Askarimtu
JF-Expert Member
- Sep 7, 2019
- 277
- 185
Paap...!
Nimeamka asubuhi nikawaza jinsi tu waafrika tunavyojidharau. Nikasema kwa nini tusiwakomeshe wazungu siku moja?? Tuchukue madini yetu, tutumie kama pesa...yaani nipe dhahabu nikurudishie chenchi almasi tatu. Toa Tanzanite, nikurudishie rubi 100. Kwanza tunaishije masikini, si tujianzishie tu masoko ya barter trade? Una unga kilo 100 lakini huna mboga, mjinga wewe!!! Njoo nikupe kilo 20 za nyama ya mbuzi, unipe kilo 50 za unga. Biashara ni makubaliano. Nikiwa mkubwa nitaanzisha barter trade upya, no...nikimaliza shule....no...nikirudi Tanzania.Website zitakuwa nyingi tu, hatuwezi kulala na njaa bhana kizembe wakati sote ni ndugu!
Lakini baadae nikaona ni wazo la kijinga.
Ila nikafikiria, hivi hawa watu waliotuibia historia yetu na kufanya ya kwao nitawapikuje?? Kisasi sipendi, ila nataka watoto wangu wafahamu kuwa vitu vikubwa vyote vilitoka Afrika, Afrika itaendelea kutajirisha na kulisha dunia nzima mpaka nchi ya sasa itakapopita. Nataka nibadilishe zile movies zote zenye historia yetu na kufanya ziigizwe upya na waafrika. Nani atanipa bajeti ya bilion 1 za kitanzania nikamilishe ndoto yangu?? Looh...! Ujinga sometimes ni kichangamsha kichwa tu, kwani hukuwahi kusikia kuwa akili nyingi huondoa maarifa??
Jioni imefika, nipe wewe wazo lako la kijinga ulilolifikiria ulipoamka leo ukiachana na wazo la kunywa supu ya kongoro!!!
Nimeamka asubuhi nikawaza jinsi tu waafrika tunavyojidharau. Nikasema kwa nini tusiwakomeshe wazungu siku moja?? Tuchukue madini yetu, tutumie kama pesa...yaani nipe dhahabu nikurudishie chenchi almasi tatu. Toa Tanzanite, nikurudishie rubi 100. Kwanza tunaishije masikini, si tujianzishie tu masoko ya barter trade? Una unga kilo 100 lakini huna mboga, mjinga wewe!!! Njoo nikupe kilo 20 za nyama ya mbuzi, unipe kilo 50 za unga. Biashara ni makubaliano. Nikiwa mkubwa nitaanzisha barter trade upya, no...nikimaliza shule....no...nikirudi Tanzania.Website zitakuwa nyingi tu, hatuwezi kulala na njaa bhana kizembe wakati sote ni ndugu!
Lakini baadae nikaona ni wazo la kijinga.
Ila nikafikiria, hivi hawa watu waliotuibia historia yetu na kufanya ya kwao nitawapikuje?? Kisasi sipendi, ila nataka watoto wangu wafahamu kuwa vitu vikubwa vyote vilitoka Afrika, Afrika itaendelea kutajirisha na kulisha dunia nzima mpaka nchi ya sasa itakapopita. Nataka nibadilishe zile movies zote zenye historia yetu na kufanya ziigizwe upya na waafrika. Nani atanipa bajeti ya bilion 1 za kitanzania nikamilishe ndoto yangu?? Looh...! Ujinga sometimes ni kichangamsha kichwa tu, kwani hukuwahi kusikia kuwa akili nyingi huondoa maarifa??
Jioni imefika, nipe wewe wazo lako la kijinga ulilolifikiria ulipoamka leo ukiachana na wazo la kunywa supu ya kongoro!!!