Waziri Mbarawa: Treni za SGR zitakuwa na uwezo wa kubeba mzigo wa Tani 10,000 kwa mkupuo sawa na Malori 500

Waziri Mbarawa: Treni za SGR zitakuwa na uwezo wa kubeba mzigo wa Tani 10,000 kwa mkupuo sawa na Malori 500

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amesema Treini za kisasa zitakuwa na uwezo wa kubeba tani 10,000 kwa mkupuo jambo amesema kuwa ni sawa na mzigo ambao unabebwa na malori 500.

photo_2024-07-30_14-41-27 (2).jpg
"Treni za kisasa zenye kutumia nishati ya umeme, zitakuwa na uwezo wa kubeba mzigo mkubwa hadi tani 10,000 kwa mkupuo ambazo ni sawa na malori 500 ya mizigo ambapo itapunguza mrundikano wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam na kupunguza uharibifu wa barabara.

Aidha, kupitia mradi huu Tanzania imekuwa nchi ya kwanza Afrika na ya tano Duniani kwa kuwa na Mtandao mrefu zaidi wa reli ya SGR," amesema Mbarawa.

photo_2024-07-30_14-41-27.jpg

Amedai kuwa hatua hiyo itasaidia kuepusha uharibifu wa barabara, kuongeza mapato, kukuza maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa kutoa huduma ya usafiri wa uhakika.

"Kuanza kwa huduma za usafiri katika reli ya kiwango cha kimataifa kutachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la pato la taifa pamoja na maendeleo ya shughuli nyingi za kiuchumi, kijamii na kiutawala kwa kutoa usafiri wa uhakika na wa haraka. Sekta ambazo zinatarajiwa kuguswa moja kwa moja na usafiri wa reli ya SGR ni pamoja na Biashara, Utalii, Viwanda, Kilimo, Uvuvi na Ufugaji," amesema Mbarawa.

Aidha ameeleza kuwa mpaka sasa Serikali imeshatumia kiasi cha Dola za Marekani bilioni 3.138 kwa ujenzi wa miundombinu ya SGR kwa vipande viwili vya Dar es Salaam - Morogoro-Makutopora Dodoma jumla ya kilomita 722, ambapo amesema kwamba kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro zimetumika Dola za Marekani Dola Bilioni 1.215 na kipande cha Morogoro hadi Makutopora Dodoma zimetumika Dola za Marekani Bilioni 1.923.

Ameyasema hayo Julai 30, 20 wakati akizungumza na vyombo vya habari kuelekea uzinduzi rasmi wa ruti ya Treini Dar es Salaam - Dodoma, ambao utafanyika August 1, 2024 Jijini Dodoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
 
Kama ni hivyo basi serikali ingejenga haraka sana na kipande cha reli kuelekea zambia ili kurahisisha ysafiri huo na kuvutia wawekezaji zaidi.

Pia baadae ijenge na reli kutoka dar kwenda kaskazini tanga, kilimanjaro, na arusha maana pia huko itavutia watalii, wasafiri na mizigo pia.
 
Watulize akili tu, reli ina faida nyingi ila kwa laana za kitanzania utashangaa wanaharibu kusudi, wanashindwa kuendesha ili waje wampangishe mtu wapige 10%
 
Kama ni hivyo basi serikali ingejenga haraka sana na kipande cha reli kuelekea zambia ili kurahisisha ysafiri huo na kuvutia wawekezaji zaidi.

Pia baadae ijenge na reli kutoka dar kwenda kaskazini tanga, kilimanjaro, na arusha maana pia huko itavutia watalii, wasafiri na mizigo pia.
Ya Arusha inaweza anzia Kilosa...Inawezekana ni fupi sana hiyo route
 
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amesema Treini za kisasa zitakuwa na uwezo wa kubeba tani 10,000 kwa mkupuo jambo amesema kuwa ni sawa na mzigo ambao unabebwa na malori 500.
"Treni za kisasa zenye kutumia nishati ya umeme, zitakuwa na uwezo wa kubeba mzigo mkubwa hadi tani 10,000 kwa mkupuo ambazo ni sawa na malori 500 ya mizigo ambapo itapunguza mrundikano wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam na kupunguza uharibifu wa barabara.

Aidha, kupitia mradi huu Tanzania imekuwa nchi ya kwanza Afrika na ya tano Duniani kwa kuwa na Mtandao mrefu zaidi wa reli ya SGR," amesema Mbarawa
Amedai kuwa hatua hiyo itasaidia kuepusha uharibifu wa barabara, kuongeza mapato, kukuza maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa kutoa huduma ya usafiri wa uhakika.

"Kuanza kwa huduma za usafiri katika reli ya kiwango cha kimataifa kutachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la pato la taifa pamoja na maendeleo ya shughuli nyingi za kiuchumi, kijamii na kiutawala kwa kutoa usafiri wa uhakika na wa haraka. Sekta ambazo zinatarajiwa kuguswa moja kwa moja na usafiri wa reli ya SGR ni pamoja na Biashara, Utalii, Viwanda, Kilimo, Uvuvi na Ufugaji," amesema Mbarawa.

Aidha ameeleza kuwa mpaka sasa Serikali imeshatumia kiasi cha Dola za Marekani bilioni 3.138 kwa ujenzi wa miundombinu ya SGR kwa vipande viwili vya Dar es Salaam - Morogoro-Makutopora Dodoma jumla ya kilomita 722, ambapo amesema kwamba kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro zimetumika Dola za Marekani Dola Bilioni 1.215 na kipande cha Morogoro hadi Makutopora Dodoma zimetumika Dola za Marekani Bilioni 1.923.

Ameyasema hayo Julai 30, 20 wakati akizungumza na vyombo vya habari kuelekea uzinduzi rasmi wa ruti ya Treini Dar es Salaam - Dodoma, ambao utafanyika August 1, 2024 Jijini Dodoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Na nchi ya kwanza kwa wizi wa kura kisini mwa jangwa la Sahara, pia nchi ya kwanza duniani chama tawala kuwa cha kifamilia.
 
Back
Top Bottom