Waziri wa Mkapa amshukia Kikwete ataka CCM imtose 2010

Wadau tusipoteze Jasho letu na watu CCM....Kwanini hatubadili mwelekeo...?

Sofia Simba ameshawapa data hakuna msafi..mnataka nini? walio wachafu zaidi?
 
..Mateo Qares namkubali kama mtu asiyekuwa na uoga kutetea lile analoliamini.

..alikuwepo hata kwenye lile kundi maarufu la G-55.

..wananchi wa Mbeya wanakumbuka kama mtu asiyependa majungu ktk kazi.


Siuo kutopenda majungu tu bali alikomesha tabia ya majungu, watu walienda pale ofisini kwa mambo ya maana na sio majungu.

Pili kiwango cha elimu wakati wake kilipanda hadi asilimia 75 na mkoa uliongoza kitaifa.

Lakini kikubwa ni mtu asiye mnafiki, TAKUKURU waliwahimwalika na kumtayarishia hotuba iliyojaa majisifu ya jinsi walivyowashughulikia wala rushwa, yeye akaiweka pembeni na kuwamegea vipande vyao.

Aliwaeleza TAKUKURU kuwa wanawaonea masikini watumishi wa ngazi za chini kama trafiki, manesi, makarani wa mahakama na watendaji wa vijiji na kuwaogopa wakubwa.

Kama sikosei alikuwa kiongozi wa kwanza kukosoa utendaji wa TAKUKURU na kubainisha kuwa viongozi wa juu serikali wakiwemo mawaziri, wakuu wa mikoa, waziri mkuu na rais ndo wenye dhamana ya mikataba na huko kwenye rushwa, hivyo aliwaelekeza waende huko badala ya kufukazana na dagaa.

Hivyo sishangai kumsikia akipingilia msumari kiasi hicho, hasemi kwa sababu yuko nje ya serikali, hata wakati yumo serikali aliikosoa serikali wazi wazi.
 
Swali langu kwa kina mama,2005 walisema JK ni kijana na handsome wakamchagua,miaka mitano inakaribia kwisha wote tutakubaliana kuwa uhandsome wake umwpungua(kama sio kuisha) na Uzee unaanza kumkaa vyema,nini kitakuwa kigezo cha kumpa 2010?
 
Sijashangaa sana mtazamo wa Mathew Qares kwa sababu niliutarajia! Huyu bwana katika kampeni za kugombea uraisi za mwaka 2005 alikuwa katika kambi ya waziri mkuu mstaafu Frederick Sumaye, pamoja na mwenzake Stephen Mashishanga, kwa hiyo hawa wawili ni majeruhi wa siasa za makundi za sisiem na ndio sababu wao walikuw watendaji wa mwanzo kabisa wa utawala huu kuondolewa madarakani kama wakuu wa mikoa mara baada ya JK kushika madaraka.
JK ana kazi sana ya kutibu makovu haya, vinginevyo critisisms kama hiz hazitakoma!

If you cant beat us join us!
Qares please join them
 
Ikiwa kweli wanamaanisha ingekuwa bora zaidi ila sidhani kuwa wanapambana kutoka ndani ya mioyo yao kupambana na ufisadi na utawala mbovu wa serikali iliyopo madarakani.tATIZO LAO NI KUTOPEWA NAFASI KWENYE SERIKALI MANAKE WASINGEJIUZULU KAMA WANGEKUWA MAWAZIRI
 
MIAKA 48 YA UHURU: MKULIMA KATIKA JEMBE LA MKONO NA TUMAINI LA KILIMO KWANZA

Na Subira Kaswaga

Ni miaka 48 ya uhuru wa Tanganyika tangu tulipojitwaa kutoka katika mikono ya wakoloni iliyojaa ukatili, unyonjaji na udhalilishaji na kuanza kujitawala wenyewe katika ardhi yetu.


Wakati wa ukoloni watanzania tulidhalilishwa na kuchukia ngozi nyeusi kutokana na unyama uliofanywa dhidi yetu na hivyo wote tuliamini kuwa mzungu ni adui na kujipa tumaini la kupata haki zetu pale madaraka yatakapokuwa chini ya mweusi.

Bila kujua kama tunachochea moto ndani ya chumba tulicholala na leo wote tunashuhudia ukatili unaofanywa dhidi yetu na viongozi wasiojali utu wa watu wao waliowaweka madarakani.

Baada ya uhuru mwalimu alitaka haki sawa na kuanza na sera ya ujamaa na kujitegemea huku akisistiza kilimo kwa maendeleo ya taifa kutokana na kuwepo kwa ardhi safi yenye ruruba na nguvukazi ya kuitumia.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo katika tovuti Tanzania ina wastani wa hekari 43 milioni zinafaa kwa kilimo, ambazo zinaweza kulisha nusu ya Bara la Afrika zikitumiwa vizuri.

Hata hivyo ni wastani wa hekari 6.3 milioni tu zinazolimwa kila mwaka tena na wakulima wadogo wanaotumia zana duni. Mashamba ya wakulima wakubwa sio mengi na yanachukua silimia nne tu ya mashamba yote nchini.


Kilimo ambacho ndio uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania toka miaka ya 1960 kiko katika hali mbaya na mchango wake hivi sasa ni asilimia 50 tu ya pato la taifa ingawa sekta ya kilimo inaajiri asilimia 70 ya nguvukazi yote ya Tanzania.

Kwa mujibu wa takwimu za Serikali pato la jumla la kilimo linaongezeka kwa asilimia 3.5 kwa mwaka toka 1981

Kilimo bado kinashikilia nafasi kubwa kama uti wa mgongo wa taifa letu kutokana na 70% ya watanzania masikini kuendelea kutegemea kilimo kwa ajili ya kupata chakula na si katika uingizaji wa pato la taifa.

Viongozi wameshawatupa wakulima kwa kuwaongezea kodi kila mwaka na kuwahadaa kwa kauli za kisiasa za kuwapa matumaini ya kuwasaidia katika miaka 48 ya uhuru.

Ikiwa ni miaka 48 tangu tujitawale bado mkulima anaendelea kutumia jembe la mkono na kulima kwa ajili ya tumbo na si maendeleo ni lini viongozi wataacha porojo za kuwahadaa wakulima?

Leo hii katika kipindi kifupi baada ya kudangawya na maisha bora kwa kila mtanzania, sasa tunawageukia wakulima kwa kauli ya kilimo kwanza.

Kilimo kwanza utabaki kuwa msemo kama ulivyokuwa ule wa maisha bora kwa mtanzania na baadaye kuambulia maisha magumu kwa kila mtanzania.

Ikiwa hata nusu ya ardhi tuliyonayo hatuitumiii kwa kilimo kwa muda wa miaka 48 sasa na kuiuza kwa wawekezaji ambao kila uchao tunashuhudia madhara zaidi ya faida kwa wazalendo.

Muwekezaji wa mgodi wa North Mara (Barick) amesababisha wakazi wa kijiji jirani kushindwa kulima kwa sababu ya sumu kali iliyopo katika ardhi inayotokana na kemikali kali kutoka viwandani.

Zaidi ya miaka mitatu sasa wakazi hao wanalalamika kutokana na ukame na mifugo yao kufa kutokana na kutumia maji ya sumu yanayotoka kiwandani hapo.

Lakini bado viongozi wetu manakaa kimya na kuendelea kujitanua kwa kununua mashangingi, kujiongezea mishahara na kutamba kwa mbwembwe kwa kuweza kutumbua kodi za wananchi katika kipindi cha miaka 48 ya uhuru wa bendera.

Wakazi hao masikini ambao msingi wa maisha yao ni kilimo leo wanafarijiwa katika miaka 48 ya uhuru wa Tanganyika na kilimo kwanza huku ardhi yote ikiwa imejaa sumu ambapo hakuna mmea utakaoweza kustahamili.

Ni vema kujiuliza hawa wakulima watalima eneo gani ikiwa eneo wanaloishi amepewa mwekezaji anayeua mifugo, na wakazi wa kijiji kutokana na ukame, na sumu kali anazomwaga ardhini.

Leo hii tena wanaitwa kupewa tumaini lisilokuwa na ukweli kwakuwa wao katika miaka 48 ya uhuru wanasherekea uwezo wa kustahamili mazingira magumu yanayoletwa na muwekezaji.

Tutajisifu sana na amani na kilimo kwanza, lakini ukweli ni kuwa 70% ya watanzania hawana amani kutokana na maisha magumu na ukoloni wa watanzania wenmyewe katika miaka hii 48 ya uhuru.

Miaka hii 48 tunayoshangilia ni dhahiri kuwa watanzania hawako huru kutokana na kukabiliwa na ugumu wa maisha, dharau, unyonyaji na ukatili unaofanywa na viongozi wasiojali utu wa watu.

Katika hili tujifunze mengi na tukatae kushangilia tunapotakiwa kulia ni vema tuwe wazi kuliko kuuficha ukweli kwa kusema “miaka 48 ya uhuru kwa tajiri na utumwa kwa myonge”.
 
ndugu zangu hakuna lolote wao walikuwa mawaziri siku za nyuma ndio wameifika hii nchi hapa tulipo ,haya madhara ya sasa ni pamoja na mipango na misingi mibovu ya serekali zilizopita.kwani mambo yalifanywa mengi sana ila ilikuwa sio rahisi kupata taarifa .

mfano mzuri kipindi cha mkapa yalifanyika madudu mengi lakini mkapa alikaripia waandishi na kuwa mbali na vyombo vya habari pamoja na yeye kuwa na background ya journalism alijua akivisogeza karibu vitajua hayo madudu.

na hapakuwa na mtu aliethubutu kuongea kwenye mikutano ya hadhara kuikosoa serikali.
sasa huyu amekuza demokrasia kwa kuwapa watu uhuru wa kuongea na kutoa mawazo yao,vyombo vya habari nanvyo vikapewa mwanya mkubwa sana wa kuikosoa serikali itakavyo na yeye rais kukaa kimya.huo ndio utawala bora ni accumulation ya mambo na sio jambo moja kama hao wajinga kina mateo wanasema barabarani.

dhana ya demokrasia na utawala bora ni pana haitaki serikali ku act kwa vile wananchi ,au watu fulani fulani wenye chuki zao wamesema.
tunajua historia zao vizuri na manyangu yao waliyofanya kipindi chao.
mamlaka ya raisi ni makubwa sana akiamua hao watu wanaopiga kelele barabarani wasikojoe kwa mwezi mzima ila wajikojolee anaweza ,na kukaa kimya hakumaanishi kushindwa au kuogopa watu.

acheni kumkejeli raisi ,muda wenu ulikuwepo na mlishindwa kazi kutukoregea tu nchi yetu,kila kukicha mnatuletea hili kesho hili,yaani ingekuwa ruhusa yangua hao wazee wote wanaopiga kelele barabarani kila kukicha ningewafungulia home)wakakaa huku wakapigia kelele huko sisi vijana tukaendesha nchi yetu.

nashangaa mara huyu hii nchi hii nchi wakati wao kulikuwa hakuna uhuru wa kusema ukisema unafichwa ndani unaonekana baadae kama kina mzee mtei wanavyosimulia yaliwakuta wakiwa vijana lakini hawakuthubutu kusema wakati ule wanasema leo na wameshazeeka.

kikwete ongoza nchi na hatumwoni so far wa kusema wewe haufai
 
Pamoja na habari nzuri ila simuamini kabisa huyu mwandishi.nafahamu kuwa sio muadilifu na najua ameandika stori hii kwa sababu zake nyingine wal si za kiuandishi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…