Mshangai
JF-Expert Member
- Feb 16, 2008
- 468
- 1,086
Usajili wavyuo vingi tarehe za mwisho zinakaribia na kwa vile masharti ni kuwa mpka ada ilipwe zaidi ya nusu wengi watashindwa kujisajili kwa wakati na kupoteza nafasi hii ya kusoma kwa vile hawakupata mikopo.
Taarifa ya kukosa mikopo imewafikia wazazi muda mchache kabla ya vyuo kufunguliwa na kama hali halisi ya maisha ya Watanzania inavyofahamika sio rahisi mtu kumkuta na akiba ya kuweza kutosheleza dharula kama hizo.
Ingekuwa ni jambo la hekima vyuo vikawapokea wanafunzi wote wanaojisajili hata kama hiyo ada aliyonayo haifiki nusu ya ada nzima halafu wazazi wakaendelea kudaiwa na kuwabana wakati wa mitihani kuliko kushindwa kujisajili kabisa.
Nimeona chuo kama Ardhi sharti hilo wamelipa uzito na vijana wengi waliokosa mikopo na wazazi wao hawataweza kulipa kabla ya hiyo tarehe 18/10/2013 waliyoiweka watakosa fursa hiyo.
Huu ni wakati wa kutumia hekima sana hasa kwa hivi vyuo vya Umma,si vema serikali ikaonekana kama inamalengo ya kukomoa raia wake. Maana kama mtu umemnyima haki yake ya mkopo,basi mpe hata nafasi ya kuweza kutafuta atakachoweza kulipa
Bado vyuo vinaweza kuwabana wakati wa mitihani na ada ikalipwa.
Taarifa ya kukosa mikopo imewafikia wazazi muda mchache kabla ya vyuo kufunguliwa na kama hali halisi ya maisha ya Watanzania inavyofahamika sio rahisi mtu kumkuta na akiba ya kuweza kutosheleza dharula kama hizo.
Ingekuwa ni jambo la hekima vyuo vikawapokea wanafunzi wote wanaojisajili hata kama hiyo ada aliyonayo haifiki nusu ya ada nzima halafu wazazi wakaendelea kudaiwa na kuwabana wakati wa mitihani kuliko kushindwa kujisajili kabisa.
Nimeona chuo kama Ardhi sharti hilo wamelipa uzito na vijana wengi waliokosa mikopo na wazazi wao hawataweza kulipa kabla ya hiyo tarehe 18/10/2013 waliyoiweka watakosa fursa hiyo.
Huu ni wakati wa kutumia hekima sana hasa kwa hivi vyuo vya Umma,si vema serikali ikaonekana kama inamalengo ya kukomoa raia wake. Maana kama mtu umemnyima haki yake ya mkopo,basi mpe hata nafasi ya kuweza kutafuta atakachoweza kulipa
Bado vyuo vinaweza kuwabana wakati wa mitihani na ada ikalipwa.