Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Mhandisi Ndolezi Petro, Waziri Kivuli wa Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera, Vijana, Kazi na Ajira kutoka ACT Wazalendo, ametangaza nia ya kugombea ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini katika uchaguzi wa 2025.
Akizungumza Januari 16, 2025, kijijini Nguruka, alisisitiza dhamira yake ya kushughulikia changamoto za jimbo hilo, ikiwemo miundombinu mibovu, ukosefu wa pembejeo za kilimo, migogoro ya ardhi, na huduma duni za afya vijijini.
Pia ameahidi kuzingatia ajira kwa vijana, kuimarisha Baraza la Taifa la Vijana, na kuhakikisha sekta isiyo rasmi inajumuishwa katika mifuko ya hifadhi ya jamii.
ACT Wazalendo ilifungua rasmi mchakato wa watia nia kwa nafasi za uongozi Januari 15, 2025, ambapo Dorothy Semu na Othman Masoud wamejitokeza kugombea urais kwa Tanzania Bara na Zanzibar.
Source: Jambo TV
Akizungumza Januari 16, 2025, kijijini Nguruka, alisisitiza dhamira yake ya kushughulikia changamoto za jimbo hilo, ikiwemo miundombinu mibovu, ukosefu wa pembejeo za kilimo, migogoro ya ardhi, na huduma duni za afya vijijini.
Pia ameahidi kuzingatia ajira kwa vijana, kuimarisha Baraza la Taifa la Vijana, na kuhakikisha sekta isiyo rasmi inajumuishwa katika mifuko ya hifadhi ya jamii.
ACT Wazalendo ilifungua rasmi mchakato wa watia nia kwa nafasi za uongozi Januari 15, 2025, ambapo Dorothy Semu na Othman Masoud wamejitokeza kugombea urais kwa Tanzania Bara na Zanzibar.
Source: Jambo TV