Waziri Kigwangala alituambia huduma za afya huwa hazitangazwi, mbona hopitali hii inatangaza huduma zake kupitia Fiesta 2019?

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Wakati Dr. Kigwangala akiwa Naibu Waziri wa Afya alituambia ni mwiko kutangaza huduma za afya kupitia vyombo vya habari. Akamfungia Dr. Mwaka kwa sababu hizo hizo za kutangaza huduma za afya ambazo ni mwiko kutangaza sio Tanzania tu bali duniani kote huwa iko hivyo.

Cha kushangaza kuna hospitali inaitwa Uhuru hospital inajitangaza kupitia Clouds Fiesta 2019. Wizara ya afya haikuliona hili kuwa ni mwiko kama alivyosema Kigwangala?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…