama Septemba 3, 2024 amekabidhi vifaa vya studio vitakavyosaidia Kitengo cha Mawasiliano na Elimu ya Afya kwa Umma kufanya kazi kwa ufanisi zaidi katika kuhabarisha umma kuhusu taarifa mbalimbali za maendeleo ya Sekta ya Afya nchini pamoja na Elimu ya Afya.

Waziri Mhagama wakati akikabidhi vifaa hivyo amewataka watumiaji wa vifaa hivyo kuvitunza na kuvitumia vizuri ili kufikia lengo lililokusudiwa la kuihabarisha jamii katika masuala ya Sekta ya Afya.

"Twendeni tukavitunze vifaa hivi, kwa kuwa huu ni uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ambapo wananchi wanatakiwa kufaidika kwa kupata Habari mbalimbali za Afya pamoja na Elimu ya Afya." Amesema Waziri Mhagama.

Waziri Mhagama amewataka wataalam hao kufanya kazi zenye ubunifu na viwango vya juu huku maudhui yatakayozalishwa yawe yamezingatia maadili, mila na desturi za Kitanzania.

Vifaa hivyo ni pamoja na Camera, Boom Mike, Mixer, Laptop, Macbook, Drone's, Tripod Stand pamoja na vifaa vingine vya Studio ambavyo vyote vimenunuliwa na Wizara.

GWom5ZAWoAATHGW.jpg
GWom5Y2XUAE-77F.jpg

GWom6YBXAAEahPw.jpg
 
Back
Top Bottom