Waziri Ummy: Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yanafilisi NHIF

Waziri Ummy: Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yanafilisi NHIF

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Ni kuhusu huduma za mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) - Dodoma, Septemba 1, 2022





Kuna ongezeko kubwa la idadi ya wahanga wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza nchini. Hii inaongeza mzigo wa gharama za matibabu kwa Serikali na watu binafsi. Magonjwa haya ni tofauti na mengine kwani mgonjwa hudumu nayo kwa muda mrefu.

Jukumu la kwanza la wizara ya afya ni kuwakinga watu wasiugue. Hivi sasa nchini Tanzania kuna ongezeko kubwa la wagonjwa hasa wenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza, watu hawa wanaongeza hatari ya kuufilisi mfuko wa bima ya taifa.

Matumizi na gharama za kushughulikia magonjwa haya zinazidi uwezo wa fedha zinazokusanywa na NHIF. Ni lazima sasa tuwekeze kwenye kijikinga zaidi kuliko kutibu.

Mfano, watu wapunguze matumizi makubwa ya sukari, sigara, chumvi, mafuta pamoja na kunywa pombe kupita kiasi. Aidha, watu wafanye mazoezi. Tusipopabili mbinu NHIF itaelemewa, itashindwa kutoa huduma.

Mwanzoni ilikuwa na lengo la kusaidia watumishi wa umma pekee, lakini mabadiliko ya sheria yaliruhusu watu wengine kujiunga kwa hiari. Watu hawa kwa idadi kubwa wanajiunga wakiwa wagonjwa tayari.

Mfano, Toto afya kadi ina wanachama 186,000. Fikiria visa vya baadhi ya watoto ambao siku hizi wanazaliwa wakiwa hawana njia ya haja kubwa. Gharama ya matibabu ni kama 1,200,000/= huku yeye amelipia 54,000/=. Gharama hizi ni kubwa.

Idadi ndogo ya wanachama ndiyo inafanya NHIF ikose fedha za kutosha ndiyo maana serikali inapanga kuleta sheria ya bima kwa wote ili kuondoa mzigo huu kupitia kuchangiana. Kwa sasa kuna wanufaika milioni 4.8 tofauti na laki 6 ambayo ilianza nao.

Kumekuwepo pia na udanganyifu mkubwa miongoni mwa watoa huduma kwa kutoa huduma zisizo za lazima pamoja na dawa nyingi kwa wagonjwa kisa tu wana bima. Pia, baadhi ya maafisa wa NHIF hushirikiana na watoa huduma kuihujumu NHIF kwa kuandika madeni makubwa kinyume cha hali halisi. Watu hawa hawana nia njema na mfuko huu, wanataka utajiri wa haraka hivyo sheria kali zitachukuliwa kwa watu wenye nia hii ovu.

Mfano mwingine unaoleta mzigo mkubwa kwa NHIF ni watu kubadilisha wanufaika wa mfuko huu. Baadhi ya watu huwatoa watoto ambao mara nyingi huwa hawaumwi na kuingiza mama mkwe mwenye magojwa sugu (Mfano) . Huu ni mzigo mwingine mkubwa.

Pamoja na uwepo wa changamoto zote hizi, Serikali imewatoa hofu wanufaika kwa kutoa uhakika kuwa imejipanga katika kuusimamia mfuko huu ili usife kwa kupitia upya mapendekezo ya mifumo ya tehama, kubadili taratibu za upimaji wa magonjwa (hasa kwa watu wenye magonjwa yanayo fahamika) pamoja na kuongeza idadi ya watumiaji wa mfuko huu.

Akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua ni jinsi gani bima ya afya kwa wote itawafikia watanzania wote, Waziri Ummy amesisitiza kuwa bima hii itakuwa inachangiwa kiasi kidogo tu cha pesa ili kuwafanya hata watanzania wenye hali duni waweze kunufaika. Aidha, wataweka mfumo na utaratibu rafiki wa kuwafikia kwa urahisi.

Ni asilimia 8 tu ya watanzania ndiyo wanatumia NHIF
 
Mifuko ya hifadhi za jamii ikiwemo NHIF inakuwa na hali mbaya kutokana na ukopwaji wa serikali na pia uwezekezaji usio na TIJA.Sina uhakika lakini pia nasikia NHIF ni mojawapo ya mashirika yanayolipa "handsomely".
 
Ushauri: Hosp zote zikazo patikana zina hujumu NHIF (bei tofauti na uhalisi, wanaume kujifungua, nk) wapewe kesi za Uhujumu uchumi CEO na Wakubwa wote hadi Boards. Na Hosp husika ifungiwe jumla.
 
Ukiondoa hizo changamoto alizotaja nafikiri kuna haja ya kuongelea pia ‘Mishahara na Marupurupu’ ya wafanyakazi wa taasisi. Hiyo pia ni moja ya changamoto inayofilisi mfuko.
 
Ni kuhusu huduma za mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) - Dodoma





Kuna ongezeko kubwa la idadi ya wahanga wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza nchini. Hii inaongeza mzigo wa gharama za matibabu kwa Serikali na watu binafsi. Magonjwa haya ni tofauti na mengine kwani mgonjwa hudumu nayo kwa muda mrefu.

Jukumu la kwanza la wizara ya afya ni kuwakinga watu wasiugue. Hivi sasa nchini Tanzania kuna ongezeko kubwa la wagonjwa hasa wenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza, watu hawa wanaongeza hatari ya kuufilisi mfuko wa bima ya taifa.

Matumizi ya magonjwa haya unazidi uwezo wa fedha zinazokusanywa na NHIF. Ni lazima sasa tuwekeze kwenye kijikinga zaidi kuliko kutibu.

Mfano, watu wapunguze matumizi makubwa ya sukari, chumvi, mafuta pamoja na kunywa pombe kupita kiasi. Aidha, watu wafanye mazoezi. Tusipopabili mbinu NHIF itaelemewa, itashindwa kutoa huduma.

Mwanzoni ilikuwa na lengo la kusaidia watumishi wa umma pekee, lakini mabadiliko ya sheria yaliruhusu watu wengine kujiunga kwa hiari. Watu hawa kwa idadi kubwa wanajiunga wakiwa wagonjwa.

Mfano, Toto afya kadi ina wanachama 186,000. Fikiria visa vya baadhi ya watoto ambao siku hizi wanazaliwa wakiwa hawana njia ya haja kubwa. Gharama ya matibabu ni kama 1,200,000/= huku yeye amelipia 54,000/=. Gharama hizi ni kubwa.

Idadi ndogo ya wanachama ndiyo inafanya NHIF ikose fedha za kutosha ndiyo maana serikali inapanga kuleta sheria ya bima kwa wote ili kuondoa mzigo huu kupitia kuchangiana. Kwa sasa kuna wanufaika milioni 4.8 tofauti na laki 6 ambayo ilianza nao.

Kumekuwepo pia na udanganyifu mkubwa miongoni mwa watoa huduma kwa kutoa huduma zisizo za lazima pamoja na dawa nyingi kwa wagonjwa kisa tu wana bima. Pia, baadhi ya maafisa wa NHIF hushirikiana na watoa huduma kuihujumu NHIF kwa kuandika madeni makubwa kinyume cha hali halisi. Watu hawa hawana nia njema na mfuko huu, wanataka utajiri wa haraka hivyo sheria kali zitachukuliwa kwa watyu wenye nia hii ovu.

Mfano mwingine unaoleta mzigo mkubwa kwa NHIF ni watu kubadilisha wanufaika wa mfuko huu. Baadhi ya watu huwatoa watoto ambao mara nyingi huwa hawaumwi na kuingia mama mkwe mwenye magojwa sugu (Mfano) . Huu ni mzigo mwingine mkubwa.

Pamoja na uwepo wa changamoto zote hizi, Serikali imewatoa hofu wanufaika kwa kutoa uhakika kuwa imejipanga katika kuusimamia mfuko huu ili usife kwa kupitia upya mapendekezo ya mifumo ya tehama, kubadili taratibu za upimaji wa magonjwa (hasa kwa watu wenye magonjwa yanayo fahamika) pamoja na kuongeza idadi ya watumiaji wa mfuko huu.

Akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua ni jinsi gani bima ya afya kwa wote itawafikia watanzania wote, Waziri Ummy amesisitiza kuwa bima hii itakuwa inachangiwa kiasi kidogo tu cha pesa ili kuwafanya hata watanzania wenye hali duni waweze kunufaika. Aidha, wataweka mfumo na utaratibu rafiki wa kuwafikia kwa urahisi.

Ni asilimia 8 tu ya watanzania ndiyo wanatumia NHIF
Lengo lao ni kuvuruga tu! Subirini mtaona huwezi kumkatalia mtu matibabu eti kwasababu amekula chumvi au sukari nyingi!

Punguzeni sumu na uchafu kwenye hewa na maji ya kunywa kwmfn PCBs, heavy metals, microplastics, etc; air pollution by asbestos, carbon monoxide etc. Hayo ndiyo yanachangia maradhi kama saratani za figo, mapafu, damu, nk.

Kama ni kweli watu wanakula chips za mafuta ya transformers kupata saratani ni ajabu?

Mnawakamua wananchi kwa kodi na tozo kibao halafu mnasema wale vizuri na kuwalisha watoto wao chakula bora! Inawezekana vipi?
 
Very easy equations mifuko igawanywe uwepo wa juu na wa chini,
1)mmoja uwe oriented Kwa magonjwa ya ngazi za kimsingi,
2)mwingine uwe Kwa ngazi za juu,hawa mfuko wao uwe unasaidiwa Kwa maksudi na serekali.(hapa Kwa mabosi zaidi)
@ummy_chukuwa hili.
 
Madereva afya bodaboda afya machinga afya 😀😄 kwa category kama hizi za kimchongo mchongo lazm shirika likate moto
 
Madereva afya bodaboda afya machinga afya [emoji3][emoji1] kwa category kama hizi za kimchongo mchongo lazm shirika likate moto
Huu ubaguzi wenu utawamaliza na mfuko wenu.

Bodabaoda mwenye kadi ya bima ya afya hapiganii kutibiwa hata kama haumwi kwa sababu asipo endesha boda hakuna kinacho ingia , Khali kadhalika chinga yeye kuumwa sio big isue. Kwanyinyi walipwa mishara ndio mnapohana cikumbo kwenye cordo za specialist clinic Huku mkijua kua mnaumwa mafua.

roho mbaya zabaazi ya watu huona kama nihasara kwa kutokumwa wakati wanakata mishahara Yao.
 
Back
Top Bottom