Bashir Yakub
Member
- May 27, 2013
- 96
- 1,745
NDG. LUKUVI, SIO LAZIMA KISHERIA JINA LA MKE NA MME KUWA KWENYE HATI YA KIWANJA.
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255 714 047 241.
Lazima tunapotoa kauli tuwe tunatofautisha matamanio yetu, na kile sheria inachosema. Tuangalie haya 6 kuhusu kauli ya ndg Lukuvi.
1. Mpaka sasa hakuna sheria inayolazimisha kuwa jina la mke na mme lazima yawe kwenye hati ya kiwanja. Tuna Sheria ya Ardhi Na. 4, Na.5, Sheria ya Usajili wa Ardhi Sura ya 334, Sheria Na. 17/2008 ya Rehani ya Mikopo nk nk.
Zote hizi hakuna jambo hilo, isipokuwa limefanywa kuwa la hiari.
2. Tafsiri ya neno Umiliki wa Ardhi, ni umiliki unaohusu mtu mmoja peke(exclusively), mtu zaidi ya mmoja(co-occupancy), ushirika(partnership), kampuni nk. Soma kifungu cha 19(1) cha Sheria ya ardhi Na.4.
Kwa mujib wa kifungu hiki umiliki wa mtu mmoja peke haujafa bado upo.
3. Kwà mujib wa Sheria ya Ndoa ili mwanandoa awe na share kwenye kiwanja/mali lazima awe amechangia(joint effort/contribution). Hata km alifanya kaz za ndan(domestic duties) ni mchango, la msingi lazima achangie.
4. Si lazima hati ya kiwanja iwe na majina yote ya mke na mme ndipo haki ya umiliki wa pamoja ipatikane. Hati inaweza kuwa na jina la mmoja mf. mme tu lakini mke bado akawa na haki/share.
Haki ya pamoja inatokana na nguvu/jitihada za pamoja(joint efforts) ktk upatikanaji wa mali husika, haitokani na nani kaandikwa kwenye hati.
5. Sheria ya Ardhi na ya ndoa zinahuruhusu kitu kinaitwa "ESTATE PLANNING" . Kupitia hiki kitu wanandoa wanaweza kuamua baadhi ya mali ziwe zao wote yaani za ndoa, na baadhi kila moja imilikiwe na mmoja bila kumhusisha mwingine.
Kitu hiki kinaweza fanyika kabla ya ndoa km maandalizi ya ki-mali ya kuingia kwenye ndoa ili kuepusha mgogoro baadae, au ndani ya ndoa tayar.
Kupitia kitu hiki ndipo wanandoa wanaweza amua kusajili ardhi kwa majina yao wote wawili ama hapana.
6. Lukuvi anaongelea ardhi zenye hati, vipi zile ambazo hazina hati anatwambiaje. Kuwa wakienda kuandikishana huko serikali za mitaa wanakoendaga(japo hairuhusiwi) wawabebe na wake zao au waume zao ndo mauziano ya ardhi yawe halali !!!.
Atangaze bas taifa zima lijue kuwa kuanzia sasa ni kosa kisheria kununua ardhi bila mke au mme wako.
Pia soma
www.jamiiforums.com
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255 714 047 241.
Lazima tunapotoa kauli tuwe tunatofautisha matamanio yetu, na kile sheria inachosema. Tuangalie haya 6 kuhusu kauli ya ndg Lukuvi.
1. Mpaka sasa hakuna sheria inayolazimisha kuwa jina la mke na mme lazima yawe kwenye hati ya kiwanja. Tuna Sheria ya Ardhi Na. 4, Na.5, Sheria ya Usajili wa Ardhi Sura ya 334, Sheria Na. 17/2008 ya Rehani ya Mikopo nk nk.
Zote hizi hakuna jambo hilo, isipokuwa limefanywa kuwa la hiari.
2. Tafsiri ya neno Umiliki wa Ardhi, ni umiliki unaohusu mtu mmoja peke(exclusively), mtu zaidi ya mmoja(co-occupancy), ushirika(partnership), kampuni nk. Soma kifungu cha 19(1) cha Sheria ya ardhi Na.4.
Kwa mujib wa kifungu hiki umiliki wa mtu mmoja peke haujafa bado upo.
3. Kwà mujib wa Sheria ya Ndoa ili mwanandoa awe na share kwenye kiwanja/mali lazima awe amechangia(joint effort/contribution). Hata km alifanya kaz za ndan(domestic duties) ni mchango, la msingi lazima achangie.
4. Si lazima hati ya kiwanja iwe na majina yote ya mke na mme ndipo haki ya umiliki wa pamoja ipatikane. Hati inaweza kuwa na jina la mmoja mf. mme tu lakini mke bado akawa na haki/share.
Haki ya pamoja inatokana na nguvu/jitihada za pamoja(joint efforts) ktk upatikanaji wa mali husika, haitokani na nani kaandikwa kwenye hati.
5. Sheria ya Ardhi na ya ndoa zinahuruhusu kitu kinaitwa "ESTATE PLANNING" . Kupitia hiki kitu wanandoa wanaweza kuamua baadhi ya mali ziwe zao wote yaani za ndoa, na baadhi kila moja imilikiwe na mmoja bila kumhusisha mwingine.
Kitu hiki kinaweza fanyika kabla ya ndoa km maandalizi ya ki-mali ya kuingia kwenye ndoa ili kuepusha mgogoro baadae, au ndani ya ndoa tayar.
Kupitia kitu hiki ndipo wanandoa wanaweza amua kusajili ardhi kwa majina yao wote wawili ama hapana.
6. Lukuvi anaongelea ardhi zenye hati, vipi zile ambazo hazina hati anatwambiaje. Kuwa wakienda kuandikishana huko serikali za mitaa wanakoendaga(japo hairuhusiwi) wawabebe na wake zao au waume zao ndo mauziano ya ardhi yawe halali !!!.
Atangaze bas taifa zima lijue kuwa kuanzia sasa ni kosa kisheria kununua ardhi bila mke au mme wako.
Pia soma
Waziri Lukuvi: Kuanzia sasa ukiwa na kiwanja kinatakiwa kiitwe kwa jina lako na la mke wako
Serikali imesema sheria inaruhusu hati ya kumiliki viwanja kuandikwa majina ya familia ikiwemo mume, mke pamoja na watoto hatua ambayo itasaidia kuondoa migogoro ya mirathi. Akizungumza leo Jumamosi Desemba 19, mkoani Kilimanjaro. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliamu Lukuvi...