Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 593
- 1,376
Wakuu,
Mtando wa ClubHouse umezuiwa kupatika nchini toka mwaka jana (2023) mwanzoni, ambapo huwezi kupata kupata huo mpakata utumie VPN.
Hii ni ukiukwaji wa haki ya kujieleza na kupata kupata habari, ni kwenda kinyume na Katiba ya Tanzania inayotoa haki ya mtu kuwasiliana na kupata habari bila kujali mipaka ya nchi.
Kifupi ni kwamba tuna haki ya kupata mitandao yote iwe ClubHouse, X, TikTok, Instagram, FB, nk kwa mujibu wa Katiba, na anayekwenda kinyume na hili anavunja Katiba na anatakiwa kuchukuliwa hatua.
Watanzania wote tumefanya kosa gani mpaka tuzuiwe mtandao wa ClubHouse? Tumekiuka sheria gani mpaka wote tuzuiwe kutumia mtandao huu? Watu karibia milioni 40 sasa hivi tunakosa mtandao huu sababu "unashughulikia" watu wachache waliovunja sheria? Unaona ni sawa kabisa, na uko proud kama Waziri kufanya ujinga huu?
Waziri Nape ni ipi justification ya wewe kufanya uvunjifu huu wa Katiba?
Unaweza kuja na kisingizio kuna watu wanatumia vibaya mtandao huo kuharibu maadili... wamevunja sheria... sasa kwanini hujawashataki wakawajibika na sisi tukajua uvunjufu huo wa sheria uliofanywa?
Yaani kikundi cha watu wachache ndio kinafanya uzuie mtandao kupatikana nchi nzima? Hapo ndio umefikiria mpaka mwisho ukaona hii ndio suluhu mujaribu ya kutatua changamoto hiyo.
Na tuseme ukweli, "Kwenda kinyume na maadili", au "Kuvunja Sheria" kwa serikali inamaanisha watu wao wamekosoa serikali hivyo wanatakiwa kudhibitiwa.
Kama uwezo ni mdogo si utafute washauri wataalamu kwenye mambo haya wakueleze ukifanya hivi unaleta athari gani na inamaanisha nini kwa Wanzania na nafasi uliyoshika?!
Kusema ukweli wewe Nape kama Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ni MZIGO kwa Taifa na AIBU kwa Rais. Hutoshei kabisa kwenye hiyo nafasi, viatu vinapwaya mno!
Mtando wa ClubHouse umezuiwa kupatika nchini toka mwaka jana (2023) mwanzoni, ambapo huwezi kupata kupata huo mpakata utumie VPN.
Hii ni ukiukwaji wa haki ya kujieleza na kupata kupata habari, ni kwenda kinyume na Katiba ya Tanzania inayotoa haki ya mtu kuwasiliana na kupata habari bila kujali mipaka ya nchi.
Kifupi ni kwamba tuna haki ya kupata mitandao yote iwe ClubHouse, X, TikTok, Instagram, FB, nk kwa mujibu wa Katiba, na anayekwenda kinyume na hili anavunja Katiba na anatakiwa kuchukuliwa hatua.
Watanzania wote tumefanya kosa gani mpaka tuzuiwe mtandao wa ClubHouse? Tumekiuka sheria gani mpaka wote tuzuiwe kutumia mtandao huu? Watu karibia milioni 40 sasa hivi tunakosa mtandao huu sababu "unashughulikia" watu wachache waliovunja sheria? Unaona ni sawa kabisa, na uko proud kama Waziri kufanya ujinga huu?
Waziri Nape ni ipi justification ya wewe kufanya uvunjifu huu wa Katiba?
Unaweza kuja na kisingizio kuna watu wanatumia vibaya mtandao huo kuharibu maadili... wamevunja sheria... sasa kwanini hujawashataki wakawajibika na sisi tukajua uvunjufu huo wa sheria uliofanywa?
Yaani kikundi cha watu wachache ndio kinafanya uzuie mtandao kupatikana nchi nzima? Hapo ndio umefikiria mpaka mwisho ukaona hii ndio suluhu mujaribu ya kutatua changamoto hiyo.
Na tuseme ukweli, "Kwenda kinyume na maadili", au "Kuvunja Sheria" kwa serikali inamaanisha watu wao wamekosoa serikali hivyo wanatakiwa kudhibitiwa.
Kama uwezo ni mdogo si utafute washauri wataalamu kwenye mambo haya wakueleze ukifanya hivi unaleta athari gani na inamaanisha nini kwa Wanzania na nafasi uliyoshika?!
Kusema ukweli wewe Nape kama Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ni MZIGO kwa Taifa na AIBU kwa Rais. Hutoshei kabisa kwenye hiyo nafasi, viatu vinapwaya mno!