MHASIBU HALISI
Member
- Aug 10, 2011
- 35
- 13
Ni hivi majuzi tu Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda aliunda tume kuchunguza sababu za kufeli kwa wanafunzi wa Form Four iliyopelekea kuwa na matokeo mabaya nchi nzima.
Tunakuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu kuunda tume nyingine ili kuchunguza kuwepo kwa matokeo mabovu kila mwaka kwa miaka nenda rudi kwa watahiniwa wa mitihani ya CPA (Certified Public Accountant) inayotolewa na Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi wa mahesabu (NBAA).
Tunasema kuna umuhimu wa kuunda tume kuchunguza bodi hii kutokana na ukweli kwamba mitihani inayotolewa na bodi hii ni ya kukomoana sana.Lengo lao ni kuhakikisha kwamba wanaopata hiyo CPA wawe wachache mno. Kwa mfano wanaweza wakafanya mitihani hiyo watahiniwa zaidi ya elfu tatu (3,000) lakini watakaopata hiyo CPA ni chini ya watahiniwa mia tatu tu (300).
Sisi wahasibu tunaona bodi hii haikuundwa kuendeleza taaluma hii ya uhasibu bali ni kuididimiza taaluma hii ili kuwe na wahasibu wachache mno wenye sifa za kuitwa wahasibu. Kwa sababu kwa mujibu wa Ndugu Ludovick Utouh ambae ni mkaguzi mkuu wa serikali (CAG) anamtambua mhasibu ni yule mwenye CPA tu. Hawa wengine wanaofanya kazi za uhasibu lakini hawana CPA wanajipendekeza tu na ndio wanaoharibu kazi na sifa za taaluma ya uhasibu.
Bodi hii ya NBAA imejihakikishia maisha ya kifahari kwa kila mtumishi wake kutokana na kukusanya mabilioni ya pesa ya bure kutoka kwa watahiniwa wa mitihani yake.
Kwa mfano hii sheria waliyoiweka ya kwamba Mtahiniwa akifanya mitihani na kufaulu somo moja basi wanalifuta, ni sheria kandamizi yenye lengo la kuwarudisha nyuma watu wanaopenda kujiendeleza katika fani hii na vile vile kuleta aina mpya ya UTUMWA kupitia sekta ya elimu. Yaani mtu atumie robo tatu ya umri wake wa kufanya kazi akiwa anasoma.
Sisi binafsi(Wahasibu) hatuelewi kama mtu somo amefaulu eti kwa kuwa ni moja linafutwa kwa nini ? Wakati mpaka huyo mtu amelifaulu hilo somo ametumia rasirimali chungu nzima ikiwemo Muda,Fedha na Jitihada kubwa mpaka kufaulu somo hilo.
Imefikia mahala waajiri wengi hawataki kuwalipia wala kuwaruhusu wafanyakazi wao kufanya mitihani hii kwa kuwa wameona ni kupoteza muda na rasilimali tu. Mtu badala ya kutumia muda wake mwingi katika kufanya kazi ili kuinua uchumi wa taifa, badala yake anatumia muda mwingi kusomea CPA ambayo kuipata kwake ni mpaka Mabwana wakubwa wa NBAA watakapokuwa tayari kukupa. Tunasikitika sana kuona nchi kama ya Uingereza ambayo imetuacha mbali mno kiuchumi na kimaendeleo kwa ujumla, ukifanya mitihani yao ya ACCA hata kama ni somo moja moja na ukafulu wanali-record na unamalizia mengine yaliyobaki. Lakini kwa NBAA ukifaulu somo moja wanalifuta.
Kwa kumalizia tunakuomba Mheshimiwa Waziri mkuu, usisubiri mpaka kutokee maandamano unda tume kuchunguza utendaji kazi wa Bodi ya NBAA kwani imekithiri kwa kufelisha watahiniwa wake kwa makusudi.
Tunakuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu kuunda tume nyingine ili kuchunguza kuwepo kwa matokeo mabovu kila mwaka kwa miaka nenda rudi kwa watahiniwa wa mitihani ya CPA (Certified Public Accountant) inayotolewa na Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi wa mahesabu (NBAA).
Tunasema kuna umuhimu wa kuunda tume kuchunguza bodi hii kutokana na ukweli kwamba mitihani inayotolewa na bodi hii ni ya kukomoana sana.Lengo lao ni kuhakikisha kwamba wanaopata hiyo CPA wawe wachache mno. Kwa mfano wanaweza wakafanya mitihani hiyo watahiniwa zaidi ya elfu tatu (3,000) lakini watakaopata hiyo CPA ni chini ya watahiniwa mia tatu tu (300).
Sisi wahasibu tunaona bodi hii haikuundwa kuendeleza taaluma hii ya uhasibu bali ni kuididimiza taaluma hii ili kuwe na wahasibu wachache mno wenye sifa za kuitwa wahasibu. Kwa sababu kwa mujibu wa Ndugu Ludovick Utouh ambae ni mkaguzi mkuu wa serikali (CAG) anamtambua mhasibu ni yule mwenye CPA tu. Hawa wengine wanaofanya kazi za uhasibu lakini hawana CPA wanajipendekeza tu na ndio wanaoharibu kazi na sifa za taaluma ya uhasibu.
Bodi hii ya NBAA imejihakikishia maisha ya kifahari kwa kila mtumishi wake kutokana na kukusanya mabilioni ya pesa ya bure kutoka kwa watahiniwa wa mitihani yake.
Kwa mfano hii sheria waliyoiweka ya kwamba Mtahiniwa akifanya mitihani na kufaulu somo moja basi wanalifuta, ni sheria kandamizi yenye lengo la kuwarudisha nyuma watu wanaopenda kujiendeleza katika fani hii na vile vile kuleta aina mpya ya UTUMWA kupitia sekta ya elimu. Yaani mtu atumie robo tatu ya umri wake wa kufanya kazi akiwa anasoma.
Sisi binafsi(Wahasibu) hatuelewi kama mtu somo amefaulu eti kwa kuwa ni moja linafutwa kwa nini ? Wakati mpaka huyo mtu amelifaulu hilo somo ametumia rasirimali chungu nzima ikiwemo Muda,Fedha na Jitihada kubwa mpaka kufaulu somo hilo.
Imefikia mahala waajiri wengi hawataki kuwalipia wala kuwaruhusu wafanyakazi wao kufanya mitihani hii kwa kuwa wameona ni kupoteza muda na rasilimali tu. Mtu badala ya kutumia muda wake mwingi katika kufanya kazi ili kuinua uchumi wa taifa, badala yake anatumia muda mwingi kusomea CPA ambayo kuipata kwake ni mpaka Mabwana wakubwa wa NBAA watakapokuwa tayari kukupa. Tunasikitika sana kuona nchi kama ya Uingereza ambayo imetuacha mbali mno kiuchumi na kimaendeleo kwa ujumla, ukifanya mitihani yao ya ACCA hata kama ni somo moja moja na ukafulu wanali-record na unamalizia mengine yaliyobaki. Lakini kwa NBAA ukifaulu somo moja wanalifuta.
Kwa kumalizia tunakuomba Mheshimiwa Waziri mkuu, usisubiri mpaka kutokee maandamano unda tume kuchunguza utendaji kazi wa Bodi ya NBAA kwani imekithiri kwa kufelisha watahiniwa wake kwa makusudi.