Wazo la kuanzisha 'Ujamaa shop & Eqn x'

Wazo la kuanzisha 'Ujamaa shop & Eqn x'

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Ujamaa shop
Kama una mtaji mdogo, unaweza kufanya biashara hii huku ukijitengenezea 'brand' 'ujamaa shop'

  • Tembelea vijiji 2 au zaidi kutokana na nafasi uliyonayo
  • Anzisha maduka madogo madogo yenye muonekano wa gende; yatakayokuwa yanauza vitu vidogo vidogo kama vile vile; kiberiti, sukari ya kufunga, vitunguu, majani ya chai, viazi mviringo, dagaa, tangawizi, iliki n.k
  • Tumia hayo maduka kukusanya bidhaa kijijini na kuleta mjini, mfano kuku, mayai, mbuzi, sungura n.k
  • Unaweza kuanza na viduka 5, vitakavyotofautiana kwa umbali usiopungua kilomita 2 au 3.
  • Tafuta kijana wa kijijini hapo, ndio umuajiri kwenye hilo duka. Kwa sababu wewe ushakuwa mwekezaji wa eneo hilo, na unatoa ajira kwa vijana/wazawa.
  • Ongeza vijiduka vingi vingi, kutokana na uwezo wako, kwa vijiji mbalimbali.
  • Tathmini hali ya soko, na tumia njia mbalimbali ili kuongeza mauzo.
  • Fanya ukaguzi kwa kutengeneza mfumo, ili vijana wasikuibie sana.
Baada ya kufanikisha hayo, njoo mjini tupige bia usiku na mchana, huku kule vijijini vijana wakikufanyia kazi.
 
Ujamaa shop
Kama una mtaji mdogo, unaweza kufanya biashara hii huku ukijitengenezea 'brand' 'ujamaa shop'

  • Tembelea vijiji 2 au zaidi kutokana na nafasi uliyonayo
  • Anzisha maduka madogo madogo yenye muonekano wa gende; yatakayokuwa yanauza vitu vidogo vidogo kama vile vile; kiberiti, sukari ya kufunga, vitunguu, majani ya chai, viazi mviringo, dagaa, tangawizi, iliki n.k
  • Tumia hayo maduka kukusanya bidhaa kijijini na kuleta mjini, mfano kuku, mayai, mbuzi, sungura n.k
  • Unaweza kuanza na viduka 5, vitakavyotofautiana kwa umbali usiopungua kilomita 2 au 3.
  • Tafuta kijana wa kijijini hapo, ndio umuajiri kwenye hilo duka. Kwa sababu wewe ushakuwa mwekezaji wa eneo hilo, na unatoa ajira kwa vijana/wazawa.
  • Ongeza vijiduka vingi vingi, kutokana na uwezo wako, kwa vijiji mbalimbali.
  • Tathmini hali ya soko, na tumia njia mbalimbali ili kuongeza mauzo.
  • Fanya ukaguzi kwa kutengeneza mfumo, ili vijana wasikuibie sana.
Baada ya kufanikisha hayo, njoo mjini tupige bia usiku na mchana, huku kule vijijini vijana wakikufanyia kazi.
Mkuu km nakuelewa hv, heb fafanua kdg hapo namna ya kukusanya mazao toka huko kijijini kwa kutumia hilo genge hapo yan how?
 
Mkuu km nakuelewa hv, heb fafanua kdg hapo namna ya kukusanya mazao toka huko kijijini kwa kutumia hilo genge hapo yan how?
Mara nyingi vijijini, mzunguko wa fedha huwa ni mdogo, ila wana bidhaa kama mifugo,mazao n.k Duka lako litatumika kama 'centre' ya ununuzi wa bidhaa zao kwa bei nafuu, huku ukivileta mjini kwa mauzo. Pia 'centre' yako inaweza kuwasaidia kufanya mihamala kwa wale wanaotumiwa fedha na ndugu na jamaa.
 
Back
Top Bottom