Ni takribani Mwaka wa 2 sasa tangu Serikali ya Awamu ya 6 iingie Madarakani. Serikali iliyojipambanua kwa kufungua mipaka na kuichora upya ramani ya Tanzania kwenye ramani ya dunia. Katika safari hii yenye mafanikio makubwa na matumaini kwa Watanzania, Mh Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan , Makamu wa Rais Dr.Mpango na Waziri Mkuu Majaliwa K. Majaliwa wamekuwa mifano ya kuigwa kwa hatua za kiutendaji wanazozichukua kila kukicha.
Pamoja na uwezo huo unaoneshwa na Viongozi hawa, hivi sasa nchini kumetokea tabia ya ajabu kabisa ambayo inafanywa na watu waliopata jina pendwa la MACHAWA🕷️🕷️🕷️🕷️ yaani wala Rushwa . Machawa hawa wameamua kujipa kazi moja tu ya kusambaza chuki baina ya Viongozi ili Viongozi wetu watofautiane na washindwe kufanya kazi kwa ushirikiano na kuaminiana. TUMEWASHTUKIA na hamtafanikiwa kwa kuwa agenda zenu zote tunazijua.
Hivi majuzi Mama akiwa kwenye Mkutano mkuu wa chama cha mapinduzi alisikika akiahidi kuipanga Serikali yake upya kwa sababu aliyoitaja kuwa wapo watu kwenye Serikali yake wasioendana na kasi yake. "Sisi wananchi tunakubaliana na Mama kabisa kwamba kuna watu hawaendani na kasi yake na sisi wananchi tunamuunga mkono kuchukua hatua maana ndio hao wanaomrudisha nyuma yeye na Serikali.” Inashangaza sana unakuta kwenye Sekta mbalimbali kuna madudu na mawaziri husika wapo na Viongozi wa ngazi za Mkoa ,Wilaya na Wakurugenzi wa Almashauri wapo ila wanasubiri Waziri Mkuu afanye ziara ndio yagundulike madudu, hii si sawasawa na ndio maana tunaunga mkono nia ya mama ya kufanya mabadiliko.
Hata hivyo, MACHAWA wametafsiri wanavyotaka wao kwa nia zao ovu, wakiwa na mpango wao wa kuendeleza NONGWA mitandaoni.
Wapo MACHAWA wanaojenga hoja kuwa Waziri Mkuu hatakiwi kukaa muda mrefu kwenye Serikali . Kiufupi hoja yao hii haina msingi wowote, ebu tujikumbushe kidogo
mifano kutoka hapa nchini na nchi zilizoendelea hasa Uingereza, ambako Robert Walpole Waziri Mkuu wa Uingereza aliekaa muda mrefu zaidi alieongoza Serikali kwa miaka 21, lakini pia hapa nchini tunae Waziri mkuu mstaafu Mhe. Fredrick Sumaye aiehudumu kwa miaka 10, kwakuwa kinachoangaliwa ni utendaji wake na namna anavyomsaidia kazi Rais wake.
Waziri Mkuu ambae ni mtendaji mkuu serikalini amekuwa akiendeleza kasi yake ile ile ya kiutendaji kila kukicha, na ambaye kupitia ziara zake amekuwa akiibua mambo mbalimbali kama vile utendaji usioridhisha kwa baadhi ya watumishi na matumizi mabaya ya fedha za umma kwa baadhi ya maeneo mbalimbali nchini.
Tunafahamu ya kwamba kwa miaka 2 ya Mhe. Samia fedha nyingi zimepelekwa maeneo mbalimbali nchini kutekeleza miradi ya maendeleo na mara kwa mara amekuwa akisisitiza uadilifu katika matumizi ya fedha hizo. Na ndio maana Waziri Mkuu wake amekuwa mkali katika kufatilia matumizi ya fedha hizo.Waziri Mkuu ameibua na kuweka wazi ufujaji wa pesa za Serikali kwenye miradi ya maendeleo na katika maeneo baadhi ya utendaji, na hata kuikataa miradi ambayo hakuridhishwa na utendaji wake mzalendo huyu. Mara kadhaa kupitia mikutano yake Mhe. Dr. Samia Suluhu Hasan Rais wetu ,amekuwa akionya vikali utendaji mbovu, wizi wa fedha za umma, miradi isiyokidhi viwango na kwamba wale wote watakaojihusisha atawaonyesha rangi zake. Hivyo anachokifanya waziri Mkuu ni kutekeleza maagizo . Niukweli usiopingika kwamba hatua zinazochukuliwa ndizo wananchi tunazotaka kuziona zikichukuliwa na Viongozi wetu tuliowapa dhamana ya kutuongoza.
Wakati MACHAWA wanamwaga sifa za kujipendekeza kwa maneno bila vitendo, ni kipindi hicho hicho mchapa kazi PM yupo bize na maswala ya msingi kwenye utendaji AKIMSAIDIA MAMA KWA VITENDO, ameibua madudu ya baadhi wa watumishi wanaofuja fedha na mali za umma kupitia ziara zake .
Sisi watanzania tunamwelewa Waziri Mkuu na dhamira yake njema ya utendaji na KUMSAIDIA Mheshimiwa Rais majukumu yake kuliko hao wanaoshinda mitandaoni wakiwachonganisha viongozi. Watanzania tunaona na tuna macho, tunanajua ni nani anawajibika katika majukumu yake kumsaidia Rais na ni nani yupo bize kusaka madaraka 2025. Waziri Mkuu ni mchapa kazi na kazi lazima ziendelee.
Wananchi tunapenda kuona watu wenye uchungu na rasilimali za taifa, watu wenye matendo kuliko maneno, watu wanaojua mahitaji ya nchi kwa sasa. Tunahitaji kuona RUSHWA inapungua/inaisha, tuwe na UMEME, MAJI, na VITUO vya AFYA, Taifa hili la uwekezaji linahitaji umeme wa uhakika na sio mgao usioisha.
MACHAWA TUSIKILIZANE “Mama yetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wake Dkt. Mpango, na Waziri Mkuu Mh. Majaliwa ni mpango wa Mungu” na wana nia ya dhati ya kulikomboa taifa hili. Sisi wananchi tunasimama na Mama na Wasaidizi wake wote wenye nia njema na nchi yetu kwa umoja wao na KAZI IENDELEE…..
Mwananchi
Issa Mkuya
Pamoja na uwezo huo unaoneshwa na Viongozi hawa, hivi sasa nchini kumetokea tabia ya ajabu kabisa ambayo inafanywa na watu waliopata jina pendwa la MACHAWA🕷️🕷️🕷️🕷️ yaani wala Rushwa . Machawa hawa wameamua kujipa kazi moja tu ya kusambaza chuki baina ya Viongozi ili Viongozi wetu watofautiane na washindwe kufanya kazi kwa ushirikiano na kuaminiana. TUMEWASHTUKIA na hamtafanikiwa kwa kuwa agenda zenu zote tunazijua.
Hivi majuzi Mama akiwa kwenye Mkutano mkuu wa chama cha mapinduzi alisikika akiahidi kuipanga Serikali yake upya kwa sababu aliyoitaja kuwa wapo watu kwenye Serikali yake wasioendana na kasi yake. "Sisi wananchi tunakubaliana na Mama kabisa kwamba kuna watu hawaendani na kasi yake na sisi wananchi tunamuunga mkono kuchukua hatua maana ndio hao wanaomrudisha nyuma yeye na Serikali.” Inashangaza sana unakuta kwenye Sekta mbalimbali kuna madudu na mawaziri husika wapo na Viongozi wa ngazi za Mkoa ,Wilaya na Wakurugenzi wa Almashauri wapo ila wanasubiri Waziri Mkuu afanye ziara ndio yagundulike madudu, hii si sawasawa na ndio maana tunaunga mkono nia ya mama ya kufanya mabadiliko.
Hata hivyo, MACHAWA wametafsiri wanavyotaka wao kwa nia zao ovu, wakiwa na mpango wao wa kuendeleza NONGWA mitandaoni.
Wapo MACHAWA wanaojenga hoja kuwa Waziri Mkuu hatakiwi kukaa muda mrefu kwenye Serikali . Kiufupi hoja yao hii haina msingi wowote, ebu tujikumbushe kidogo
mifano kutoka hapa nchini na nchi zilizoendelea hasa Uingereza, ambako Robert Walpole Waziri Mkuu wa Uingereza aliekaa muda mrefu zaidi alieongoza Serikali kwa miaka 21, lakini pia hapa nchini tunae Waziri mkuu mstaafu Mhe. Fredrick Sumaye aiehudumu kwa miaka 10, kwakuwa kinachoangaliwa ni utendaji wake na namna anavyomsaidia kazi Rais wake.
Waziri Mkuu ambae ni mtendaji mkuu serikalini amekuwa akiendeleza kasi yake ile ile ya kiutendaji kila kukicha, na ambaye kupitia ziara zake amekuwa akiibua mambo mbalimbali kama vile utendaji usioridhisha kwa baadhi ya watumishi na matumizi mabaya ya fedha za umma kwa baadhi ya maeneo mbalimbali nchini.
Tunafahamu ya kwamba kwa miaka 2 ya Mhe. Samia fedha nyingi zimepelekwa maeneo mbalimbali nchini kutekeleza miradi ya maendeleo na mara kwa mara amekuwa akisisitiza uadilifu katika matumizi ya fedha hizo. Na ndio maana Waziri Mkuu wake amekuwa mkali katika kufatilia matumizi ya fedha hizo.Waziri Mkuu ameibua na kuweka wazi ufujaji wa pesa za Serikali kwenye miradi ya maendeleo na katika maeneo baadhi ya utendaji, na hata kuikataa miradi ambayo hakuridhishwa na utendaji wake mzalendo huyu. Mara kadhaa kupitia mikutano yake Mhe. Dr. Samia Suluhu Hasan Rais wetu ,amekuwa akionya vikali utendaji mbovu, wizi wa fedha za umma, miradi isiyokidhi viwango na kwamba wale wote watakaojihusisha atawaonyesha rangi zake. Hivyo anachokifanya waziri Mkuu ni kutekeleza maagizo . Niukweli usiopingika kwamba hatua zinazochukuliwa ndizo wananchi tunazotaka kuziona zikichukuliwa na Viongozi wetu tuliowapa dhamana ya kutuongoza.
Wakati MACHAWA wanamwaga sifa za kujipendekeza kwa maneno bila vitendo, ni kipindi hicho hicho mchapa kazi PM yupo bize na maswala ya msingi kwenye utendaji AKIMSAIDIA MAMA KWA VITENDO, ameibua madudu ya baadhi wa watumishi wanaofuja fedha na mali za umma kupitia ziara zake .
Sisi watanzania tunamwelewa Waziri Mkuu na dhamira yake njema ya utendaji na KUMSAIDIA Mheshimiwa Rais majukumu yake kuliko hao wanaoshinda mitandaoni wakiwachonganisha viongozi. Watanzania tunaona na tuna macho, tunanajua ni nani anawajibika katika majukumu yake kumsaidia Rais na ni nani yupo bize kusaka madaraka 2025. Waziri Mkuu ni mchapa kazi na kazi lazima ziendelee.
Wananchi tunapenda kuona watu wenye uchungu na rasilimali za taifa, watu wenye matendo kuliko maneno, watu wanaojua mahitaji ya nchi kwa sasa. Tunahitaji kuona RUSHWA inapungua/inaisha, tuwe na UMEME, MAJI, na VITUO vya AFYA, Taifa hili la uwekezaji linahitaji umeme wa uhakika na sio mgao usioisha.
MACHAWA TUSIKILIZANE “Mama yetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wake Dkt. Mpango, na Waziri Mkuu Mh. Majaliwa ni mpango wa Mungu” na wana nia ya dhati ya kulikomboa taifa hili. Sisi wananchi tunasimama na Mama na Wasaidizi wake wote wenye nia njema na nchi yetu kwa umoja wao na KAZI IENDELEE…..
Mwananchi
Issa Mkuya