Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 1,278
- 797
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb),ameshiriki maadhimisho ya miaka 50 ya uhusiano baina ya Tanzania na UAE yaliyoandaliwa na Chuo cha Diplomasia cha Anwar Gargash cha nchi hiyo.
Akizungumza mbele ya wanafunzi na wahadhiri wa Chuo hicho, Mhe. Waziri Kombo alitoa rai ya kuendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na UAE na kuweka misingi imara ya Kidiplomasia kwa vizazi vijavyo.
Kupitia mazungumzo yake chuoni hapo, Mhe. Waziri aliwasilisha salamu za pongezi kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu na Mtawala wa Abu Dhabi Mtukufu Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan na wananchi wa UAE kote duniani kwa kuadhimisha miaka 53 ya siku adhimu ya Taifa lao.
Mhe. Kombo amesema, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Umoja wa Falme za Kiarabu zina historia ndefu ya urafiki na uhusiano tangu enzi za biashara za Ghuba ya Uajemi kupitia Bahari ya Hindi hadi mwambao wa Tanzania, kuanzia Zanzibar, Dar es Salaam hadi Mtwara.
“Msingi imara uliowekwa na waasisi wa mataifa haya, marehemu Sheikh Zayed bin Sultan al Nahyan na hayati Mwalimu Julius Nyerere, Tanzania na UAE ziliimarisha uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1974 baada ya kuungana kwa UAE mwaka 1971, “ alisema Balozi Kombo.
Ameongeza kuwa uhusiano huo umeendelea kuwa wa kirafiki na wenye mshikamano tangu wakati huo na kwamba anaamini kuwa uhusiano huo utaimarika zaidi katika miaka mingi ijayo.
Mhe. Waziri Kombo ametumia mhadhara huo kunadi fursa za biashara, uwekezaji na Utalii zilizopo nchini na kuwaita wananchi wa UAE kuja nchini kuwekeza na hivyo kuzinufaisha pande mbili kupitia Diplomasia ya Uchumi .
Akiongea kuhusu Ushirikiano na Chuo cha Diplomasia cha Anwar Gargash amesema Chuo hicho kina uhusiano na Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim ambao mwezi huu umetimiza mwaka mmoja tangu kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano (MoU) iliyoanzisha uhusiano huo ambayo ilisainiwa mwezi Desemba 2023, wakati wa Mkutano wa COP28 uliofanyika Dubai.
Akizungumza mbele ya wanafunzi na wahadhiri wa Chuo hicho, Mhe. Waziri Kombo alitoa rai ya kuendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na UAE na kuweka misingi imara ya Kidiplomasia kwa vizazi vijavyo.
Kupitia mazungumzo yake chuoni hapo, Mhe. Waziri aliwasilisha salamu za pongezi kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu na Mtawala wa Abu Dhabi Mtukufu Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan na wananchi wa UAE kote duniani kwa kuadhimisha miaka 53 ya siku adhimu ya Taifa lao.
“Msingi imara uliowekwa na waasisi wa mataifa haya, marehemu Sheikh Zayed bin Sultan al Nahyan na hayati Mwalimu Julius Nyerere, Tanzania na UAE ziliimarisha uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1974 baada ya kuungana kwa UAE mwaka 1971, “ alisema Balozi Kombo.
Mhe. Waziri Kombo ametumia mhadhara huo kunadi fursa za biashara, uwekezaji na Utalii zilizopo nchini na kuwaita wananchi wa UAE kuja nchini kuwekeza na hivyo kuzinufaisha pande mbili kupitia Diplomasia ya Uchumi .