Waziri Mulamula: Watanzania walioko Ukraine wajitahidi waingie Poland. Wananchi msiwe na wasiwasi Serikali inafuatilia!

Hii ndiyo sababu kubwa ya serikali kukataa kutoa pasipoti kwa kila mwananchi. Serikali inajua raia wake wakipata matatizo kwenye nchi za watu, haina uwezo wa kuwasaidia.
Wajibu wa Serikali na hizo balozi huko nje ni wa nini hasa kama wanashindwa kusaidia raia wakati wa shida.
 
Tusiwe na wasiwasi wakati tunaona mbwa anapakiwa kwenye treni kupelekwa Poland mswahili anashushwa.
Sisi tuandae ubwabwa na maturubai tu
 
Hilo nalo neno...na warusi maswahiba zetu haswa.....

Wana uswahiba gani na nyinyi, mkishaona tu nchi yenye nguvu isiyohoji wizi wenu wa kura mnajifanya rafiki zenu.
 
Poland kwa sasa haiwezekani.wameondoka kuelekea Romania na Hungary.Tuwaombee ALLAH awafanyie wepesi na tutoe sadaka kwa nia ya vijana wetu wasidhurike.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Na hao wa ukraine hapo zenji mkawabwage kwa balozi wao (kama wanao) maana si watu wale
 
Waziri anasema tusiwe na wasiwasi. Waziri hazifahamu fat bombs za Warusi walizozitumia Syria.
 
nilifikiri angetuelezea hatua zilizo chukuliwa. aelezee wamefanya nn kuhakksha wanapita mipakani salama, mabalozi wetu wanasaidia vp ...nk. kufatilia anakozngmzia maana yake nn? tumeona wenzetu Ghana wakikumbatiana na watoto wao baada ya kuwasili makwao, au mambo yataji solve yenyewe!?
 
Kama mnasoma huu uzi na mpo Ukraine ,nawataka sana sana mbanane huko huko ,msije mkaingia mkenge na kutaka kurudi huku,maana hali ya maisha ni tete joto ,kama mtanisikiliza bananeni huko chini ya reli. Majuto ni mjukuu kama zako zipo hutakufa kwa kupigwa misaili maana hata huku mnakoambiwa mrudi ni kama kumepigwa nyuklia .
 
Unapotosha uma.Ulichoandika sicho alichosema waziri🐒🐒🐒

Mods please pigeni huyu mpotoshaji ban kwa manufaa mapana ya JF na kwa manufaa mapana ya uma kwa ujumla.
Your browser is not able to display this video.
 
Waingie Poland kwa usafiri gani.

Hivi ukimwambia mtu aliyeko mtwara aingie Kenya bila msaada wa kumuwezesha kufika Namanga again ataingia kweli Kenya?

Watawezaje kufika huko na watakuwa wanakula nini?
Ongezea na baridi lililopo huko !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…