Pre GE2025 Waziri Kassim Majaliwa: Polisi msizuie Wananchi wanaokuja na mabango kwenye mikutano yangu

Pre GE2025 Waziri Kassim Majaliwa: Polisi msizuie Wananchi wanaokuja na mabango kwenye mikutano yangu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amelitaka Jeshi la Polisi Temeke kutozuia wananchi watakaobeba mabango kuwasilisha kero zao, kwa kile alichosema ni utaratibu wa ziara zake kusikiliza na kutatua kero za wananchi, pia amesema hapangiwi ratiba.

Katika kufafanua hilo Majaliwa amesema:

Nitatembelea baadhi ya miradi ilizungumzwa hapa kwamba yamekuja mabilioni mabilioni, nitaenda kuona mabilioni hayo yalivyotumika kwenye miradi hiyo.
Lakini pia wakati wowote naweza kubadilisha ratiba nikaenda kwenye mradi wowote ule, muwe mmepanga nyie au nimepanga mimi, nitaambia madereva nataka kwenda huku nao watanyosha kwenda huko.
Tukiwa kwenye miradi hiyo tutakutana na Wananchi, moja kati ya jukumu letu kama Watumishi wa Umma ni kuwahudumia Wananchi na moja kati ya huduma ni kusikiliza matatizo yao ili tuyafanyie kazi tuondoe changamoto hizo waendelee na maisha yao. Kwahiyo nitapata nafasi ya kusikiliza wananchi wanasema nini.
Kwenye mikutano hii ya Wananchi Wakuu wa Idara wote mnatakiwa kuwa kwenye kituo hicho mimi ntakapokuwa. Wananchi wakija na Mabango mtalazimika kuyaacha, Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya usizuie bango lolote hiyo ndo forum yao ya kunieleza yaliyopo

Aidha, Majaliwa amewasisitiza Viongozi wakiona Mabango hayo ya Wananchi wayasome na kuyatafutia majibu badala ya kuyazuia.

PIA SOMA
- Waziri Mkuu Majaliwa - Tekelezeni kwa vitendo falsafa ya 4r za Rais Samia

- LIVE - Uzi Maalum wa Matukio ya Kiusalama kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amelitaka Jeshi la Polisi Temeke kutozuia wananchi watakaobeba mabango kuwasilisha kero zao, kwa kile alichosema ni utaratibu wa ziara zake kusikiliza na kutatua kero za wananchi, pia amesema hapangiwi ratiba.

Aidha, Majaliwa amewasisitiza Viongozi wakiona Mabango hayo ya Wananchi wayasome na kuyatafutia majibu badala ya kuyazuia.
Chawa wa mama wanakuja sasa hivi kupinga
 
Maandamano ya amani kuelezea kero na malalamiko ...No

Mabango ya amani kuelezea kero na malalamiko.....YES

2025
 
Back
Top Bottom