Wazo kubwa la kibiashara 'Entertainment Group'

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kuna hili wazo naliweka mezani; kwa nini tusianzishe kundi litakaloitwa 'Entertainment Group'?

Hili kundi liwe na wanachama angalau 100,000 ambapo kila mmoja atachangia shilingi 2000; ikiwa na maana ya kuwa kutakuwa na pato la Tsh. 200,000,000/=, iwe kwa event moja ama zaidi, kutokana na muongozo utakao kuwepo.

Hili kundi, kazi yake ni kuleta wasanii kutoka popote duniani, na kufanya marketing ili watu wengi waweze kushiriki tamasha hilo, na faida itakayopatikana, wagawiwe wanachama.

Wakuu, mnalionaje hili wazo?​
 
Hili wazo kama nakupa marks nakupa 15% ya 100%.

Wanachama 100,000 ni wengi mno na wote umewapa nguvu sawa. Mnaweza fanya vikao mwaka bila kuwa na hatma ya mjadala. Kampuni huwa zinatoa hisa unakuta wamiliki wa kampuni ni 200,000 ila kati yao kuna watu wanne wanamiliki zaidi ya 60% ya kampuni. Hao wanne ndio wanasikilizana. Simba haiwezi acha kumsikiliza Mo mwenye 49% ikamsikiliza Fundi baiskeli aliyechanga elfu ngapi kwenye App.
Kama hutaki iwe kampuni basi ikiwa kikundi kitakuwa kigumu mno kuongozwa.

Wazo lako lingekuwa na maana kidogo kama linahusisha watu wachache watakaoweka hela nyingi. Kawaida ya shareholders wa hela nyingi huwa wanaijua hiyo sekta au hufanya consultation. Na hawajali faida ya haraka
 
Halafu watu wasipoingia kwnye tamasha pesa za wanachama unarudishaje, Aisee hili wazo lako bado hujachanganua ila kwa ishu za entertainment nichek
Watu watakaochangia sh. 2000 inakuwa kama hisa, ila wapo watakaotoa zaidi; kuhusu watu kutoingia au kuingia, kutakuwa na wataalamu wa hayo maeneo ambayo ni kazi yao, pia watu wa 'risk management' watakuwepo.
 
Nimekupata mkuu, watu wanavyozidi kuwa wengi, inakuwa ngumu katika 'management' ila wakiwa wachache, inamaana hao wachache watoe mzigo wa kutosha, kwa hiyo wazo litakuwa limeamia kwa matajiri na si kwa masikini wenye kipato labda cha laki 5 kwa mwezi​
 
Hapo shida ni kwa waweka hazina tu. Maana kila mtu atataka kuwa mhasibu. Piga jesabu buku 2 kila mwezi kwa mwaka kwa hao watu, huo si utajiri kbsa?
Au ndo yale ya Mange kimavi?🤔
 
Hapo shida ni kwa waweka hazina tu. Maana kila mtu atataka kuwa mhasibu. Piga jesabu buku 2 kila mwezi kwa mwaka kwa hao watu, huo si utajiri kbsa?
Au ndo yale ya Mange kimavi?🤔
Nini kifanyike mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…