Waziri Ummy: Magonjwa yasiyoambukiza yanauelemea Mfuko wa Bima ya Afya

Waziri Ummy: Magonjwa yasiyoambukiza yanauelemea Mfuko wa Bima ya Afya

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1662020943121.png

Waziri amesema wagonjwa wa saratani wanaopata tiba za mionzi kwa Bima ya NHIF mwaka 2015/16 zilikuwa Tsh. Bilioni 9 na hadi kufikia mwaka 2021/22 gharama za malipo zimefikia Tsh. Bilioni 22.5, ongezeko ambalo haliendani na idadi ya wanachama wa NHIF.

Ameongeza kuwa huduma za matibabu ya figo mwaka 2015/16 ziliigharimu NHIF Tsh. Bilioni 9.5 na hadi kufikia mwaka 2021/22 gharama zimeongezeka na kufikia Tsh. Bilioni 35.44 ambapo wagonjwa wa Figo wameongezeka kutoka 280 hadi 2099.

Kwa upande wa magonjwa ya Moyo Waziri amesema mwaka 2015/16 NHIF ililipa Tsh. Milioni 500 lakini kufikia mwaka 2021/22 gharama za wagonjwa wa Moyo zimefikia Tsh. Bilioni 4.33.

Kuhusu Ongezeko la Wagonjwa Wanaohitaji Vipimo Maalum

Akitolea ufafanuzi kuhusu kuelemewa kwa Bima ya NHIF, Waziri amesema mwaka 2015/16 wagonjwa waliohitaji vipimo vya CT-Scan na MRI waliugharimu mfuko Tsh. Bilioni 5.43 lakini mwaka 2021/22 Mfuko umelipa Tsh. Bilioni 10.89 za vipimo hivyo.

Kutokana na gharama hizo, Waziri amewataka Wananchi kuchukua tahadhari ikiwemo kujua Afya zao mapema, kupunguza unywaji wa pombe, kuzingatia ulaji mzuri kwa kupunguza matumizi ya Sukari, Mafuta na Chumvi na kufanya mazoezi mara kwa mara.

Amekiri kuwa kama ongezeko la Magonjwa hayo litazidi kuwa juu, uwezekano wa Mfuko wa Bima wa Taifa (NHIF) kufa utakua mkubwa.

Chanzo cha kuelemewa kwa Bima Ya Afya

Waziri ameeleza kuwa baada ya Serikali kubadili Sheria na kuruhusu watu ambao sio Watumishi wa Umma kuingia kwenye Bima ya Afya, ndipo mwanzo wa tatizo la kuzidiwa Mfuko lilipotokea.

Amesema kuwa endapo Serikali ingeamua kuwahudumia Watumishi wa Umma pekee kusingekuwa na tatizo linalojitokeza sasa ambapo 99% ya wanaojiunga NHIF kwa hiari ikiwemo Toto Afya tayari ni wagonjwa, na ndio sababu Serikali inakuja na Sheria ya Bima ya Afya kwa wote ili kuongeza wachangiaji.

Ametolea mfano idadi ya Watoto waliojiandikisha kwenye Kadi ya Toto Afya inayogharimu Tsh. 50,400 imefikia watoto 186,000, na inapotokea kuna mgonjwa anayehitaji upasuaji unaogharimu Tsh. Milioni 1, Bima inalipa fedha hiyo bila kujali michango mingapi imelipiwa kupitia kadi hiyo.

PIA SOMA: Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

 
  • Thanks
Reactions: MCN
Tufanye mazungumzi na Marekani ili Tanzania liwe jumbo la Marekani na Watanzania wote wawe Wamarekani na kupata haki zote za kiraia.

Hawa tulionao akili zao zimefikia kikomo na hawapo tayari kuachia Madaraka.
 
Waziri anakosea kusema kuwa wa Hiari ndo wanasababisha hasara kwa Mfuko...

Anatakiwa aongelee deni la NHIF kwa BMH
 
Tufanye mazungumzi na Marekani ili Tanzania liwe jumbo la Marekani na Watanzania wote wawe Wamarekani na kupata haki zote za kiraia.

Hawa tulionao akili zao zimefikia kikomo na hawapo tayari kuachia Madaraka.
Tufanye mazoezi, tuache pombe na michips iliyojazana mafuta, tukifuata ushauri wake tutajiponya achana na kutaka watu watoke madarakani kwa sababu hawatatoka.
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Ukifiatilia kwa undani kupitia mfuko wa bima ya afya na msd Hakuna sababu ya uwepo wa Ummy Mwalimu Waziri wa afya.

Waziri wengine wajinsia hiyo hiyo wanatamani kuikimbia nchi kwa Hali ilivyo sasa.
2. Waziri wa ardhi na makazi yuko hoi.

3. Waziri wa uwekezaji yuko hoi.

4. Waziri wa ulinzi hajulikani aliko
5. ….
 
Mzizi wa fitna ni kijani, hakuna jinsi ummy aweza fanya. Huo mfuko na wa nssf wameshaifilisi.
 
Waziri amesema wagonjwa wa saratani wanaopata tiba za mionzi kwa bima ya NHIF mwaka 2015/16 zilikuwa Tsh. bilioni 9 na hadi kufikia mwaka 2021/22 gharama za malipo zimefikia Tsh. bilioni 22.5, ongezeko ambalo haliendani na idadi ya wanachama wa NHIF.

Ameongeza kuwa huduma za matibabu ya figo mwaka 2015/16 ziliigharimu NHIF Tsh. Bilioni 9.5 na hadi kufikia mwaka 2021/22 gharama zimeongezeka na kufikia Tsh. bilioni 35.44 ambapo wagonjwa wa figo wameongezeka kutoka 280 hadi 2099.

Kwa upande wa magonjwa ya moyo Waziri amesema mwaka 2015/16 NHIF ililipa Tsh. milioni 500 lakini kufikia mwaka 2021/22 gharama za wagonjwa wa moyo zimefikia Tsh. bilioni 4.33.

Kuhusu Ongezeko la Wagonjwa Wanaohitaji Vipimo Maalum
Akitolea ufafanuzi kuhusu kuelemewa kwa Bima ya NHIF, Waziri amesema mwaka 2015/16 wagonjwa waliohitaji vipimo vya CT-Scan na MRI waliugharimu mfuko Tsh. Bilioni 5.43 lakini mwaka 2021/22 Mfuko umelipa Tsh. Bilioni 10.89 za vipimo hivyo.

Kutokana na gharama hizo, Waziri amewataka Wananchi kuchukua tahadhari ikiwemo kujua Afya zao mapema, kupunguza unywaji wa pombe, kuzingatia ulaji mzuri kwa kupunguza matumizi ya Sukari, Mafuta na Chumvi na kufanya mazoezi mara kwa mara.

Amekiri kuwa kama ongezeko la Magonjwa hayo litazidi kuwa juu, uwezekano wa Mfuko wa Bima wa Taifa (NHIF) kufa utakua mkubwa.

PIA SOMA: Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa


Waziri home work yake kaifanyia NHIF halafu kaja kutoa statement yake na wanahabari anaendelea na mambo yake. laiti kama angetuuliza sie tungemwambia kwanza aende wanapotibiwa wagonjwa wa saratani na magnifier lens kuona kweli wamepokea Tsh. billion 9 na zimefanya nini huko. Kama kweli Ocean road wanaingiza kipato chote hiko misaada huko ya nini???

Sasa mnachukua pesa za Bima kwa ajili ya matibabu na hamtaki kulipia, ruhusuni watu wakatibiwe wanakokujua wenyewe, hapa ukimsikiliza waziri utafikiri pesa hizi zimetoka na watu wamepata huduma bora kumbe wagonjwa wametaabika na mamia wameshatangulia mbele za haki kwa usumbufu wa bima.

Waziri kabla ya press angeongea na wagonjwa kwanza taarifa yake ingekuwa bora zaidi.
 
Nini maana ya kodi? Serikali inapaswa kutoa ruzuku ya kutosha katika mfuko. Haiingii akilini serikali inakuwa na bajeti kuuubwa ya ununuzi magari halafu inalalamika gharama za bima ambazo hapo hazifiki hata bilioni 60,
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Waziri ameeleza kuwa baada ya Serikali kubadili Sheria na kuruhusu watu ambao sio Watumishi wa Umma kuingia kwenye Bima ya Afya, ndipo mwanzo wa tatizo la kuzidiwa Mfuko lilipotokea.

Amesema kuwa endapo Serikali ingeamua kuwahudumia Watumishi wa Umma pekee kusingekuwa na tatizo linalojitokeza sasa ambapo 99% ya wanaojiunga NHIF kwa hiari ikiwemo Toto Afya tayari ni Wagonjwa, na ndio sababu Serikali inakuja na Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ili kuongeza wachangiaji
Kwa maana hiyo bima kwa wote haitekelezeki kamwe!
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Tanzania nchi ya maajabu sana, eti mfuko umeelemewa kwa kuingiza wasio watumishi wa Umma

Wazungu wametoa kadi za matibabu mpaka kwa wanafunzi kwa mwaka kwa cad 902 pekee.

Akili hatuna
 

Waziri amesema wagonjwa wa saratani wanaopata tiba za mionzi kwa bima ya NHIF mwaka 2015/16 zilikuwa Tsh. bilioni 9 na hadi kufikia mwaka 2021/22 gharama za malipo zimefikia Tsh. bilioni 22.5, ongezeko ambalo haliendani na idadi ya wanachama wa NHIF.

Ameongeza kuwa huduma za matibabu ya figo mwaka 2015/16 ziliigharimu NHIF Tsh. Bilioni 9.5 na hadi kufikia mwaka 2021/22 gharama zimeongezeka na kufikia Tsh. bilioni 35.44 ambapo wagonjwa wa figo wameongezeka kutoka 280 hadi 2099.

Kwa upande wa magonjwa ya moyo Waziri amesema mwaka 2015/16 NHIF ililipa Tsh. milioni 500 lakini kufikia mwaka 2021/22 gharama za wagonjwa wa moyo zimefikia Tsh. bilioni 4.33.

Kuhusu Ongezeko la Wagonjwa Wanaohitaji Vipimo Maalum
Akitolea ufafanuzi kuhusu kuelemewa kwa Bima ya NHIF, Waziri amesema mwaka 2015/16 wagonjwa waliohitaji vipimo vya CT-Scan na MRI waliugharimu mfuko Tsh. Bilioni 5.43 lakini mwaka 2021/22 Mfuko umelipa Tsh. Bilioni 10.89 za vipimo hivyo.

Kutokana na gharama hizo, Waziri amewataka Wananchi kuchukua tahadhari ikiwemo kujua Afya zao mapema, kupunguza unywaji wa pombe, kuzingatia ulaji mzuri kwa kupunguza matumizi ya Sukari, Mafuta na Chumvi na kufanya mazoezi mara kwa mara.

Amekiri kuwa kama ongezeko la Magonjwa hayo litazidi kuwa juu, uwezekano wa Mfuko wa Bima wa Taifa (NHIF) kufa utakua mkubwa.

Chanzo cha Kuelemewa kwa Bima Ya Afya

Waziri ameeleza kuwa baada ya Serikali kubadili Sheria na kuruhusu watu ambao sio Watumishi wa Umma kuingia kwenye Bima ya Afya, ndipo mwanzo wa tatizo la kuzidiwa Mfuko lilipotokea.

Amesema kuwa endapo Serikali ingeamua kuwahudumia Watumishi wa Umma pekee kusingekuwa na tatizo linalojitokeza sasa ambapo 99% ya wanaojiunga NHIF kwa hiari ikiwemo Toto Afya tayari ni Wagonjwa, na ndio sababu Serikali inakuja na Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ili kuongeza wachangiaji.

Ametolea mfano idadi ya Watoto waliojiandikisha kwenye kadi ya Toto Afya inayogharimu Tsh. 50,400 imefikia watoto 186,000, na inapotokea kuna mgonjwa anayehitaji upasuaji unaogharimu Tsh. Milioni 1, Bima inalipa fedha hiyo bila kujali michango mingapi imelipiwa kupitia kadi hiyo.

PIA SOMA: Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

Mbona hajatuambia ghara za stationary mfano zile za 2A, 2B zinakula kiasi gani cha mfuko
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Mbona hajatuambia ghara za stationary mfano zile za 2A, 2B zinakula kiasi gani cha mfuko
Umesahau na ma file yao ya kupeleka madai yalivyomabaya Sasa.
Yaani aliyepewa order ya kuyatengeneza hakuna kitu
 
Mfuko ufumuliwe,wanaostahili wawe watumishi tu.au kuwe na mifuko miwili,ya watumishi na wasio watumishi.
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Mizigo imeongezeka maladufu Tz maana Haina hata inachojua kuhusu Nchi na wananchi
 
Mfuko ufumuliwe,wanaostahili wawe watumishi tu.au kuwe na mifuko miwili,ya watumishi na wasio watumishi.
Tatizo halipo kwa mfuko , ni serikali hailipi madeni unayodaiwa na mfuko huo
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Back
Top Bottom