Waziri Mkenda: Ni marufuku kumfukuza Mwanafunzi kwa kushindwa kuchangia mchango wowote

Waziri Mkenda: Ni marufuku kumfukuza Mwanafunzi kwa kushindwa kuchangia mchango wowote

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Snapinsta.app_452870052_991993826039393_2671002642674282009_n_1080.jpg
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema ni marufuku Mwanafunzi yeyote kufukuzwa kwenye shule za umma, kurudishwa nyumbani kwa sababu mzazi ameshindwa kuchangia mchango wowote ikiwemo huduma za chakula.

Mkenda ametoa agizo hilo Julai 26, 2024 jijini Dodoma wakati akizungumza katika Kongamano la Utoaji Chakula na Lishe Shuleni, akisisitiza mzazi anayekataa kuchangia mchango uliowekwa kulingana na miongozo waliyojiwekea Mamlaka za Serikali za Mitaa zinaweza kuchukua hatua dhidi ya mzazi wakati Mwanafunzi akiendelea na masomo.
Snapinsta.app_452403801_1004249451197435_1431095065571710978_n_1080.jpg
Akihutubia Kongamano hilo Waziri huyo amewataka Wadau mbalimbali kuendelea kushirikiana kuhamasisha huduma ya chakula kwa Wanafunzi wakiwa shuleni.

"Lishe bora shuleni ni msingi muhimu katika maendeleo ya kiafya na kiakili na kwamba inachangia Mwanafunzi kujifunzaji kwa ufanisi. Mwanafunzi anapokosa chakula hukabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo njaa, utoro wa rejareja na hata kukatisha masomo kwa baadhi yao," alisema Mkenda.

Chanzo: Wizara ya Elimu


=========

Pia soma...
~ Wazazi wa wanafunzi Shule ya Sekondari BUJUNANGOMA, tumechoka na Michango, Rushwa, Utumikishwaji wa watoto wetu shuleni
~ Shule ya Msingi Tumaini ya Tabata Kimanga Wanafunzi wasiochangia Tsh. 800 wanatolewa Darasani
~ Malalamiko yaendelea kuhusu malipo ya 'Mchango wa Uendeshaji wa Shule Tsh 65,000' licha ya Serikali kufuta ada
~ Wanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Chanika wazuiliwa kuingia darasani kutokana na kutochangia 500 ya masomo
 
Kwa Nini asifukuzwe ni asile basi maisha yaendelee
 
Vikoba na kaushadamu walimu watalipa na nini?
Mhe. Waziri Mkenda, walimu wako huko damu zinakaushwa.

Walimu wa kike kimekuwa chakula cha bodaboda, Vijana wanajipigia watakavyo.
Hiyo michango ya chakula inawapa unafuu wa kulipa mikopo umiza.
 
Bajeti bilioni 9 wamepewa MADC huko elimu milioni 56 ni heri wakoloni wangebaki
 
Haya mambo mengine magumu sana,mbaya Zaidi kuna watu bila kutake action hawatekelezi,imagine umempeleka mwanao shule kila kitu ukalipa safi mwisho wa siku mtoto anakupigia simu baba au mama nimelala njaa siku ya pili leo unauliza sababu anakwambia chakula shule kimeisha kwasababu baadhi ya watu hawajatoa Hela utajisikaje?Sina hakika kama kuna budget ya kufidia Kwa wale watakaoshindwa kulipia.
 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema ni marufuku Mwanafunzi yeyote kufukuzwa kwenye shule za umma, kurudishwa nyumbani kwa sababu mzazi ameshindwa kuchangia mchango wowote ikiwemo huduma za chakula.

Mkenda ametoa agizo hilo Julai 26, 2024 jijini Dodoma wakati akizungumza katika Kongamano la Utoaji Chakula na Lishe Shuleni, akisisitiza mzazi anayekataa kuchangia mchango uliowekwa kulingana na miongozo waliyojiwekea Mamlaka za Serikali za Mitaa zinaweza kuchukua hatua dhidi ya mzazi wakati Mwanafunzi akiendelea na masomo.
Akihutubia Kongamano hilo Waziri huyo amewataka Wadau mbalimbali kuendelea kushirikiana kuhamasisha huduma ya chakula kwa Wanafunzi wakiwa shuleni.

"Lishe bora shuleni ni msingi muhimu katika maendeleo ya kiafya na kiakili na kwamba inachangia Mwanafunzi kujifunzaji kwa ufanisi. Mwanafunzi anapokosa chakula hukabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo njaa, utoro wa rejareja na hata kukatisha masomo kwa baadhi yao," alisema Mkenda.

Chanzo: Wizara ya Elimu


=========

Pia soma...
~ Wazazi wa wanafunzi Shule ya Sekondari BUJUNANGOMA, tumechoka na Michango, Rushwa, Utumikishwaji wa watoto wetu shuleni
~ Shule ya Msingi Tumaini ya Tabata Kimanga Wanafunzi wasiochangia Tsh. 800 wanatolewa Darasani
~ Malalamiko yaendelea kuhusu malipo ya 'Mchango wa Uendeshaji wa Shule Tsh 65,000' licha ya Serikali kufuta ada
~ Wanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Chanika wazuiliwa kuingia darasani kutokana na kutochangia 500 ya masomo
Kazi Ipo
 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema ni marufuku Mwanafunzi yeyote kufukuzwa kwenye shule za umma, kurudishwa nyumbani kwa sababu mzazi ameshindwa kuchangia mchango wowote ikiwemo huduma za chakula.

Mkenda ametoa agizo hilo Julai 26, 2024 jijini Dodoma wakati akizungumza katika Kongamano la Utoaji Chakula na Lishe Shuleni, akisisitiza mzazi anayekataa kuchangia mchango uliowekwa kulingana na miongozo waliyojiwekea Mamlaka za Serikali za Mitaa zinaweza kuchukua hatua dhidi ya mzazi wakati Mwanafunzi akiendelea na masomo.
Akihutubia Kongamano hilo Waziri huyo amewataka Wadau mbalimbali kuendelea kushirikiana kuhamasisha huduma ya chakula kwa Wanafunzi wakiwa shuleni.

"Lishe bora shuleni ni msingi muhimu katika maendeleo ya kiafya na kiakili na kwamba inachangia Mwanafunzi kujifunzaji kwa ufanisi. Mwanafunzi anapokosa chakula hukabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo njaa, utoro wa rejareja na hata kukatisha masomo kwa baadhi yao," alisema Mkenda.

Chanzo: Wizara ya Elimu


=========

Pia soma...
~ Wazazi wa wanafunzi Shule ya Sekondari BUJUNANGOMA, tumechoka na Michango, Rushwa, Utumikishwaji wa watoto wetu shuleni
~ Shule ya Msingi Tumaini ya Tabata Kimanga Wanafunzi wasiochangia Tsh. 800 wanatolewa Darasani
~ Malalamiko yaendelea kuhusu malipo ya 'Mchango wa Uendeshaji wa Shule Tsh 65,000' licha ya Serikali kufuta ada
~ Wanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Chanika wazuiliwa kuingia darasani kutokana na kutochangia 500 ya masomo
Huyu naye ni boya tu! Kila siku mnatoa kauli kama hizo lakini walimu wooooooooooooooooooote wa primary wanatenda makatazo hayo hayo na hamchukui hatua yoyote! sasa hivi uji ni lazima, 220 kila siku, mtihani kila siku kwa 1000, kila leo mitihani...mradi wa walimu
 
Kijana wa binamu yangu kesho anaenda kuanza wiki ya pili nyumbani kwa kusimamishwa shule sababu ya Ada ambayo imebaki elfu 70 kwenye 551000 kwa mwaka mzima. Mwalimu mkuu kwenye shule hiyo ya English medium ya serikali huko kwa mkwawa.
Ushauri wangu kwenu wazazi tuwasomeshe watoto wetu kwenye shule zisizo na Ada ili kuepukana na hii adha. Inawezekana yule mwalimu mkuu yupo sahihi kuwarudisha watoto nyumbani kutokana na kukosa mshahara wa kuwalipa walimu kwenye shule yake hivyo si rahisi akaenda Sawasawa na TAMKO la waziri
 
Mzazi atachukuliwa hatua gani?
 
Back
Top Bottom