Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
WAZIRI ''MAESTRO'' ALLY NA LITTLE STEVIE WONDER
Watafiti wote naamini haweshi kujuta wanapomaliza kumhoji mtu kisha mtu yule akawa hapatikani tena kwa sababu yoyote ile kwa kujilaumu kwa nini sikumuuliza hiki au kile.
Nimepata picha ya Waziri naamini ya miaka ya katikati 1960s akiwa na Lucky Star ya Shakila Tanga akipiga organ.
Najilaumu kwa nini muda wote katika miaka yote niliyokuwa na Maestro sikukaa na yeye kitako tukazungumza utoto wake Tanga alipoanza muziki na kumpigia Shakila wa Lucky Star.
Inaelekea Maestro alianza muziki kipindi kile kile ambacho Stevie Wonder alianza Marekani kwa kurekodi na Tamla Motown ya Berry Gordy.
Shakila halikadhalika alikuwa akirekodi muziki wake na kutoa santuri huku kwetu na bila shaka sauti yake ikisindikizwa na na kinanda cha Waziri Ally.
Lakini wapi tutapata ''discography,'' ya Shakila na Lucky Star na kusikiliza keyboard ya Maestro?
Labda Masoud Masoud Manju la Muziki anaweza kutusaidia.
Leo nimezungumza na jamaa zangu Tanga kutafuta habari za Waziri akiwa na Shakila na Lucky Star.
Naambiwa Lucky Star takriban wote wametangulia mbele ya haki hawa ndiyo wangeliweza kunipa historia ya enzi zile.
Lakini sijakata tamaa.
Afrika tuna shida zetu nyingi tu.
Nimemtafuta Stevie Wonder.
Taarifa zake zote zipo kiasi inaweza kukuzamisha ukapotea baharini kwa uzito wake.
Huyo kulia ni Stevie Wonder ambae kama nilivyosema hapo juu alianza muziki wakati mmoja na Maestro na wote wakiwa wapiga kinanda wa sifa.
Watafiti wote naamini haweshi kujuta wanapomaliza kumhoji mtu kisha mtu yule akawa hapatikani tena kwa sababu yoyote ile kwa kujilaumu kwa nini sikumuuliza hiki au kile.
Nimepata picha ya Waziri naamini ya miaka ya katikati 1960s akiwa na Lucky Star ya Shakila Tanga akipiga organ.
Najilaumu kwa nini muda wote katika miaka yote niliyokuwa na Maestro sikukaa na yeye kitako tukazungumza utoto wake Tanga alipoanza muziki na kumpigia Shakila wa Lucky Star.
Inaelekea Maestro alianza muziki kipindi kile kile ambacho Stevie Wonder alianza Marekani kwa kurekodi na Tamla Motown ya Berry Gordy.
Shakila halikadhalika alikuwa akirekodi muziki wake na kutoa santuri huku kwetu na bila shaka sauti yake ikisindikizwa na na kinanda cha Waziri Ally.
Lakini wapi tutapata ''discography,'' ya Shakila na Lucky Star na kusikiliza keyboard ya Maestro?
Labda Masoud Masoud Manju la Muziki anaweza kutusaidia.
Leo nimezungumza na jamaa zangu Tanga kutafuta habari za Waziri akiwa na Shakila na Lucky Star.
Naambiwa Lucky Star takriban wote wametangulia mbele ya haki hawa ndiyo wangeliweza kunipa historia ya enzi zile.
Lakini sijakata tamaa.
Afrika tuna shida zetu nyingi tu.
Nimemtafuta Stevie Wonder.
Taarifa zake zote zipo kiasi inaweza kukuzamisha ukapotea baharini kwa uzito wake.
Huyo kulia ni Stevie Wonder ambae kama nilivyosema hapo juu alianza muziki wakati mmoja na Maestro na wote wakiwa wapiga kinanda wa sifa.