Kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Jerry William Silaa (Mb) chini ya Kifungu cha 9 (1) cha Sheria ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (USCAF) ya Mwaka 2009 amemteua Mhandisi Peter Phillip Mwasalyanda kuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (USCAF). Aidha, uteuzi huo ni wa muda wa kipindi cha miaka mitano (05) kuanzia tarehe 07 Oktoba, 2024 hadi tarehe 06 Oktoba, 2029.