TANZIA Waziri Mkuu wa zamani nchini Italia afariki dunia

TANZIA Waziri Mkuu wa zamani nchini Italia afariki dunia

101 East

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2015
Posts
1,057
Reaction score
2,221
Screenshot 2023-06-13 044035.png


Waziri Mkuu wa zamani wa Italy na Tajiri namba mbili nchini humo ndugu Silvio Berlusconi amefariki dunia leo hii 12/06/2023

Berlusconi ambaye alikuwa ni mmiliki wa vyombo vya habari na timu ya AC Milan amefariki akiwa na umri wa miaka 86 kwa Ugonjwa wa Kansa ya Damu.

====


Waziri Mkuu wa zamani wa Italy Silvio Berlusconi amefariki dunia, akiwa na umri wa miaka 86. Tajiri huyo bilionea ambaye alikuwa anamiliki vyombo kadhaa vya habari, amekuwa akitibiwa Ugonjwa wa Saratani ya Damu.

Berlusconi alianza kutengeneza utajiri wake katika sekta ya ujenzi wa majumba kisha akaendelea kuunda mtandao wa vituo vya televisheni, akifanikiwa sana katika biashara hiyo. Wakati fulani, alijulikana kama tajiri mkubwa wa Italy.

Mwanasiasa huyo wa mrengo wa kulia alihudumu kama Waziri Mkuu katika serikali nne kuanzia mwaka wa 1994.

Berlusconi alikabiliwa na kashfa nyingi za kisiasa wakati wa maisha yake. Alijulikana kwa karamu zake mashuhuri za bunga bunga kuhusiana na kufanya ngono na makahaba, lakini kashfa hizo hazikumuzuia kujenga urithi wa kudumu wa kisiasa.
 
Waziri MKUU wa zamani wa Italy na Tajiri namba mbili nchini humo ndugu SILVIO BERLUSCON amefariki dunia Leo hii 12/06/2023
BERLUSCON ambaye alikuwa ni mmiliki wa vyombo vya habari na timu ya AC MILAN amefariki akiwa na umri wa miaka 86 Kwa ugonjwa wa kansa ya damu
Wape pole Italia
 
Huu mwaka unafukia watu wa mabebezi sana..
Boma yeee wa Italia ila zake sio za urithi
 
Alikuwa rafiki mkubwa wa Rais Gaddafi, wakati Gaddafi anashambuliwa na majeshi ya ushirika kila akimpigia simu Berlusconi akawa hapokei simu yake , Gaddafi alichoka !
 
Alikuwa rafiki mkubwa wa Rais Gaddafi, wakati Gaddafi anashambuliwa na majeshi ya ushirika kila akimpigia simu Berlusconi akawa hapokei simu yake , Gaddafi alichoka !
Wazungu Lao moja
 
Aliisha maisha yake to the fullest. Rest easy legend wa Italian politics
 
Aliposhindwa uchaguzi ambao ungempa uwaziri mkuu kwa mara nyingine, wataliano walisherehekea anguko lake kwa wiki zima😎
 
Back
Top Bottom