Tusidanganyane hii yote ni kwa sababu ya PESA tu !!
Pesa zimefanyaje?
Pesa zipo tu ili zipangiwe matumizi kwa ajili ya kuleta matokeo yenye manufaa.
Kama huna watu sahihi wa kutunza pesa, kuzipangia matumizi sahihi, wenye mipango sahihi na endelevu na wenye kufuatilia kuona fedha inatumika kweli katika miradi husika ili ilete matokeo, basi hata uwape pesa zote za dunia hii watu hawa, they won't do anything...watazitapanya tu!
Hawa ndiyo CCM ya leo na ndivyo wanavyofanya!!!
Narudia tena kusema. Tatizo siyo pesa. Tuna matatizo makubwa mawili tu;
[1.] Kwanza linaanzia kwenye mfumo mbaya na dhaifu wa utawala
[2.] Kupitia mfumo huu, tunapata viongozi wa serikali na taasisi zake wabovu wasio na uwezo au wenye uwezo lakini uwezo wao unakuwa spoiled na system mbovu ya kiutawala na kisiasa.
Kutoka kwenye mfumo wa kiutawala mbovu, kunazaliwa series of problems ambayo ni;
✓Sera za hovyo
✓Mipango ya hovyo na isiyo endelevu
✓ Vipaumbele vya hovyo
✓Usimamizi wa hovyo wa mipango hiyo
##Mwisho, hii inakupeleka kwenye matumizi mabaya ya fedha yasiyoleta tija!
Hebu jaribu kutumia akili kidogo tu za kufikiri kwa kujiuliza maswali haya muhimu ya msingi;
1. Kwamba, ni mapesa kiasi gani yameshatupwa kwenye miradi mingi ya umeme ndani ya miaka karibu 30 sasa tangu utawala wa serikali ya awamu ya Mkapa, kisha Kikwete, baadae Magufuli na sasa huyu Mama Samia?
2. Yameleta tija gani katika sekta ya umeme?
3. Yameondoa tatizo la umeme hapa nchini?
4. Ni kipi kipya ambacho Makamba na huyu mama watafanya ambacho wenzao huko nyuma hawakufanya hata kama watapewa $30trilion?
##NARUDIA TENA, shida siyo fedha. Shida ni watu na maamuzi yao na mabovu yakihanikizwa na tamaa, ubinafsi na grand corruption?
Kwanini hamulioni na kuelewa haya mambo rahisi tu kwa kutumia akili ya kawaida tu? Au nyie mmezaliwa jana na hamjui historia ya tatizo la umeme nchi hii?????