Waziri wa michezo tunataka kuona hatima ya Serengeti Boys

Mzalendowadamu

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2016
Posts
218
Reaction score
318
Sote Watanzania tunashuhudia kiwango vya vijana wa timu ya mpira kwa vijana wa until wa miaka 17 au Serengeti Boys. Katika uchungu wangu kikosi cha sasa ni bora na kimesheheni vipaji pengine kuliko vikosi vya awali.

Jambo la kusikitisha ni kwamba vipaji hivi vitakwenda kupote kama ambavyo vilipotea vipaji vya walio tangulia. Ni aibu kwa nchi kushindwa kuwa na Academy ya Taifa ambayo inaweza kuwatumia hawa vijana ili wakae kwa pamoja kwa Muda Mrefu na kutafutiwa mwalimu.

Lakini kama hilo halitoshi, ni jambo la ajabu pia kwamba vijana hawa watakosa kupata Academy za nje ya Africa ambazo wanayo miundo mbinu ya kukuza vipaji hivi. Tunazo Barozi kila kona ya Dunia na tunaweza kutumia hizi Barozi kutafuta Academy na kuwaunganisha hawa vijana.

Ni wakati sasa tujue Mipango ya wizara ya Michezo chini ya Mh. Mwakyembe, inayo mipango gani juu ya hawa vijana. Imetokea wakati sasa Watanzania tuungane kutoka timu bora ya Taifa.

Mh. Waziri tunataka majibu kwa vitendo. juu
 
Nenda TFF wakupe mpango mkakati wao.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii nchi ina vipaji vingi sana vinafia mtaani

Haikii akilini nchi yenye watu zaaidi ya mil 40 kukosa wanandunga 12 wanao ujua mpira sawa sawa kutupa raha mashabiki wasoka.

Na kuzidiwa na nchi kama za ireland zenye watu laki 2 sjui hko
Mipango mibovu ,mikakati mibovu
Viongozi wanawazia chakula cha watoto wao kuliko kutengeneza kilocho bora kwa taifa

Kwa taarifa tu hii sio serengeti boys bora kuliko zote zilizopita
Hii ni Serengeti boys iliyo onekana zaidi kutokana na KUKUA na kuendelea lwa technolojia na kuonesha Mechi zao na walio wengi wamepata kuwaona ila walianza mdaa sana kuwa na soka bora

Vizazi vingi sana vyenye mafundi vimepita ila chaajabu wabakuwa ila raifa starts ni ILE ILE

Kuna mda najiuliza Kwani ukishaingia timu ya Taifa ndio huwezi kutoka mpaka uamue au walio kuweka waamue hata kama kuna vupaji na kizazi chenye uwezo zaidi kipo??

Wamepita Serengeti boys wengi Sana,
Lakini Leo wote hawajulikani walipo yani ni pumbapumba tuuu!
Watu wanalazimsha tuu kung'ang'ania wazee wasio jiweza wakati vijana wanao jua wapo
Trust me hawa watoto 2020 ndio wanatakiwa waanze kuitumikia nchi ipasanyo lakin cha ajabu hauta msikia hata mmoja.
#Nchiyamatumbo
#kichwachamwendawazimu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi serengeti boys hii na ile ya kina ramadhan kabwili..dickson job...kibabaje ipi nzur zaidi... na ipi ni nzuri ya ile ilio tolewaga kwenye mashindano kwa kumchezesha mchezaji mkubwa na yule mchezaji alichezaga na yanga jina sikumbuki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa vijana kwa miaka miwili ya karibuni wameonyesha soka safi lakini cha kushangaza wanaishia Ndanda na Stand United, Cuz wamekosa mawakala na mfumo mbaya wa wachumia tumbo wa pale tifutifu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera sana kwa mada hii ya kizalendo
 
Hawa vijana kwa miaka miwili ya karibuni wameonyesha soka safi lakini cha kushangaza wanaishia Ndanda na Stand United, Cuz wamekosa mawakala na mfumo mbaya wa wachumia tumbo wa pale tifutifu

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanapotea tu wengine wakifaulu wnaenda chuo wanaacha mpira! Sasa soko limehamia Burundi! Wanakimbilia 'cheap labour' wanaacha vipaji vinakufa sababu vijana hawataki kutoa 10% wanajielewa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…