Waziri Matiang'i amedhihirisha tunaweza vita dhidi ya ufisadi tukiwa na nia

Waziri Matiang'i amedhihirisha tunaweza vita dhidi ya ufisadi tukiwa na nia

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Mtihani wa darasa la nane umehitimishwa, kawaida tulizoea habari za visa vya udanganyifu miaka yote kila tukifikia mwisho. Lakini waziri na timu yake wamekomaa mwaka huu, waliibuka na mikakati mipya na kwa kweli imefua dafu.

Kila fununu ya tatizo lolote imekuwa ikishughulkiwa kwa nguvu nyingi sana. Watu wachache wamekamatwa kwa kujaribu kuchovya, wao huishi kwa mazoea.

Ama kwa kweli juhudi kama hizi zikitiliwa mkazo na maanani, tutakua na kizazi cha Wakenya wapya waadilifu, na wenye bidii kwenye masuala ya elimu. Maana tukiwanyoosha watoto wetu wakiwa wadogo, lazima hatimaye wataishia kuwa watu wanaostahili kwenye jamii. Taarifa za wazazi kuwanunulia watoto wao mitihani zilikua zinatamausha, maana ndio hapo mbegu ya ufisadi ilikua inafukiwa na kuota.

Kumdhihirishia mtoto kwamba kwa kuhonga anaweza akawa mshindi hata kwenye elimu ni jambo hatari sana kwa jamii. Bora aje na alama mbaya umsaidie kujiboresha lakini sio kumnunulia alama kwenye mtihani eti ndio ahitimu kuingia chuo kikuu. Hao ndio wanaishia kuwa wakurugezi vila.za wasiojua mwanzo au mwisho wa wanakoenda na wanakotoka.

Heko waziri kwa kazi nzuri, kweli tunaweza kushinda vita dhidi ya ufisadi tukimaanisha na bila kuwan na unafiki.
 
Huyo katiba haimzuii kupambana na ufisadi kama Uhuru ama? 🙁🙁🙁

Katiba haizuii na hailindi mtu yeyote kwenye suala la ufisadi. Vita dhidi ya ufisadi huwa nasema vinahusu watu wote bila kumuachia mtu mmoja. Kwa mfano hili la mtihani, Wakenya wote tumeungana, imekua taharuki nchi yote, kwamba ikitajwa hata fununu kwamba kuna mtu kapatikana na makaratasi, Wakenya hawakua wanamsubiri waziri aje afanye chochote, hatua inachukuliwa.

Tatizo lipo sasa mahakamani, wote waliokamatwa itabidi wakawasilishwe mahakamani, na huko ndiko ngoma huanza. Waziri hawezi kuwafuata huko akawaadhibu. Katiba inatenganisha majukumu, ukituhumiwa, polisi wanakukamata, halafu unawasilishwa mahakamani kiongozi wa mashtaka anachukua usukani na hatimaye inakua jukumu la hakimu kuamua nini cha kutendeka. Sio kama huko kwenu rais anaweza hata akapangia mahakama na bunge jinsi ya kutumia hela zao, niliona Magufuli alivyojibu swali fulani linalohusu yeye kuingilia uhuru wa bunge na mahakama.

Vipi kuna sehemu nimeona Mbowe anasema nyie wafuasi wa CCM mumegawana mamilioni kifisadi kwenye huu utawala wa Magufuli.
 
lazima na mimi nipige zangu za haraka...nani mjinga wengine waibe na yeye awe mnyonge tu yani kuwa raia mwema asiyevuna mazao yanapokuwa tayari?
 
Katiba haizuii na hailindi mtu yeyote kwenye suala la ufisadi. Vita dhidi ya ufisadi huwa nasema vinahusu watu wote bila kumuachia mtu mmoja. Kwa mfano hili la mtihani, Wakenya wote tumeungana, imekua taharuki nchi yote, kwamba ikitajwa hata fununu kwamba kuna mtu kapatikana na makaratasi, Wakenya hawakua wanamsubiri waziri aje afanye chochote, hatua inachukuliwa.

Tatizo lipo sasa mahakamani, wote waliokamatwa itabidi wakawasilishwe mahakamani, na huko ndiko ngoma huanza. Waziri hawezi kuwafuata huko akawaadhibu. Katiba inatenganisha majukumu, ukituhumiwa, polisi wanakukamata, halafu unawasilishwa mahakamani kiongozi wa mashtaka anachukua usukani na hatimaye inakua jukumu la hakimu kuamua nini cha kutendeka. Sio kama huko kwenu rais anaweza hata akapangia mahakama na bunge jinsi ya kutumia hela zao, niliona Magufuli alivyojibu swali fulani linalohusu yeye kuingilia uhuru wa bunge na mahakama.

Vipi kuna sehemu nimeona Mbowe anasema nyie wafuasi wa CCM mumegawana mamilioni kifisadi kwenye huu utawala wa Magufuli.


Mbowe kampokea mtuhumiwa wa rushwa kubwa ya kwanza Tz kwenye chama chake baada ya kumsema sana, Mbowe sio mara ya kwanza kusema atatoa ushahidi, alisema angetoa ushahidi kuhusiana na vifo vilitokea kwenye rally ya chama chake arusha, hajawahi kutoa huo ushahidi hadi sasa hivi, huo ni ushahidi kuhusu vifo, jamaa kaleta siasa na hajatoa hadi sasa huo ushahidi, Mbowe anadaiwa kodi kubwa sana na serikali tokea miaka hujazaliwa, wanachohubiri na kutenda ni two diff tings, nimekupa mifano kadhaa ujionee wanasiasa wetu wa upinzani walivo, tungojee tuone kama atatoa ushahidi.
 
Katiba haizuii na hailindi mtu yeyote kwenye suala la ufisadi. Vita dhidi ya ufisadi huwa nasema vinahusu watu wote bila kumuachia mtu mmoja. Kwa mfano hili la mtihani, Wakenya wote tumeungana, imekua taharuki nchi yote, kwamba ikitajwa hata fununu kwamba kuna mtu kapatikana na makaratasi, Wakenya hawakua wanamsubiri waziri aje afanye chochote, hatua inachukuliwa.

Tatizo lipo sasa mahakamani, wote waliokamatwa itabidi wakawasilishwe mahakamani, na huko ndiko ngoma huanza. Waziri hawezi kuwafuata huko akawaadhibu. Katiba inatenganisha majukumu, ukituhumiwa, polisi wanakukamata, halafu unawasilishwa mahakamani kiongozi wa mashtaka anachukua usukani na hatimaye inakua jukumu la hakimu kuamua nini cha kutendeka. Sio kama huko kwenu rais anaweza hata akapangia mahakama na bunge jinsi ya kutumia hela zao, niliona Magufuli alivyojibu swali fulani linalohusu yeye kuingilia uhuru wa bunge na mahakama.

Vipi kuna sehemu nimeona Mbowe anasema nyie wafuasi wa CCM mumegawana mamilioni kifisadi kwenye huu utawala wa Magufuli.

Mbowe huyu huyu aliyetangazia watu kwa miaka 8 kuwa Lowassa ni fisadi na kuishia kumsafisha kwa sekunde moja? Inajulikana wazi kuwa wabunge wa CCM wataupitisha huo mswada wa habari, hawahitaji pesa yoyote kufanya hivyo.
Mbowe anayumbayumba hajui wapi pa kusimamia.
 
Katiba haizuii na hailindi mtu yeyote kwenye suala la ufisadi. Vita dhidi ya ufisadi huwa nasema vinahusu watu wote bila kumuachia mtu mmoja. Kwa mfano hili la mtihani, Wakenya wote tumeungana, imekua taharuki nchi yote, kwamba ikitajwa hata fununu kwamba kuna mtu kapatikana na makaratasi, Wakenya hawakua wanamsubiri waziri aje afanye chochote, hatua inachukuliwa.

Tatizo lipo sasa mahakamani, wote waliokamatwa itabidi wakawasilishwe mahakamani, na huko ndiko ngoma huanza. Waziri hawezi kuwafuata huko akawaadhibu. Katiba inatenganisha majukumu, ukituhumiwa, polisi wanakukamata, halafu unawasilishwa mahakamani kiongozi wa mashtaka anachukua usukani na hatimaye inakua jukumu la hakimu kuamua nini cha kutendeka. Sio kama huko kwenu rais anaweza hata akapangia mahakama na bunge jinsi ya kutumia hela zao, niliona Magufuli alivyojibu swali fulani linalohusu yeye kuingilia uhuru wa bunge na mahakama.

Vipi kuna sehemu nimeona Mbowe anasema nyie wafuasi wa CCM mumegawana mamilioni kifisadi kwenye huu utawala wa Magufuli.

Wabunge wa CCM hawaitaji 10m ili kupitisha chochote, wanahitaji kupigwa mkwara tu na wakuu wao, vilevile it doesn't make any sense ya kusema waziri mkuu anaweza kutoa rushwa kwa wabunge wote wa CCM, sababu atakuwa ni mjinga hata wa kutoa rushwa. Magu hawezi kupoteza hela kizembe wakati kuna njia nyingi tu za ku influence matokeo.
 
Mbowe huyu huyu aliyetangazia watu kwa miaka 8 kuwa Lowassa ni fisadi na kuishia kumsafisha kwa sekunde moja? Inajulikana wazi kuwa wabunge wa CCM wataupitisha huo mswada wa habari, hawahitaji pesa yoyote kufanya hivyo.
Mbowe anayumbayumba hajui wapi pa kusimamia.

Sasa mbona naona hapo kwenye video mnamzima bungeni asitoe ushahidi, wakati anauliza hilo swali, tena kafafanua vizuri kwamba swali lake linahusu sera wakati spika naye amekomalia mambo ya sera.
Mbowe hata kama historia yake sio nzuri, lakini hauwezi kupinga anachokisema kwa kutumia historia yake, unafaa kufuata ukweli upo wapi. Yeye amesema huo ni ufisadi mkubwa ambao haujawahi kutokea katika historia ya Tanzania tena ndani ya utawala wa Magufuli.

Ni kama Raila wa Kenya, japo tunajua kipindi akiwa waziri mkuu Kenya, ofisi yake ilitajwa kwenye ufisadi wa hali ya juu, lakini pia leo hii akizungumzia ufisadi huwa unafuatiliwa hata kama tunajua historia yake. Kwa mfano alitaja ufisadi wa NYS Kenya na ikatokea kuwa kweli.
cc: MwendaOmo
 
Sasa mbona naona hapo kwenye video mnamzima bungeni asitoe ushahidi, wakati anauliza hilo swali, tena kafafanua vizuri kwamba swali lake linahusu sera wakati spika naye amekomalia mambo ya sera.
Mbowe hata kama historia yake sio nzuri, lakini hauwezi kupinga anachokisema kwa kutumia historia yake, unafaa kufuata ukweli upo wapi. Yeye amesema huo ni ufisadi mkubwa ambao haujawahi kutokea katika historia ya Tanzania tena ndani ya utawala wa Magufuli.

Ni kama Raila wa Kenya, japo tunajua kipindi akiwa waziri mkuu Kenya, ofisi yake ilitajwa kwenye ufisadi wa hali ya juu, lakini pia leo hii akizungumzia ufisadi huwa unafuatiliwa hata kama tunajua historia yake. Kwa mfano alitaja ufisadi wa NYS Kenya na ikatokea kuwa kweli.
cc: MwendaOmo
Hii mijitu hata ueleze namna gani hawawezi kukuelewa .
 
Sasa mbona naona hapo kwenye video mnamzima bungeni asitoe ushahidi, wakati anauliza hilo swali, tena kafafanua vizuri kwamba swali lake linahusu sera wakati spika naye amekomalia mambo ya sera.
Mbowe hata kama historia yake sio nzuri, lakini hauwezi kupinga anachokisema kwa kutumia historia yake, unafaa kufuata ukweli upo wapi. Yeye amesema huo ni ufisadi mkubwa ambao haujawahi kutokea katika historia ya Tanzania tena ndani ya utawala wa Magufuli.

Ni kama Raila wa Kenya, japo tunajua kipindi akiwa waziri mkuu Kenya, ofisi yake ilitajwa kwenye ufisadi wa hali ya juu, lakini pia leo hii akizungumzia ufisadi huwa unafuatiliwa hata kama tunajua historia yake. Kwa mfano alitaja ufisadi wa NYS Kenya na ikatokea kuwa kweli.
cc: MwendaOmo
MK254 za kuambiwa changanya na zako, Mbowe ni kiongozi mkubwa ameropoka fulani ametoa rushwa hatoi maelezo wala ushahidi wowote, hizo ni siasa mufilisi ambazo kichaa yoyote anaweza kufanya, ndio maana ameropokea bungeni ambako kuna kinga, anaweza kuita press conference na kutoa ushahidi au hata maelezo, nje ya bunge hakuna kinga, polisi na takukuru watamfuata asaidie uchunguzi kama hutasikia sina imani na chombo chochote cha serikali, atakupa story nyingine ya uchunguzi wa taasis ya nje ya Tz, kwa ufupi Mbowe alikuwa anatafuta political attention tu.
 
Sasa mbona naona hapo kwenye video mnamzima bungeni asitoe ushahidi, wakati anauliza hilo swali, tena kafafanua vizuri kwamba swali lake linahusu sera wakati spika naye amekomalia mambo ya sera.
Mbowe hata kama historia yake sio nzuri, lakini hauwezi kupinga anachokisema kwa kutumia historia yake, unafaa kufuata ukweli upo wapi. Yeye amesema huo ni ufisadi mkubwa ambao haujawahi kutokea katika historia ya Tanzania tena ndani ya utawala wa Magufuli.

Ni kama Raila wa Kenya, japo tunajua kipindi akiwa waziri mkuu Kenya, ofisi yake ilitajwa kwenye ufisadi wa hali ya juu, lakini pia leo hii akizungumzia ufisadi huwa unafuatiliwa hata kama tunajua historia yake. Kwa mfano alitaja ufisadi wa NYS Kenya na ikatokea kuwa kweli.
cc: MwendaOmo
Kumbe na wewe onyango ni bavichaa?
 
Sasa mbona naona hapo kwenye video mnamzima bungeni asitoe ushahidi, wakati anauliza hilo swali, tena kafafanua vizuri kwamba swali lake linahusu sera wakati spika naye amekomalia mambo ya sera.
Mbowe hata kama historia yake sio nzuri, lakini hauwezi kupinga anachokisema kwa kutumia historia yake, unafaa kufuata ukweli upo wapi. Yeye amesema huo ni ufisadi mkubwa ambao haujawahi kutokea katika historia ya Tanzania tena ndani ya utawala wa Magufuli.

Ni kama Raila wa Kenya, japo tunajua kipindi akiwa waziri mkuu Kenya, ofisi yake ilitajwa kwenye ufisadi wa hali ya juu, lakini pia leo hii akizungumzia ufisadi huwa unafuatiliwa hata kama tunajua historia yake. Kwa mfano alitaja ufisadi wa NYS Kenya na ikatokea kuwa kweli.
cc: MwendaOmo
Raila mtu makini kulinganisha na Mbowe, siamini kama kuna siku Raila anaweza kumchukua Anne Waiguru CORD na kuanza kumsafisha.
CCM haiwezi kutoa Tsh 2.7b kuhonga wabunge wake ambao siku zote huunga mkono hoja. Mbowe amepoteza muelekeo kiasi cha kutetea mafisadi Lowassa na Sumaye.
 
Raila mtu makini kulinganisha na Mbowe, siamini kama kuna siku Raila anaweza kumchukua Anne Waiguru CORD na kuanza kumsafisha.
CCM haiwezi kutoa Tsh 2.7b kuhonga wabunge wake ambao siku zote huunga mkono hoja. Mbowe amepoteza muelekeo kiasi cha kutetea mafisadi Lowassa na Sumaye.

Utapata presha kama ajira yako ipo kwenye kuwatetea wanasiasa na ufisadi wao maana wote wanafiki. Iwe wa serikali au wa upinzani, hakuna wa kuaminiwa. Leo unahangaika kuwatetea wanaotajwa kisa ni CCM yako, kesho wakihamia upinzani utawaponda.
Nawaelewa wanasiasa wa nchi zote mbili, tena vizuri tu.

Kenya, Raila unayemsema hawezi kuwapokea mafisadi CORD, ikuingie tayari amempokea aliyekua waziri Ngilu ambaye alipigwa chini na rais Uhuru kwa ufisadi. Anatupa mawe kwenye serikali kwamba wapige chini mafisadi, halafu papo hapo anawapokea wakija kwake.

Unafiki wa Afrika huwa unanichosha sana. Hakuna msafi hata mmoja, hata Uhuru na naibu wake Ruto likija kwa ufisadi sio wa kuamini.
 
Utapata presha kama ajira yako ipo kwenye kuwatetea wanasiasa na ufisadi wao maana wote wanafiki. Iwe wa serikali au wa upinzani, hakuna wa kuaminiwa. Leo unahangaika kuwatetea wanaotajwa kisa ni CCM yako, kesho wakihamia upinzani utawaponda.
Nawaelewa wanasiasa wa nchi zote mbili, tena vizuri tu.

Kenya, Raila unayemsema hawezi kuwapokea mafisadi CORD, ikuingie tayari amempokea aliyekua waziri Ngilu ambaye alipigwa chini na rais Uhuru kwa ufisadi. Anatupa mawe kwenye serikali kwamba wapige chini mafisadi, halafu papo hapo anawapokea wakija kwake.

Unafiki wa Afrika huwa unanichosha sana. Hakuna msafi hata mmoja, hata Uhuru na naibu wake Ruto likija kwa ufisadi sio wa kuamini.
Mimi sio mwanachama wa CCM wala sijawahi kupiga kura tokea kuzaliwa, siwaamini wanasiasa hata kidogo. Natumia akili yangu kwa kila jambo, sijawaachia wanasiasa wautumie ubongo wangu.
Ukweli unabaki palepale, hakuna hata siku moja CCM wakapinga mswada wowote ambao unaungwa mkono na serikali. Mbowe anaongea bila ushahidi wowote hatuwezi kumtilia maanani.
 
Kesi ya ccm na rushwa kumpelekea Magufuli wanajisumbuwa. Kesi ya nyani hakimu tumbili.
 
Mtihani wa darasa la nane umehitimishwa, kawaida tulizoea habari za visa vya udanganyifu miaka yote kila tukifikia mwisho. Lakini waziri na timu yake wamekomaa mwaka huu, waliibuka na mikakati mipya na kwa kweli imefua dafu.

Kila fununu ya tatizo lolote imekuwa ikishughulkiwa kwa nguvu nyingi sana. Watu wachache wamekamatwa kwa kujaribu kuchovya, wao huishi kwa mazoea.

Ama kwa kweli juhudi kama hizi zikitiliwa mkazo na maanani, tutakua na kizazi cha Wakenya wapya waadilifu, na wenye bidii kwenye masuala ya elimu. Maana tukiwanyoosha watoto wetu wakiwa wadogo, lazima hatimaye wataishia kuwa watu wanaostahili kwenye jamii. Taarifa za wazazi kuwanunulia watoto wao mitihani zilikua zinatamausha, maana ndio hapo mbegu ya ufisadi ilikua inafukiwa na kuota.

Kumdhihirishia mtoto kwamba kwa kuhonga anaweza akawa mshindi hata kwenye elimu ni jambo hatari sana kwa jamii. Bora aje na alama mbaya umsaidie kujiboresha lakini sio kumnunulia alama kwenye mtihani eti ndio ahitimu kuingia chuo kikuu. Hao ndio wanaishia kuwa wakurugezi vila.za wasiojua mwanzo au mwisho wa wanakoenda na wanakotoka.

Heko waziri kwa kazi nzuri, kweli tunaweza kushinda vita dhidi ya ufisadi tukimaanisha na bila kuwan na unafiki.

Kweli hapo namweshimu Matiangi. Ndiposa aitwa Magufuli wa Kenya kweli. Hatujamuona akilalamika eti ohh polisi, sijui KNEC, sijui EACC. Au arushe mikono juu aulize sasa nifanyeje? Lazima tuwe na individuals wenye nia ya kupigana na ufisadi ndiposa taasisi zetuziweze kufanya kazi. Kutegemea tu eti taasisi zifanye kazi, ni kujidanganya. Sasa hivi sijui Jacob Kaimenyi afanya kazi ipi?
 
Back
Top Bottom