Wazo Bora zaidi juu ya kushuka kwa Shilingi (Tsh)

American nigga

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2014
Posts
673
Reaction score
974
Kipindi cha zamani kabisa, enzi za mwalimu, "Tsh" ilikuwa na thamani kubwa, kiasi kwamba mtu aliweza kujenga nyumba bora na ya kifahari kwa Tsh 800 Tuu! Ila kutokana na hawa viongozi wetu na mfumo wao mbovu, Mambo yalibadilika Ghafla na Tsh kuanza kuporomoka kwa kasi kama maporomoko ya Mto Ruaha, kwa Usd na Currents nyingine. Hali hiyo iliendelea ila kwa sasa hali imezidi kuwa mbaya zaidi, Leo ikitokea mtu aliyefariki mwaka 1970 akafufuka na kuja Leo hapa Tanzania atashtuka mno kwa maisha yalivyo ghali na huenda akakimbilia hukohuko alikotoka (akhera).

Kwa jicho la Tatu suala la Tsh kurudi na kuja kuwa kama mwanzo ni ndoto za mchana kweupe kabisa!
Kipi kifanyike ili kunusuru Maisha ya Watanzania na Hii sarafu yetu inayoporomoka kila kukicha!!?
Nchi kama vile Congo, Zimbabwe na nyingine nyingi zilipoona Hela yao imeshuka Thamani kwa kiasi kikubwa waliamua kuteketeza na kuipoteza hela yao kisha kuanza kutumia USD" Hivyo nikiwa kama raia nawashauri wabunge na viongozi wa juu kupeleka muswada Bungeni juu ya hili, TUIPOTEZE TSH KISHA TUTUMIE USD maana kuja kuzinduka baada ya miaka 20 mbele na kuanza kutumia USD tutakuwa tumechelewa ni bora tukaanza sasa, maana Tsh kurudi thamani yake za miaka 40 iliyopita ni sawa na Vipande vya nyama ya Nguruwe kuliwa Msikitini! Haiwezekani, Never kwa hii Tanzania ninayoijua mimi.
 
Nadhani inabidi tuangalie sababu ya tsh kuporomoka against USD.
Unachokula lazima ukizalishe na kama uzalishi lazima ukigalamie kukinunua, Tanzania kwa kiasi kikubwa tunakula tusichozalisha hivyo tunaagiza nje hata vitu tunavyoweza kazalisha wenyewe. Sasa kama tunaagiza nje bidhaa hatuwezi kwenda ulaya kununua bidhaa kwa tsh, lazima tuwe na USD. Kwa hiyo lazima tubadilishe tsh yetu iwe ktk USD ili tuweze kuagiza vitu kutoka ulaya kimsingi tunanunua USD kwa kutumia tsh.
Kama hatuwezi kuizalisha USD itaadimika kwenye masoko yetu wkt mahitaji ni makubwa lazima itapanda thamani tu. Ni kama bidhaa nyingine ikiadimika inapanda bei.
Suluhisho:
Tuzalishe bidhaa na huduma tunavyoweza tukauze nje ili tupate USD nyingi kwenye masoko na bei yake itashuka kinyume na hapo ni stori na suluhisho la muda mfupi.
Tubadilike na tujaribu kufikiria viwanda vidogo vidogo, tuongeze thamani ya mazao yetu tufikirie na masoko ya nje sio kaliakoo peke yake kwenye madalali feki. Wakenya wananunua bidhaa zetu kwa tshs wanapeleka kwao wanapaki vizuri alafu wanauza nje wanapata USD uchumi wao unakua. Sisi kwa uvivu wetu wa kufikiri, kujituma na kuunganisha nguvu tunauzia mashambani hivyo tunabaki na tshs yetu ile ile sasa kwanini isishuke thamani?
 
Mimi Nimemuelewa Sana Lusinde Alisema "Tukitaka Shilingi yetu ipande thamani dhidi ya Sarafu za Nje,basi tuondoe sura za wanyama kwenye fedha zetu,uchumi wetu utakuwa mzuri endapo tukiweka sura ya Mwalimu Nyerere au Karume".

 

Attachments

Mimi Nimemuelewa Sana Lusinde Alisema "Tukitaka Shilingi yetu ipande thamani dhidi ya Sarafu za Nje,basi tuondoe sura za wanyama kwenye fedha zetu,uchumi wetu utakuwa mzuri endapo tukiweka sura ya Mwalimu Nyerere au Karume".


Hahahaaa huu ushauri kiboko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…