The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Dkt Saada Mkuya Salum amesema serikali itaendelea kuwachukulia hatua wafanyabiashara ambao sio waaminifu wanaoenda kinyume na sheria za kodi kwa kukwepa kodi stahiki ya serikali
Waziri Mkuya ameeleza hayo wakati alipoongoza operesheni maalum ya ukaguzi wa utoaji wa risiti za kielektroniki katika maeneo ya Mlandege akiwa ameambatana na uongozi wa mamlaka ya Mapato Zanzibar ZRA ukiongozwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Said Athumani
Dkt Mkuya amesema serikali haitokuwa tayari kuona kodi inakwepwa na baadhi ya wafanyabiashara wachache wasio waminifu
Kwa upande wake Kamishna Mkuu wa ZRA Said Athumani amesema operesheni hizo zitakua endelevu katika maeneo yote ya unguja na Pemba
Waziri Mkuya ameeleza hayo wakati alipoongoza operesheni maalum ya ukaguzi wa utoaji wa risiti za kielektroniki katika maeneo ya Mlandege akiwa ameambatana na uongozi wa mamlaka ya Mapato Zanzibar ZRA ukiongozwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Said Athumani
Dkt Mkuya amesema serikali haitokuwa tayari kuona kodi inakwepwa na baadhi ya wafanyabiashara wachache wasio waminifu
Kwa upande wake Kamishna Mkuu wa ZRA Said Athumani amesema operesheni hizo zitakua endelevu katika maeneo yote ya unguja na Pemba